Sccult 1992 Ltd

Sccult 1992 Ltd SCCULT (1992) Ltd is an umbrella organization for SACCOS in Tanzania mainland. It was established in 1991 under Cooperative Act No.15 of the year 1991

SCCULT (1992) LTD is an apex organisation for SACCOS in Tanzania mainland.

Tarehe 12 Juni 2026, SCCULT (1992) LTD ilishiriki katika Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika Mkoa wa Kagera lililowakutanish...
13/06/2026

Tarehe 12 Juni 2026, SCCULT (1992) LTD ilishiriki katika Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika Mkoa wa Kagera lililowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya ushirika kutoka ndani na nje ya Mkoa.

SCCULT (1992) LTD iliwakilishwa na Bw. Emmanuel Nestory, Afisa TEHAMA, Mtaalamu na Msaidizi wa Mifumo, ambapo alipata fursa ya kuwasilisha kuhusu Mfumo wa Kidijitali wa SOMA na mchango wake katika kuimarisha utendaji wa Vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS) kupitia matumizi ya teknolojia za kisasa.
Mgeni rasmi wa jukwaa hilo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe. Kanali Yahya R. Kido, akisindikizwa na Mrajis wa Vyama vya Ushirika Tanzania Bara, Dkt. Benson O. Ndiege.

Katika hotuba yake, Dkt. Ndiege alizihimiza vyama vya ushirika kutoa huduma bora kwa wanachama kwa kuzingatia misingi ya ushirika na kutumia mifumo ya TEHAMA ili kuongeza ufanisi, uwazi na utoaji wa huduma kwa wakati. Aidha, Mhe. Kanali Yahya R. Kido alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirika k**a chachu ya maendeleo kuanzia ngazi ya familia hadi taifa kwa ujumla.

SCCULT (1992) LTD inaendelea kuimarisha ushirikiano na wanachama pamoja na wadau mbalimbali kwa maendeleo endelevu ya sekta ya ushirika.

(1992)ltd

SCCULT (1992) LTD kwa kushirikiana na Taasisi ya Wakaguzi wa Ndani (IIA) imefanikiwa kuendesha mafunzo ya Kamati za Usim...
12/06/2026

SCCULT (1992) LTD kwa kushirikiana na Taasisi ya Wakaguzi wa Ndani (IIA) imefanikiwa kuendesha mafunzo ya Kamati za Usimamizi na Wakaguzi wa Ndani yaliyofanyika mkoani Singida kuanzia tarehe 09 – 12 Juni 2026 katika Regency Hotel & Resort.

Mafunzo haya yalilenga kuimarisha uwezo wa viongozi wa SACCOS katika usimamizi, udhibiti wa ndani, uwajibikaji na usimamizi wa vihatarishi ili kuongeza ufanisi na uwazi katika taasisi zao.

Tunawashukuru washiriki wote kwa ushiriki wao mzuri na kujitolea katika kujifunza kwa maendeleo ya sekta ya ushirika.

LeadershipTraining Singida CapacityBuilding UshirikaKwanza

SCCULT (1992) LTD kwa kushirikiana na DSIK-Tanzania ilishiriki katika Jukwaa la Ushirika Mkoa wa Ruvuma lililofanyika ta...
07/06/2026

SCCULT (1992) LTD kwa kushirikiana na DSIK-Tanzania ilishiriki katika Jukwaa la Ushirika Mkoa wa Ruvuma lililofanyika tarehe 29–30 Mei 2026, likiwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya ushirika kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kujadili fursa na changamoto pamoja na kuimarisha maendeleo ya ushirika.

Katika jukwaa hilo, SCCULT (1992) LTD iliwakilishwa na Bi. Neema Kapinga, Afisa TEHAMA na Mratibu wa Masoko wa Mfumo wa SOMA, huku DSIK-Tanzania ikiwakilishwa na Bw. Emmanuel Walwa, Mtaalamu wa Elimu ya Fedha.

Ushiriki huo ulitoa fursa ya kutangaza Mfumo wa SOMA, kuhamasisha matumizi ya TEHAMA katika shughuli za ushirika, kuonesha manufaa ya mabadiliko ya kidijitali na kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

Mafunzo hayo yalifungwa rasmi na Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye alisisitiza umuhimu wa kuimarisha shughuli za kiuchumi hususani kilimo chenye tija na matumizi ya elimu inayopatikana kupitia majukwaa ya ushirika. Kwa upande wake, Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Ruvuma, Venance Msafiri, alizihimiza AMCOS ambazo bado hazina SACCOS kuanzisha huduma hizo kwa kuzingatia mafanikio ya AMCOS zenye SACCOS.

Sambamba na hayo, washiriki walitekeleza Msingi wa Saba wa Ushirika (Kujali Jamii) kwa kuchangia madawati 26 yenye thamani ya Shilingi 2,000,000 kwa Shule ya Msingi Lituhi.

SCCULT (1992) LTD inaendelea kuimarisha ushirikiano na wanachama pamoja na wadau mbalimbali kwa maendeleo endelevu ya sekta ya ushirika.

Eid Al - Adha kwa Waislamu wote Duniani.
27/05/2026

Eid Al - Adha kwa Waislamu wote Duniani.

Tunawatakia Heri ya siku ya mama Duniani.Happy Mothers Day.
10/05/2026

Tunawatakia Heri ya siku ya mama Duniani.

Happy Mothers Day.

Tarehe 09 MEI, 2026.Katika jitihada za kuendelea kuhakikisha Ushirika Nchini unapokea mapinduzi ya Kidijitali, SCCULT (1...
10/05/2026

Tarehe 09 MEI, 2026.

Katika jitihada za kuendelea kuhakikisha Ushirika Nchini unapokea mapinduzi ya Kidijitali, SCCULT (1992) Ltd kwa kushirikiana na Kampuni ya kizalendo EmCa Technologies Limited tumezindua Mfumo wa kisasa wa Kidijitali wa uandikishaji wa matukio k**a;
1. Mafunzo;
2. Mikutano Mikuu ya Vyama vya Ushirika;
3. Majukwaa ya Ushirika;
4. Matukio yote ya Vyama vya Ushirika.

Ubunifu huu ni jitahida za SCCULT (1992) Ltd kwenye kutimiza Mpango Mkakati wa 2025/2027 ambao unatoa kipaumbele kwenye uhamasishaji na kuchochea mapinduzi ya Kidijitali. Mfumo huu utasaidia kuongeza ufanisi mkubwa, utunzaji wa kumbukumbu, uhakika wa kudhibiti na kuratibu matukio yote.

Mfumo wa SCCULTEventReg unatarajiwa kuleta faida zifuatazo;
1. Usajili wa washiriki kwa muda mfupi;
2. Utunzaji wa taarifa salama na Kidijitali;
3. Kurahisisha kuingia na kutoka kwa haraka bila kuwa na msongamano;
4. Kuondoa kabisa matumizi ya karatasi;
5. Usimamizi na upatikaji wa taarifa kwa wakati halisi;
6. Usimamizi wa tathmini ya matukio na mrejesho.

SCCULT (1992) Ltd tunajivunia hatua hii na tunakaribisha Vyama vyote vya Ushirika, Majukwaa na wadau kutumia Mfumo huu wa SCCULTEventReg kwa gharama nafuu na rafiki.

Idara ya Mahusiano ya Wanachama na Wadau ya SCCULT (1992) Ltd, ikiongozwa na Bi. Gloria Anthony, imefanikiwa kuwa na kik...
07/05/2026

Idara ya Mahusiano ya Wanachama na Wadau ya SCCULT (1992) Ltd, ikiongozwa na Bi. Gloria Anthony, imefanikiwa kuwa na kikao muhimu na BUMACO LIFE INSURANCE chenye lengo la kuimarisha ushirikiano katika masuala ya bima 🤝

Kikao hicho kiliongozwa na Afisa Mkuu wa Masuala ya Bima, Ndg. Evans Felix Makundi pamoja na timu yake, ambapo pande zote zimejadili fursa mbalimbali za ushirikiano kati ya SCCULT (1992) Ltd na BUMACO LIFE INSURANCE, pamoja na namna bora ya kuwahudumia wanachama kupitia huduma za bima.

Aidha, kikao hicho kimegusia maandalizi ya SACCA CONGRESS 2026 itakayofanyika mwezi Oktoba nchini Tanzania, na namna wadau watakavyoshiriki na kunufaika na kongamano hilo.

Vilevile, pande zote zimejadili mikakati ya kuendeleza ushirikiano wa karibu, ikiwemo ushirikiano katika shughuli mbalimbali za kijamii na michezo.

SCCULT (1992) Ltd inaendelea kujenga ushirikiano imara kwa maendeleo ya sekta ya ushirika na ustawi wa wanachama wake

SCCULT (1992) LTD inawatakia wafanyakazi wote heri ya siku ya wafanyakazi duniani.Tunapoadhimisha Siku ya Wafanyakazi Du...
01/05/2026

SCCULT (1992) LTD inawatakia wafanyakazi wote heri ya siku ya wafanyakazi duniani.

Tunapoadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani, tunapenda kuwapongeza wafanyakazi wote kwa juhudi, uaminifu na mchango wenu mkubwa katika maendeleo ya mahali pa kazi Kila mmoja ni sehemu muhimu ya mafanikio.

Kazi za wafanyakazi si tu inajenga uchumi, bali pia inaleta mabadiliko chanya katika jamii. Endeleeni kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na mshik**ano.

Tunawatakia heri njema, afya njema na mafanikio zaidi katika majukumu yenu.

Heri ya Siku ya Wafanyakazi Duniani!

SCCULT JUMUISHI KWA USTAWI WA SACCOS

ZIARA YA UWEKEZAJI WA AKIBA KWENYE MFUKO WA CFF - SAVINGS MOBILIZATION CAMPAIGN 2026Leo Tarehe 21 April 2026 Afisa Hudum...
21/04/2026

ZIARA YA UWEKEZAJI WA AKIBA KWENYE MFUKO WA CFF - SAVINGS MOBILIZATION CAMPAIGN 2026

Leo Tarehe 21 April 2026 Afisa Huduma za Fedha Ndg.Said Hassan Sakuru ametembelea ofisi za NYUMBA SACCOS Ltd zilizopo wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam.

Katika ziara hiyo kilifanyika kikao na Mtendaji mkuu wa Nyumba SACCOS Ltd. Bi. Grace Amini ambapo Nyumba SACCOS Ltd wanafanya uwekezaji rasmi kwenye mfuko wa SACCOS kukopeshana CFF

Tunaendelea kuzikaribisha SACCOS kutumia huduma ya CFF ili kuongeza ujumuishi wa huduma za kifedha nchini

SCCULT JUMUISHI KWA USTAWI WA SACCOS

Mkutano wa Afrika Mashariki wa Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo Umehitimishwa Mombasa, Kenya.Vyama vya Ushirika wa ...
19/04/2026

Mkutano wa Afrika Mashariki wa Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo Umehitimishwa Mombasa, Kenya.

Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo kutoka Tanzania, Nchi za Afrika Mashariki na Nchi nyingine 17, pamoja na viongozi na watendaji kutoka Mamlaka za usimamizi, k**a vile Benki Kuu ya Tanzania na Wizara ya Fedha na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Nchini walishiriki kwa mafanikio makubwa.

Mkutano wa Afrika Mashariki wa Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo uliofanyika Prideinn Flamingo Resort, Mombasa -Kenya. Mkutano huu ulianza tarehe 14 mpaka 17 Aprili, 2026.

Mkutano huo ulifunguliwa na Waziri wa Maendeleo ya Biashara ndogo na kati na Ushirika wa Kenya, Hon. FCPA Dr. Wycliffe Oparanya (EGH).

Katika siku ya kufunga mkutano, Waziri Hon. FCPA Dr. Wycliffe Oparanya alihutubia washiriki na alisisitiza umuhimu wa ushirika wa Akiba na Mikopo katika kukuza uchumi wa Afrika Mashariki na umuhimu wa Serikali kuunga mkono Maendeleo ya Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo. Washiriki walipata pia fursa ya kusikiliza mawasilisho na majadiliano kutoka kwa viongozi muhimu, wakiwemo Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo Ulimwenguni (WOCCU), Bwana Michael Lawrence, na Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa WOCCU, Bwana Paul Treinen.

Jumla ya Watanzania 120 walishiriki kwenye mkutano huu muhimu, na kutoa mchango mkubwa katika mijadala ya maendeleo ya vyama vya ushirika wa akiba na mikopo katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

SCCULT (1992) Ltd, Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo Nchini na Wadau wake wote tutaendelea kutoa ushirikiano mkubwa kwa ACCOSCA na kudhamini mchango wake kwenye Maendeleo ya Ushirika wa Akiba na Mikopo Tanzania hasa ukizingatia kuwa Mwaka huu 2026 Mkutano Mkubwa wa SACCA CONGRESS utafanyika Tanzania kwa mara ya kwanza katika historia yetu.

SCCULT JUMUISHI KWA USTAWI WA SACCOS

Address

Lumumba Street
Dar Es Salaam
11105

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sccult 1992 Ltd posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Sccult 1992 Ltd:

Share