Cocoda Tanzania

Cocoda Tanzania Community Concern of Orphans and Development Association (COCODA) formally registered as a non-governmental organization in Njombe, Tanzania in 2000.

COCODA is providing education to local communities so as to increase awareness about HIV/AIDS.

Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Deloitte Tanzania kwa imani, ushirikiano na uongozi madhubuti waliouonesha ka...
06/05/2026

Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Deloitte Tanzania kwa imani, ushirikiano na uongozi madhubuti waliouonesha katika utekelezaji wa mradi wa Kizazi Hodari.

Tangu kuanzishwa kwa mradi huo, Deloitte Tanzania imekuwa mshirika muhimu katika kuhakikisha utekelezaji wenye ubora, uwajibikaji na matokeo yanayopimika. Kupitia ushirikiano huu, mradi umefanikiwa kufikia malengo yake kwa kiwango cha juu, ukiwa na mchango mkubwa katika kuboresha ustawi wa jamii, hususan kwa makundi yaliyo katika mazingira hatarishi katika mkoa wa Njombe.

Matokeo ya mradi huu yameacha alama chanya na endelevu, ikiwa ni pamoja na kuimarika kwa huduma za kijamii, kuongezeka kwa uelewa wa masuala ya maendeleo ya kijamii, pamoja na kuboreshwa kwa maisha ya walengwa kwa ujumla. Haya yote yanadhihirisha umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za kiraia na sekta binafsi katika kusukuma ajenda ya maendeleo endelevu nchini.

Katika kuhitimisha mradi huo, baadhi ya viongozi wa Shirika la COCODA Tanzania pamoja na viongozi wa juu wa Deloitte Tanzania (Dorothy Matoyo na Kenneth Chima) walioongoza utekelezaji wa mradi wa Kizazi Hodari walionekana katika picha ya pamoja wakati wa hafla fupi ya kutamatisha mradi huo ngazi ya kanda, tukio lililoashiria mafanikio ya ushirikiano huo na dhamira ya kuendeleza juhudi za pamoja.

tunatambua na kuthamini mchango wa Deloitte Tanzania, na tunaamini kuwa ushirikiano huu utaendelea kuimarishwa zaidi ili kuongeza wigo wa athari chanya kwa jamii nyingi zaidi nchini.

Shirika linaendelea kujizatiti katika kubuni na kutekeleza mipango bunifu inayolenga kuleta maendeleo jumuishi na endelevu kwa Watanzania wote.

Shirika la  leo limepokea samani za ofisi kutoka Deloitte Tanzania, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono shughuli za maendele...
27/04/2026

Shirika la leo limepokea samani za ofisi kutoka Deloitte Tanzania, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono shughuli za maendeleo ya kijamii.

Makabidhiano hayo yamefanywa na Meneja wa Kanda ya Iringa na Njombe, Revocatus Kashanga.

Tunatoa shukrani za dhati kwa Deloitte Tanzania kwa mchango wao mkubwa na kwa kutambua pamoja na kuthamini juhudi zetu katika kuwafikia watoto walio katika mazingira magumu.

Pamoja, tunaendelea kujenga jamii yenye matumaini na fursa kwa wote.

28/03/2026
28/03/2026

Elice Simonile
Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Njombe.

28/03/2026

Mradi wa Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP) unaotekelezwa na Colleges and Institutes Canada kwa kushirikiana na COCODA , na kufadhiliwa na Global Affairs Canada .affairs.canada ukiwa na lengo la kukuza usawa, ushirikishwaji na maendeleo jumuishi katika jamii.

Kikao cha majumuisho ya mafunzo yaliyotolewa na COCODA kupitia Mradi wa Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP)  kimefanyika leo ...
28/03/2026

Kikao cha majumuisho ya mafunzo yaliyotolewa na COCODA kupitia Mradi wa Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP) kimefanyika leo Machi 28, 2026 kikihusisha washiriki wote waliopata mafunzo hayo.

Lengo la kikao hiki ni kupata mrejesho kuhusu namna elimu hiyo ilivyowasaidia pamoja na jinsi walivyoweza kuwafikia na kuwawezesha wanajamii wengine.

Washiriki wa kikao hiki walitoka katika kata za Ramadhani, Uwemba na Utalingolo, ambapo walipata fursa ya kubadilishana uzoefu na kujadili hatua zilizochukuliwa katika kuleta mabadiliko chanya ndani ya jamii zao.

Kikao hiki ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP) unaotekelezwa na Colleges and Institutes Canada kwa kushirikiana na COCODA , na kufadhiliwa na Global Affairs Canada .affairs.canada ukiwa na lengo la kukuza usawa, ushirikishwaji na maendeleo jumuishi katika jamii.

20/02/2026

Katekista Mwinuka amelishukuru Shirika la COCODA Tanzania pamoja na Mradi wa Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP) kwa kuwaletea mafunzo hayo wakazi wa Maheve, akibainisha kuwa elimu hiyo itasaidia jamii kutambua haki zao na kuishi kwa kuzingatia misingi ya haki na usawa.

Mafunzo haya yanafanyika kupitia Mradi wa Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP) unaotekelezwa na Colleges and Institutes Canada kwa kushirikiana na COCODA, na kufadhiliwa na Global Affairs Canada. Mradi huu unalenga kuwezesha jamii kwa elimu na ujuzi unaochochea usawa, ushirikishwaji na maendeleo jumuishi.

Siku ya kwanza ya mafunzo ya Haki za Binadamu yaliyofanyika katika Mtaa wa Maheve, Kata ya Ramadhani, yamewakutanisha ma...
13/02/2026

Siku ya kwanza ya mafunzo ya Haki za Binadamu yaliyofanyika katika Mtaa wa Maheve, Kata ya Ramadhani, yamewakutanisha makundi maalum yakiwemo viongozi wa dini, vijana, viongozi wa mitaa na kata, watu wenye ulemavu pamoja na wazee maarufu.

Mafunzo haya yanalenga kuongeza uelewa kuhusu haki za binadamu, wajibu wa kila mmoja na umuhimu wa ushiriki wa makundi yote katika kuimarisha mshikamano na maendeleo ya jamii.

Mafunzo haya yanafanyika kupitia Mradi wa Uwezeshaji kupitia Ujuzi (ESP) unaotekelezwa na Colleges and Institutes Canada (CICAN) kwa kushirikiana na COCODA, na kufadhiliwa na Global Affairs Canada. Mradi huu unalenga kuwezesha jamii kwa elimu na ujuzi unaochochea usawa, ushirikishwaji na maendeleo jumuishi.

Uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) .1975 kwa kushirikiana na Shirika la COCODA TANZANIA  tumemtembel...
11/02/2026

Uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) .1975 kwa kushirikiana na Shirika la COCODA TANZANIA tumemtembelea Diana Tailoring Mart, mdau tunayeshirikiana katika utekelezaji wa Mradi wa ESP – Uwezeshaji kwa Njia ya Ujuzi , unaofadhiliwa na Serikali ya Canada.

Ziara hiyo ilikuwa sehemu ya utaratibu wa kutathmini, kuimarisha na kuthamini mchango wa sekta binafsi katika utoaji wa mafunzo ya ufundi stadi. Diana Tailoring Mart ametoa mchango muhimu kwa kupokea wanafunzi wa ushonaji kwa mafunzo kwa vitendo, kuwajengea umahiri wa kitaaluma na kuwaandaa kwa ushindani katika soko la ajira pamoja na kujiajiri.

Uongozi wa FDC Njombe na COCODA TANZANIA tunatambua kwa heshima na kuthamini ushirikiano huu unaochangia kufanikisha malengo ya mradi, hususan katika kuwawezesha vijana kiuchumi na kuimarisha sekta ya ufundi stadi katika jamii.

Uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kwa kushirikiana na Shirika la COCODA TANZANIA, leo umefanya ziar...
10/02/2026

Uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kwa kushirikiana na Shirika la COCODA TANZANIA, leo umefanya ziara rasmi ya kutembelea Komba Tailoring Mart katika muktadha wa kuimarisha ushirikiano na kutoa shukrani kwa wadau wanaochangia utekelezaji wa Mradi wa ESP – Uwezeshaji kwa Njia ya Ujuzi, unaofadhiliwa na Serikali ya Canada.

Kupitia ziara hiyo, uongozi umepongeza mchango wa Komba Tailoring Mart katika kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa ushonaji, hatua iliyowajengea ujuzi wa kitaaluma na kuwaandaa kwa ajira na kujitegemea kiuchumi. Ushirikiano huu umeendelea kuwa na mchango chanya katika kuboresha maisha ya walengwa wa mradi na kukuza sekta ya ufundi stadi katika jamii.

Uongozi wa FDC Njombe na COCODA TANZANIA unaendelea kuthamini na kutambua mchango wa wadau wote wanaoshirikiana katika kuhakikisha malengo ya mradi yanafikiwa kwa ufanisi na kwa manufaa mapana ya jamii.

Uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kwa kushirikiana na Shirika la COCODA TANZANIA, leo umefanya ziar...
07/02/2026

Uongozi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kwa kushirikiana na Shirika la COCODA TANZANIA, leo umefanya ziara maalum ya kuwashukuru wadau wao wakuu kwa mchango mkubwa katika utekelezaji wa Mradi wa ESP – Uwezeshaji kwa Njia ya Ujuzi, unaofadhiliwa na Serikali ya Canada.

Tunatoa shukrani za dhati kwa Calvin Fashion kwa mchango wake mkubwa katika kufanikisha utekelezaji wa programu hii. Kupitia ushirikiano wake, amekuwa mstari wa mbele katika kupokea wanafunzi wa ushonaji kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo na hatimaye kuwapatia ajira, hatua iliyochangia kuwajengea ujuzi, kujitegemea kiuchumi na kuboresha maisha yao.

Aidha, Calvin Fashion wameendelea kuwa mfano bora wa ubunifu na uzalishaji katika sekta ya ushonaji, na kuchangia kukuza ajira, ujasiriamali na maendeleo ya vijana katika mkoa wa Njombe.

Asanteni sana kwa ushirikiano wenu, moyo wa kujitolea na kwa kuendelea kushirikiana nasi katika kuwawezesha vijana na kujenga jamii yenye fursa na matumaini.

Address

Chaungingi Street
Njombe
P.O.BOX712

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 14:00

Telephone

+255624890450

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Cocoda Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Cocoda Tanzania:

Share