02/06/2026
AUTISM (USONJI) NA DOWN SYNDROME (USO MFANANO) SI MARADHI YA AKILI
Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Asma Mwinyi Foundation (AMF) Mhe amesema yafwatao akiwa .tanzania kuwa Autism (Usonji) na Down Syndrome (Uso Mfanano) si maradhi ya akili. Jamii zenye hali hii wana ndoto, uwezo na haki ya kuishi kwa heshima k**a binadamu wote. Hizi ni hali za maendeleo na ukuaji wa mtu zinazohitaji uelewa, upendo, heshima na ujumuishi katika jamii.
Ni wajibu wetu sote kuondoa unyanyapaa, ubaguzi na vitendo vyote vya ukatili dhidi ya watoto, vijana na watu wanaoishi na hali hizi.
Tunaendelea kusisitiza kuwa:
Ukatili si utamaduni wetu.
Tulinde utu wa kila mmoja wetu na tuendelee kuimarisha amani, upendo, mshik**ano na maridhiano katika jamii yetu. Kwa pamoja, tujenge mazingira salama na yenye heshima kwa kila mtu bila ubaguzi.
Kila mmoja anastahili kuheshimiwa, kuthaminiwa na kupewa nafasi ya kuishi kwa usawa na heshima.
**anoNaMaridhiano