21/08/2026
TULIA TRADITIONAL DANCE FESTIVAL 2026 KUFANYIKA SEPTEMBA 24–26 | TULIA TRUST KUADHIMISHA MIAKA 10
MBEYA:
Tulia Trust inatarajia kuadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016 kwa kuandaa Tulia Traditional Dance Festival 2026, tamasha kubwa la ngoma za asili litakalofanyika kwa msimu wa 10.
Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika kuanzia Septemba 24 hadi 26, 2026, katika Uwanja wa Shule ya Msingi Gombe, Jimbo la Uyole, Jijini Mbeya, likiwa na kauli mbiu:
“TUUENZI UTAMADUNI WETU”
Kwa muda wa siku tatu, tamasha hilo linatarajiwa kuwakutanisha vikundi vya ngoma za jadi, wasanii, wananchi na wadau mbalimbali wa utamaduni kutoka maeneo tofauti, katika kusherehekea na kuendeleza utajiri wa urithi wa Tanzania.
Maadhimisho haya yanafanyika ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya muongo mmoja wa Tulia Trust, huku tamasha likilenga kutoa nafasi kwa jamii kuutambua, kuuenzi na kuurithisha utamaduni wa Tanzania kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Kupitia Tulia Traditional Dance Festival 2026, wananchi watapata fursa ya kushuhudia burudani za ngoma za asili, kujifunza kuhusu tamaduni mbalimbali na kushiriki katika juhudi za kuhakikisha urithi wa kitamaduni unaendelea kuwa sehemu muhimu ya utambulisho wa Taifa.
GREENCITY TV ONLINE itaendelea kuwafikishia taarifa zaidi kuhusu maandalizi, vikundi vitakavyoshiriki na matukio mbalimbali kuelekea tamasha hilo kubwa la utamaduni jijini Mbeya.
📌 TAREHE
24–26 SEPTEMBA 2026
📍 UKUMBI
Uwanja wa Shule ya Msingi Gombe, Jimbo la Uyole – Mbeya
🎠TAMASHA
Tulia Traditional Dance Festival 2026
🗣️ KAULI MBIU
“TUUENZI UTAMADUNI WETU”
GREENCITY TV ONLINE
Habari • Utamaduni • Vijana • Jamii • Maendeleo
Mbeya
Uyole
TuliaTrust10Years
Miaka10YaTuliaTrust
UtamaduniWaTanzania
TanzaniaCulture
GreenCityTVOnline