The Same Qualities Foundation

The Same Qualities Foundation we value the qualities of all kids

01/06/2026

Mwenezi Arusha awajia juu wanlipatiwa pikipiki za chama na kuweka makava wachukuliwe hatua kali

01/06/2026

Wanafunzi wawili wa shule ya msingi waliokuwa wanatafutwa na wazazi wao baada ya kutokuonekana nyumbani kwao kwa takribani siku nne katika kata ya Baraa Jijini Arusha, hatimaye wamepatikana, huku ikidaiwa kuwa wamekutwa kwenye chumba cha mwanamke mmoja wakiwa wanatumikishwa kingono na wanaume tofauti tofauti Jijini humo.

Inaelezwa kuwa tukio hilo limebainika, Mei 31, 2026, baada ya ndugu wa mmoja wa watoto hao kufika anapoishi mwanamke huyo anayefahamika kwa jina moja la Linnah, kwa lengo lakumweleza kuhusu upotevu wa watoto hao, k**a iwapo amewaona popote, lakini ghafla baada ya mlango kufunguliwa ndugu huyo aliwaona watoto hao wakiwa ndani ya chumba hicho.

01/06/2026

Wakazi wa Nanyuki wamefanya maandamano wakipinga mpango unaoripotiwa wa kuanzishwa kwa kituo cha karantini ya Ebola katika Kambi ya Jeshi la Anga ya Laikipia

01/06/2026

Video inaonesha maduka yaliyopo katika eneo la EmaXesibeni huko Eastern Cape yakiwa tupu na mtaa ukiwa na upweke baada ya kufukuzwa kwa wahamiaji kutoka mataifa ya Afrika wanaoishi nchini humo.

25/05/2026

Vurugu Zazuka Arusha Kufuatia Mgomo wa Madereva wa Daladala

Hali ya sintofahamu imeripotiwa katika baadhi ya maeneo ya jijini Arusha kufuatia mgomo wa madereva wa daladala ulioanza leo, ambapo baadhi ya madereva wanaodai kuunga mkono mgomo huo wameonekana kuwazuia wenzao wanaoendelea na kazi kupakia abiria.

Mashuhuda wa tukio hilo katika eneo la Ngulelo wamesema vituo kadhaa vya daladala vilitawaliwa na mvutano mkubwa baada ya madereva waliogoma kuwataka wenzao kusitisha huduma kwa madai ya kuonyesha mshik**ano katika kudai maboresho ya mazingira ya kazi.

Kutokana na hali hiyo, mamia ya wananchi wamejikuta wakikosa usafiri huku baadhi yao wakilazimika kutembea kwa miguu kuelekea maeneo mbalimbali ya kazi na shughuli nyingine za kila siku. Maeneo ya Mianzini, Sanawari pamoja na Ngulelo yameonekana kuwa miongoni mwa yaliyoathirika zaidi na uhaba wa usafiri.

Madereva hao wanadai kuwa changamoto kubwa wanazokutana nazo ni pamoja na faini za mara kwa mara kutoka LATRA pamoja na kupanda kwa gharama za uendeshaji kutokana na ongezeko la bei ya mafuta.

Aidha, wameiomba serikali kupitia mamlaka husika kuruhusu kupandishwa kwa nauli za daladala hadi kufikia shilingi 1,000, wakidai kiwango cha sasa hakikidhi gharama za uendeshaji wala kuwawezesha kupata faida.

21/05/2026

Rio Ferdinand amesema amevutiwa na maendeleo ya miundombinu ya michezo nchini Tanzania baada ya kutembelea Uwanja wa Samia uliopo jijini Arusha leo Mei 21, 2026.

Baada ya kuuzunguka na kuuangalia uwanja huo ambao unatarajiwa kutumika kwenye mashindano ya AFCON 2027, Ferdinand ameusifu kwa ubora wake na kueleza kuwa uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Tanzania katika sekta ya michezo ni hatua muhimu kwa maendeleo ya mchezo huo nchini.

Ferdinand pia amesema atarejea tena Tanzania mara baada ya kukamilika kwa uwanja mpya wa kimataifa unaojengwa jijini Arusha, akieleza kuwa miundombinu bora ndiyo msingi wa kukuza vipaji na kuinua kiwango cha michezo.

I got over 50 reactions on my posts last week! Thanks everyone for your support! ๐ŸŽ‰We continue to build pre hospital in t...
17/05/2026

I got over 50 reactions on my posts last week! Thanks everyone for your support! ๐ŸŽ‰
We continue to build pre hospital in the city of Arusha and Tanzania at large

TAWIRI YAREJESHA MATUMAINI KWA WANANCHI KWA KUDHIBITI TEMBO KISAYANSI.Wananchi katika maeneo yenye migongano na Tembo wa...
16/05/2026

TAWIRI YAREJESHA MATUMAINI KWA WANANCHI KWA KUDHIBITI TEMBO KISAYANSI.

Wananchi katika maeneo yenye migongano na Tembo wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali k**a mabomu baridi na njia nyingine nyingi katika kukabiliana na kadhia hiyo hapa nchini. Hata hivyo, Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) imetumia mbinu ya kuwafunga mikanda yenye visukuma mawimbi (GPS) Tembo viongozi katika juhudi za Wizara ya Maliasili na Utalii za kupunguza migongano hiyo

Mtafiti na Daktari wa wanyamapori kutoka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) Dkt. Iddi Lipende amesema mikanda iliyofungwa itakuwa inatoa taarifa ya mienendo ya tembo na watakapokuwa wanaelekea kwenye makazi na mashamba ambapo askari wanyamapori waliopo kwenye vituo vya uthibiti wa Wanyamapori wakali na waaribifu(PAC) watapata taarifa mapema na kuwazuia mapema kabla hawajafanya madhara kwa wananchi.

Aidha, Afisa Wanyamapori wa Wilaya ya Meatu, Bwana Joseph Sikawa, ameishukuru serikali kwa kuiwezesha TAWIRI kufanikisha zoezi hili katika wilaya ya Meatu. Wilaya ya Meatu imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya uvamizi wa tembo mashambani ambapo
Makundi ya tembo yameonekana kuingia katika mashamba katika vijiji vya Mwanyahina, Mwajidalala, Mwanzagamba, Mbugayabanya, Mwamashimba, Mangโ€™wina, Mwangudo, Mbushi, Shushumi, Mbuyuni, Sungu na Paji

Mwananchi kutoka Meatu pia ameeleza kufurahishwa na hatua hiyo, akisema hapo awali walilazimika kulala mashambani kulinda mazao yao dhidi ya tembo, lakini sasa teknolojia hiyo itasaidia kuwafuatilia wanyama hao mapema na kuwazuia kabla hawajafika katika maeneo ya kilimo, alisema Godfrey Mabula.

Kwa upande wake, Afisa Uhifadhi daraja la kwanza Bw. Ayubu Fundi kutoka (TAWA) amesema wamekuwa wakifanya juhudi kubwa kuwarudisha tembo hifadhini. lakini wakati mwingine wamekuwa wakichelewa kuwafikia kutokana na wanyama hao kutokea maeneo mbalimbali ya hifadhi. "matumizi ya vifaa hivyo yatawezesha udhibiti wa haraka zaidi kabla ya tembo hao kuingia kwenye mashamba ya wananchi" amesema.

na teknolojia ni Uti wa Mgongo katika Utafiti na Uhifadhi Endelevu.

14/05/2026

ย ya walima ๐Ÿ‡ ni ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

Team katika ubora wake
13/05/2026

Team katika ubora wake

Address

P. O BOX 11641
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Same Qualities Foundation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share