SHIKUHA TUNASHUGHULIKA NA YAFUATAYO
👉Kutozidisha kwa nauli kwa Abiria hasa vipindi vya sikukuu
👉Kupotea mizigo na kusababisha usumbufu na hasara
👉Ukatishaji wa route kwa Mabasi na Daladala
👉NA MENGINE MENGI, SOMA ZAIDI POST ZINGINE ILI KUJUA ZAIDI. SHIKUHA (SHIRIKA LA KUTETEA ABIRIA TANZANIA) ni Shirika kamili ilioundwa na watu makini kusaidia mpango wa serikali wa kuhakikisha watanzania wanafura
hia nchi yao na wanakuwa SALAMA wanaposafiri kwa kutumia vyombo mbalimbali vya usafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Lengo ni kuelimisha raia/wasafiri kwanza kuzijua haki zao, lakini pili raia/wasafiri kuwajibika kulinda usalama wao ikiwemo kusaidia kuepusha madhara yatokanayo na ajali za barabarani, Serikali inajali sana uzima, afya na usalama wa mtu. Serikali imekuwa ikipoteza raia wake kutokana na ajali za vyombo vya usafirishaji kutokana na aidha uzembe wa abiria lakini pia uzembe wa wamiliki na waendeshaji wa vyombo hivyo. Serikali haiwezi kuvumilia kuona raia wake wanapoteza maisha kwa uzembe, maana hiyo ni rasilimali watu inapotea, kwahiyo taasisi hii ipo kuiunga mkono serikali katika kutimiza malengo yake ya usalama wa vyombo nya usafirishaji pamona na abiria wao (watanzania wote)