Eco- Scope Foundation

Eco- Scope Foundation ESF is Non profit, non-governmental voluntary and non- partisan organization registered under NGO Act

As we celebrate the hardworking men and women who feed our nation  we must take note that; agriculture remains the backb...
08/08/2026

As we celebrate the hardworking men and women who feed our nation we must take note that; agriculture remains the backbone of Tanzania’s economy, contributing nearly 26% of the country’s GDP and providing livelihoods for more than 70% of the population. Its importance goes far beyond food production, it is a key driver of economic growth, poverty reduction and national development.

To unlock the sector’s full potential, we must strengthen local systems that enable farmers to access reliable markets, affordable financing and modern agricultural technologies. Investing in these areas will empower farmers, boost productivity also help agriculture continue to play a leading role in reducing poverty and creating sustainable economic opportunities.

Government and all stakeholders have a shared responsibility to consider agriculture as a strategic pathway for addressing youth unemployment. At the same time, we must safeguard the rights and interests of farmers, fishers, and livestock keepers, ensuring they receive fair opportunities and benefits throughout the entire agricultural value chain.

Usafirishaji haramu wa binadamu ni janga la kidunia linalohitaji ushirikiano wa kila mmoja wetu. Eco Scope Foundation in...
30/07/2026

Usafirishaji haramu wa binadamu ni janga la kidunia linalohitaji ushirikiano wa kila mmoja wetu. Eco Scope Foundation inatoa wito kwa Serikali, sekta binafsi, wadau wa maendeleo na jamii kwa ujumla kuendelea kuunga mkono upatikanaji wa ajira salama na kuwekeza kikamilifu katika kujenga mifumo imara ya ulinzi, kinga na fursa za kiuchumi ili kuzuia usafirishaji haramu wa binadamu.

Pamoja tunaweza kukomesha usafirishaji haramu wa binadamu na kulinda utu wa kila mtu.

Usafirishaji haramu wa binadamu si jambo la kufumbia macho. Sheria zipo, lakini kinga inaanza na sisi wote.Ukiona, usiny...
21/07/2026

Usafirishaji haramu wa binadamu si jambo la kufumbia macho. Sheria zipo, lakini kinga inaanza na sisi wote.

Ukiona, usinyamaze. Ukijua, elimisha. Ukihisi, toa taarifa.

Usafirishaji haramu wa binadamu si kosa dogo ni uhalifu unaokiuka utu na haki za msingi za binadamu.Sheria za Tanzania z...
20/07/2026

Usafirishaji haramu wa binadamu si kosa dogo ni uhalifu unaokiuka utu na haki za msingi za binadamu.

Sheria za Tanzania zinaeleza wazi kuwa mtu anayehusika na kutenda, kusaidia, kufadhili au kudhamini makosa ya usafirishaji haramu wa binadamu anaweza kuhukumiwa kifungo kisichopungua miaka 5 gerezani.

Tuwe macho, tuwe makini na tutoe taarifa za vitendo vinavyotia shaka. Tushirikiane kulinda usalama na heshima ya kila mwananchi.

> Je, unafahamu? ⚖️Usafirishaji haramu wa binadamu ni kosa kubwa la jinai lenye adhabu kali. Mbali na kifungo, mahakama ...
18/07/2026

> Je, unafahamu? ⚖️

Usafirishaji haramu wa binadamu ni kosa kubwa la jinai lenye adhabu kali. Mbali na kifungo, mahakama inaweza kutoa faini kuanzia TZS milioni 5 hadi milioni 300 kwa mtu anayepatikana na hatia.

Elimu ya sheria ni kinga. Tujifunze, tutoe taarifa za vitendo vinavyotia shaka, na tushirikiane kulinda utu, usalama na haki za kila mwananchi.

Usafirishaji haramu wa binadamu ni uhalifu mkubwa unaovunja haki na utu wa binadamu. Sheria za Tanzania zimeweka adhabu ...
17/07/2026

Usafirishaji haramu wa binadamu ni uhalifu mkubwa unaovunja haki na utu wa binadamu. Sheria za Tanzania zimeweka adhabu kali kwa yeyote anayejihusisha na vitendo hivi, hasa vinapowahusu watoto na watu wenye ulemavu.

Kila mmoja wetu ana nafasi ya kulinda jamii. Toa taarifa unapobaini viashiria vya usafirishaji haramu wa binadamu na usikae kimya dhidi ya uhalifu huu.

Tushirikiane kujenga jamii salama na kulinda haki za kila mtu.

Usikubali ukimya uwe nafasi ya wahalifu kuendelea kutenda uhalifu.Usafirishaji haramu wa binadamu ni kosa la jinai na un...
16/07/2026

Usikubali ukimya uwe nafasi ya wahalifu kuendelea kutenda uhalifu.

Usafirishaji haramu wa binadamu ni kosa la jinai na unakiuka haki za msingi za binadamu. Kila mmoja wetu ana wajibu wa kulinda jamii kwa kutoa taarifa pale anapoona au kushuku vitendo hivi.

📞 Piga bure 195 kutoa taarifa kwa usalama na kwa siri.

Usikae kimya unaposhuhudia au kushuku uhalifu wa usafirishaji haramu wa binadamu. Sauti yako inaweza kuwa mwanzo wa kuok...
15/07/2026

Usikae kimya unaposhuhudia au kushuku uhalifu wa usafirishaji haramu wa binadamu. Sauti yako inaweza kuwa mwanzo wa kuokoa maisha ya mtu.

📞 Piga bure namba 195, toa taarifa kwa usalama na kwa wakati. Ushirikiano wa kila mwananchi ni silaha muhimu katika kupambana na biashara haramu ya binadamu.

Linda maisha. Linda utu. Toa taarifa.

Usafirishaji haramu wa binadamu ni uhalifu unaokiuka haki na utu wa binadamu. Kila mmoja wetu ana wajibu wa kutambua via...
14/07/2026

Usafirishaji haramu wa binadamu ni uhalifu unaokiuka haki na utu wa binadamu. Kila mmoja wetu ana wajibu wa kutambua viashiria vya uhalifu huu, kutoa taarifa kwa mamlaka husika, na kushiriki katika kulinda jamii dhidi ya vitendo vya unyonyaji.

Biashara ya usafirishaji haramu wa binadamu si tatizo la mtu mmoja, ni changamoto ya jamii nzima. Kila mmoja wetu ana na...
13/07/2026

Biashara ya usafirishaji haramu wa binadamu si tatizo la mtu mmoja, ni changamoto ya jamii nzima. Kila mmoja wetu ana nafasi ya kuzuia uhalifu huu kwa kutoa taarifa, kuelimisha wengine na kukataa kushiriki kwa namna yoyote.

Jiunge nasi katika kampeni ya Kata Mnyororo na tushirikiane kuvunja minyororo ya usafirishaji haramu wa binadamu. Pamoja tunaweza kulinda utu, usalama na mustakabali wa jamii yetu.

Address

Kinondoni Municipal
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Eco- Scope Foundation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Eco- Scope Foundation:

Shortcuts

Share