Humanity matters MORE

Humanity matters MORE Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Humanity matters MORE, Nonprofit Organization, Dar es Salaam.

We have created this page with a concrete reason to impact humanity to all people who really knows the important of life for other people you are one of those who value others , Join us for revive

21/12/2021

TAJIRI WA MADINI ALIYETHAMINI DINI.
Alikuwa Ni mtu aliyefahamu UMUHIMU wa utu wa WATU wengine. Shughuli kuu aliyojihusisha nayo ilikuwa uuzaji na ununuzi wa vito vya THAMANI , alinunua ,aliuza na kusambaza MADINI ya dhahabu. Alijaliwa na kumiminiwa BARAKA tele , kufurika kwa neema kubwa kubwa na ndogondogo vyote alijaliwa navyo. Alimiliki majengo ,mashamba ,magari na familia nzuri YENYE mke na watoto wake watatu,
Sikutaka kusubiri wino wa kalamu yangu ikauke na karatasi hii kupeperushwa kabla ya kuyaandika haya unayoenda kuyaaoma kuhusu MTU huyu,
Kwanza kabisa hakujisahulisha kuhusu ugumu wa maisha kwa watu wa hali ya chini, maana kuna MTU akifanikiwa hudhani kuwa watu wote wamefanikiwa na kuamini hakuna MTU mwenye njaa, wasio na nguo , wanaotembea peku pasipokuwa na viatu au hata wajane na yatima wasiofahamu hatima yao na huzuni katika mitima yao. Basi tumwite Hantigaro , Alijihoji na kuwaza utofauti wake wa kiuchumi na watu wengi waliomzunguka na kugundua ulikuwa utofauti mkubwa Sana , lakini Sasa hakutaka kabisa au kusubiri kuambiwa kuhusu majanga yaliyowakabili watu Hawa , Hantigaro aliamka na kufanya tafiti mbalimbali ikiwemo uhalisia wa ugumu wa maisha ya MTU wa kawaida na kugundua kuwa watu wanaishi katika kuvumilia na sio kujivunia,
Hapa ndio kisa chetu kinanoa nanga na nahodha Makini Sana asiyeyumbishwa na mawimbi ya bahari . Hantigaro alionekana akiagiza chakula , alikula kwa mamantilie chakula Cha mchana , macho ya wengi yalimwelekea na minong'ono ya chini kwa chini zilisikika na sauti za nziii , alikula huku akiwatazama wapishi na wahudumu ,nguo walizovaa na Kanda mbili miguuni hoja si kuwaelezea mwonekano wa watu Hawa Hantigaro yeye aliwangalia kwa jicho la masikitiko na kugundua ugumu wa kipato kiliwasababisha watu wale kuishi maisha yale. Alikuja mdada mwenye ujauzito na kuomba kumhudumia , kwa unyenyekevu mkubwa Hantigaro aliulizia Bei ya chakula akaambiwa wali samaki K**a kawaida elfu moja Mia tano na juisi ya kusaga Mia tano aliagiza akala na

17/12/2021

BEING A LIVE IN LOVE WITH GOD FOR TWELVE MONTHS IN 2021 IS A GREAT FAVOUR UPON OUR LIFE ,
GLORY , HONOUR , ADORATION AND PRAISE BE TO GOD.
THANK YOU ALL FOR SHOWING MUCH CONCERN WITH OUR TEAM , WE STILL NEED YOUR VIEW ON HOW WE CAN RUN THIS PROGRAM . BE BLESSED ALL , HAPPY CHRISTMAS AND A PROSPEROUS YEAR 2022

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255752070444

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Humanity matters MORE posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share