05/05/2026
KIKAO CHA UMOJA WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI WILAYA YA MAGU. 30/04/2026.
Kikao cha mashirika yasiyo ya kiserikali wilaya ya Magu mkoani Mwanza, kilifanyika katika Halmashauri ya wilaya kwa lengo la kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za robo mwaka, pamoja na kufanya maandalizi ya jukwaa la mkutano mkuu ujao unaotarajiwa kuhudhuriwa na zaidi ya washiriki 100.
Kikao hicho kilihudhuriwa na maafisa mbalimbali wa serikali wakiwemo Afisa ustawi wa jamii, Afisa mazingira, Afisa elimu msingi, Afisa biashara na Afisa mipango, ambao walitoa mchango wao katika kujadili maendeleo na changamoto za utekelezaji wa shughuli za mashirika.
Uongozi wa kikao ulisimamiwa na mwenyekiti wa mtandao wa mashirika wilaya ya Magu akishurikiana na Katibu pamoja na msajili msaidizi wa mashirika.
Miongoni mwa mashirika yaliyohudhuria ni AHUKI pamoja na mashirika mingine ya maendeleo.
Kwa ujumla, kikao kilikuwa na mafanikio makubwa kwa kuimarisha ushirikiano kati ya mashirika na serikali, pamoja na kuweka mikakati madhubuti ya kufanikisha mkutano mkuu ujao.