10/04/2026
CEDO YATOA VYETI VYA PONGEZI KWA WASICHANA WALIOPATA MAFUNZO YA MUDA MFUPI KATIKA CHUO CHA MWANHALA FDC
Shirika la CEDO ni mionhoni mwa CBOs 12, zinazotekeleza mradi wa Uwezeshaji Kupitia Ujuzi (ESP), Kwa kushirikiana na chuo Cha Mwanhala FDC, Kwa ufadhili wa vyuo Marafiki vya Kanada.
Mojawapo ya shughuli za mradi huu ni kuwawezesha wasichana waliokatishwa ndoto zao Kwa kuwapa Ujuzi katika fani za Umeme, Ushonaji na Upishi Ili waweze kujiajiri na kuajiriwa ili kutimiza ndoto zao.
Wasichana Hawa baada ya kumaliza masomo yao Kwa takriba ya miezi sita, na kushinda vikwazo mbalimbali ambavyo vingechangia kukatisha masomo yao, CEDO iliandaa vyeti vya kuwapongeza wasichana hawa.
Tunaipongeza Serikali ya Kanada #, Serikali ya Tanzania #, Vyuo vya Norquest #, The College of North Atlantic CNA, Dr. Alice Mumbi pamoja na timu yake yote Kwa utekelezaji wao uliotukuka katika mradi huu wa ESP.
Na
Rev. Japhet Aloyce Kalegeya