TUKO SAWA -Harmony Generation

TUKO SAWA -Harmony Generation Karibu Mtandao wa KIZAZI CHA HARMONY. Tunaongozwa na UTU, UPENDO na UMOJA โ€“ ili kujenga jamii zenye MSHIKAMANO na USTAWI kwa wote.

Fuata link ๐Ÿ‘‰๐Ÿพujiunge na grupu letu leo - https://www.facebook.com/groups/2058835474948933

๐ŸŽ‰ MSHINDI WA 100,000/= YA   โ€“ MEI 2026HONGERA KWAKO Gertrude Mosanga Mabusi Paul kutoka Dar.Baada ya kuchambua kwa kina ...
26/05/2026

๐ŸŽ‰ MSHINDI WA 100,000/= YA โ€“ MEI 2026

HONGERA KWAKO Gertrude Mosanga Mabusi Paul kutoka Dar.

Baada ya kuchambua kwa kina machapisho yote yaliyowasilishwa kulingana na vigezo rasmi vya shindano la , chapisho la Gertrude lilitoka k**a bora zaidi kwa ujumla.

Baada ya mazungumzo naye, tumejiridhisha kuwa Gertrude hakushiriki tu kwa juu juu, bali alijishughulisha kwa kina, alifikiria kwa undani na kutumia lenzi pana ya Harmony inayoona miunganisho na mahusiano.

Upekee wa posti yake ni kwamba, alikutana na picha ya โ€œubuyuโ€ mitandaoni lakini yeye akaingazia kwa lenzi ya Harmony, na kuibadilisha kuwa somo lenye kina kuhusu โ€œSala ya Bwanaโ€ kati ya muwindaji Duma/Chui aliyekuwa na njaa akihitaji "mkate wake wa kila siku" na Swala aliyekuwa anakimbia kwa hofu na kuomba "aepushwe na uovu".๐Ÿ†๐ŸฆŒ

Sababu kuu za kumchagua Gertrude:

Kwanza kabisa, Gertrude aliandika kila kitu kutoka kichwani bila kutumia akili mnemba kumpa idea au kumsahihisha. (Nitashea link ya posti yake mwishoni ujionee mwenyewe.)

Pili, alihusisha ujumbe wake na kanuni ya Kutegemeana na Mizunguko ili kugeuza ubuyu kuwa somo la kina kuhusu uwiano wa asili, kutegemeana kwa viumbe, na ikolojia.

Lakini kipekee zaidi ni umahiri wake wa kujibu kilichompelekea kuchagua andiko lake na hasa kuunganisha nadharia na maisha halisi. Aliweza kutoka kwa wanyama โ†’ mfumo wa ikolojia โ†’ jamii ya binadamu โ†’ kiroho โ†’ kifo na kuzaliwa upya, bila kupoteza mwelekeo. Huu ni ustadi adimu.

Aliweza kuonesha wazi kwamba kwenye Uumbaji hakuna โ€œmbayaโ€, kwani maisha ni umoja mkubwa unaofanya kazi kupitia marekebisho ya nishati na mizunguko.

Hongera sana Gertrude! ๐Ÿ‘
Hii ndiyo elimu tunayoitaka kuieneza ili kujenga kizazi cha harmony kinachoelewa kuwa KANUNI YA DHAHABU inahusu viumbe wote. !

๐ŸŒ HAKIKA SOTE TUKO SAWA KIUUMBAJI

MWEZI JUNI TUTAENDELEA NA SHINDANO.

LINK YA POSTI YA GERTRUDE HII HAPA: https://www.facebook.com/gertrude.paul.330/posts/pfbid0a5PpeEVBxXHxLhss3ctg84ZWu8QE1UTAAqXyJ9HuqkoiouJdQxxB5cf5QTUyT8EAl?locale=en_GB

๐ŸŒ ๐ŸŒHAPPY AFRICA DAY! Leo tunapoadhimisha Siku ya Afrika, ni muhimu kujikumbusha kuwa nguvu ya kuijenga Afrika tunayoitaka...
25/05/2026

๐ŸŒ ๐ŸŒHAPPY AFRICA DAY!

Leo tunapoadhimisha Siku ya Afrika, ni muhimu kujikumbusha kuwa nguvu ya kuijenga Afrika tunayoitaka ipo ndani yetu wenyewe.

Takriban miezi kumi iliyopita, Mlezi wa Jumuiya ya Tuko Sawa, Madaraka Nyerere, aliandika kwenye safu yake ya ARUSHA NEWS makala yenye ujumbe mzito kuhusu umuhimu wa kurejesha fikra za kujitegemea, mshik**ano na kutumia uwezo wa jamii zetu kuamua hatima yetu wenyewe.

Katika zama hizi za utegemezi wa misaada na changamoto zinazotokana na uchovu wa wafadhili (donor fatigue), makala hiyo inatukumbusha umuhimu wa kujenga misingi endelevu ya maendeleo inayotokana na nguvu, maarifa na ushirikiano uliopo ndani ya jamii zetu.

Kupitia mfano wa Jumuiya ya Tuko Sawa Tanzania (JTS), anaonesha jinsi watu kutoka kada mbalimbali โ€” wanafunzi, walimu, madaktari, wafanyabiashara, wafanyakazi wa ndani na wanasheria โ€” wanavyoweza kushirikiana kujenga jamii yenye ustawi, utu na uwajibikaji wa pamoja.

Ujumbe wake haukuwa wa kukataa ushirikiano wa kimataifa, bali wa kurejesha imani katika uwezo wetu wa kufikiri, kujitegemea, kushirikiana kwa heshima, na kujenga maendeleo yanayotokana na mahitaji na nguvu za jamii zetu wenyewe.

Hiyo ndiyo roho ya Afrika yenye kujiamini, mshik**ano na uwezo wa kuamua mustakabali wake.

Karibu sana ujisomee makala nzima hapa๐Ÿ‘‰๐Ÿพ [Link ---https://www.arushanews.co.tz/columns/finding-strength-in-ourselves-to-shape-the-future/]

Hongera kwa Balozi Mtendaji wa harmony, Mwalimu Byangwamu Edwine wa shule ya msingi Airwing jijini Dar es Salaam kwa kue...
18/05/2026

Hongera kwa Balozi Mtendaji wa harmony, Mwalimu Byangwamu Edwine wa shule ya msingi Airwing jijini Dar es Salaam kwa kuendelea kuongeza USTAWI WA JAMII:

Balozi Edwin ambaye pia ni Mratibu wa Vituo vya Ubora vya Jumuiya yetu ameniambia hivi:

"Haya mahindi tumeyapanda tarehe 22.01.2026 kuanzia saa moja 1:30 Asubuhi.

Leo tarehe 18.05.2026 tumeshirikiana kuyavuna. Wanafunzi wamefurahia sana hili zoezi na kwa kweli mahindi ni matamu sana! Walimu pia wameshiba๐Ÿ˜‹"



Address

Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TUKO SAWA -Harmony Generation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share