Iqra Global Media

Iqra Global Media Spreading the light of Islam to the world.

08/12/2026

Tuanze siku yetu na kisomo kizuri chenye mazingation

Allahmdulillah tumefanikiwa kunasa Kisomo cha mwalimu wetu tena leo.Tuambie vidéo iyi ianzie Youtube, Instagram, Tiktok ...
08/12/2026

Allahmdulillah tumefanikiwa kunasa Kisomo cha mwalimu wetu tena leo.

Tuambie vidéo iyi ianzie Youtube, Instagram, Tiktok wala hapa Facebook

Mashallah vijana wadogo wadogo wana jituma sana hasahasa wakati huu w ma grande vacances.

Jiunge na groupe letu la WhatsApp
👇👇👇
https://chat.whatsapp.com/BxtZxjlAIc33zvnVXobs6e?s=cl&p=a&ilr=0

Mechi ambayo imekutanisha vijana wa CJMD na wa Centre Kalimabenge.Match imeisha CJMD 2-1 C. KALIMABENGEJe Match ni sabab...
08/10/2026

Mechi ambayo imekutanisha vijana wa CJMD na wa Centre Kalimabenge.

Match imeisha CJMD 2-1 C. KALIMABENGE

Je Match ni sababu ya kuhishi pamoja (cohésion sociale) ?
Towa maoni yako hapa 👇🏾👇🏾

https://chat.whatsapp.com/BxtZxjlAIc33zvnVXobs6e?s=cl&p=a&ilr=0

Karibuni tutaleta uchambuzi wa ili swala.

📍UVIRAKwa lengo la kusherehekea Mwezi wa Vijana, Cercle des Jeunes Musulmans pour le Développement - CJMD Uvira imepanga...
08/09/2026

📍UVIRA

Kwa lengo la kusherehekea Mwezi wa Vijana, Cercle des Jeunes Musulmans pour le Développement - CJMD Uvira imepanga na kufanikisha mechi ya urafiki na mshik**ano dhidi ya vijana wa Centre Kalimabenge

Mechi hiyo ilifanyika Jumapili tarehe 09/08/2026 saa kumi mchana (16h00) kwenye Uwanja uliopo karibu na Mto Kavimvira, maarufu uwanja wa mafuriko Kavimvira, chini ya kauli :
"ENSEMBLE POUR L'UNITÉ, LE RESPECT ET LA PAIX !"

MGENI RASMI ASIFU HATUA HIYO
Mgeni rasmi wa siku hiyo alikuwa Muheshimiwa Issa MWAKA MUSTAPHA, Kiongozi wa Vijana Mjini Uvira (CUJ-Uvira). Alifungua rasmi mechi hiyo, akisindikizwa na Mwenye Kiti Makamu wa Baraza la Vijana Waislamu Uvira (CJI), Bwana Ir. Songolo Kabenga Suleimani.

Katika hotuba yake, Muheshimiwa Issa Mwaka alionyesha furaha kubwa na kusema:

Mechi hiyo ilimalizika kwa matokeo ya bao 2-1 kwa faida ya CJMD Uvira.

Baada ya mechi, Bwana Ramazani Kwibe Saleh, Mwenye Kiti wa CJMD Uvira alionyesha matumaini yake kuwa:

Kwa upande wake, Bwana Amisi Muhammad Ali, akizungumzia upande wa vijana wa Centre ya Kalimabenge, alifurahishwa na kitendo hicho na kusema:
Hii inaweza kuwa suluhu muhimu na moja wapo ya kumaliza sinto fahamu ndani ya vijana wa jamii ya Kiislamu.

Tukio hili linaonyesha wazi kuwa kupitia michezo, vijana wanaweza kujenga umoja mshik**ano na amani badala ya migogoro. CJMD Uvira imeahidi kuendelea na mipango k**a hii.

IQRA GLOBAL Media
+243 962 825 902

Hadithi hii inatufundisha misingi mikubwa ya dini: Uislamu, Imani na Ihsani. Pia inaonyesha umuhimu wa kuuliza maswali k...
08/09/2026

Hadithi hii inatufundisha misingi mikubwa ya dini: Uislamu, Imani na Ihsani. Pia inaonyesha umuhimu wa kuuliza maswali kwa ajili ya kujifunza na kuwafundisha wengine. Jibril (A.S.) alikuja katika sura ya mwanadamu ili Maswahaba wajifunze kupitia mazungumzo yake na Mtume ﷺ.
Hii ni hadithi nzuri sana kwa Hadithi ya Siku, lakini hadithi kamili ni ndefu zaidi. Tunaweza kuigawa Sehemu ya 1 na Sehemu ya 2 bila kupunguza ujumbe wake.

Muislamu ajiepushe na kuwadhania wengine mabaya bila ushahidi.Uislamu unakataza kupeleleza siri na makosa ya watu.Husuda...
08/09/2026

Muislamu ajiepushe na kuwadhania wengine mabaya bila ushahidi.
Uislamu unakataza kupeleleza siri na makosa ya watu.
Husuda, chuki na uadui huharibu udugu na mshik**ano wa jamii.
Mtume ﷺ ametufundisha kusameheana, kupendana na kuishi k**a ndugu.
Usitafute kasoro za wengine; shughulika na kurekebisha nafsi yako na kuwatakia wengine kheri.

KISA CHA UMAR IBN AL-KHATTAB (RA)Sehemu ya Saba: Khalifa Aliyebeba Chakula kwa Familia Yenye NjaaKatika kipindi cha ukha...
08/08/2026

KISA CHA UMAR IBN AL-KHATTAB (RA)
Sehemu ya Saba: Khalifa Aliyebeba Chakula kwa Familia Yenye Njaa

Katika kipindi cha ukhalifa wake, Umar ibn Al-Khattab (RA) alikuwa na kawaida ya kutoka usiku ili kujionea mwenyewe hali za wananchi wake.
Usiku mmoja, akiwa pamoja na mtumishi wake Aslam, aliona moto kwa mbali. Walipoukaribia, wakamkuta mwanamke akiwa na watoto wake wadogo waliokuwa wakilia.
Umar (RA) akamuuliza:
“Kwa nini watoto hawa wanalia?”
Mwanamke akamjibu kuwa walikuwa na njaa.
Umar akaangalia chungu kilichokuwa juu ya moto na kumuuliza kilichokuwa ndani yake. Mwanamke akamweleza kuwa kulikuwa na maji na vitu vilivyowekwa humo ili kuwafanya watoto wafikiri chakula kinapikwa, wakisubiri mpaka usingizi uwachukue.
Mwanamke huyo hakujua kwamba mtu aliyekuwa akizungumza naye alikuwa Khalifa Umar (RA). Kwa huzuni, akalalamika kuhusu hali yao na kumlaumu Umar kwa kutofahamu mateso ya watu wake.
Maneno hayo yakamgusa sana Umar.
Akarudi haraka kwenye ghala la chakula la Waislamu na kuchukua unga na mahitaji mengine ya chakula. Aslam alipotaka kumbebea mzigo huo, Umar akakataa na akaamua kuubeba mwenyewe.
Akarudi kwa familia ile, akawasaidia kuandaa chakula mpaka watoto wakala na kushiba. Baada ya muda, watoto waliokuwa wakilia wakaanza kutulia na kucheza.
Umar (RA) hakutaka kuondoka mpaka alipoona watoto wametulia.
Huyo ndiye Umar ibn Al-Khattab (RA)—Khalifa ambaye hakutosheka kukaa katika nafasi ya uongozi, bali alihofia kuulizwa mbele ya Mwenyezi Mungu kuhusu watu waliokuwa chini ya dhamana yake.
Itaendelea...

08/08/2026

08/08/2026

Kipindi Cha Harakati zetu

08/08/2026

Address

Indianapolis, IN

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Iqra Global Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Iqra Global Media:

Shortcuts

Share