02/09/2026
NISTIRI NISIFEDHEHEKE β MABINTI 626 WA NIA NJEMA SECONDARY SCHOOL WAFIKIWA
Kupitia programu ya Nistiri Nisifedheheke (Maintain My Dignity), Asma Mwinyi Foundation (AMF) kwa kushirikiana na Hijab Sisters Hub, imewafikia mabinti 626 wa Nia Njema Secondary School, Bagamoyo.
Mabinti hawa wamepatiwa taulo za k**e za STARA, chapa ya Asma Mwinyi Foundation, ikiwa ni sehemu ya juhudi zetu za kuhakikisha kila msichana anapata fursa ya kusoma, kujiamini na kutunza heshima yake bila vikwazo vinavyotokana na changamoto za hedhi.
Kwa AMF, hedhi si sababu ya msichana kukosa shule, ndoto zake wala kujiamini.
Nistiri Nisifedheheke β kwa sababu kila binti anastahili heshima, utu na fursa sawa.
KeepGirlsInSchool EmpowerHer