09/06/2026
VIONGOZI WETU KWANINI WAKATI WA UCHAGUZI TUNAKUMBUKWA, BAADA YA UCHAGUZI TUNASAHAULIWA?
Kila uchaguzi unapokaribia, viongozi wanaotafuta kura huonekana kuwa marafiki wakubwa wa wananchi. Wanaingia kwenye nyumba zetu, wanakaa nasi vijiweni, wanakula nasi migahawani, wanasikiliza kila kero na kutuahidi kuwa watakuwa sauti yetu. Wakati huo mwananchi huonekana kuwa wa muhimu sana.
Lakini uchaguzi ukiisha na ushindi kupatikana, mambo hubadilika. Wengi wa viongozi hao huwa mbali na wananchi waliowachagua. Leo ukikutana na baadhi yao barabarani hata salamu imekuwa jambo gumu. Simu hazipokelewi, ofisi hazipatikani kirahisi, na kero za wananchi zinabaki bila majibu.
Wananchi wa Mbulu, Karatu na maeneo mengine mengi wanalia na ugumu wa maisha. Bei za mafuta zimepanda, na kila bidhaa imeongezeka bei. Wafanyabiashara wanapandisha bei kila siku wakitumia gharama za mafuta k**a sababu. Matokeo yake, mwananchi wa kawaida ndiye anayebeba mzigo mkubwa zaidi. Haya ni mambo ambayo viongozi wetu walipaswa kuyazungumzia kwa sauti kubwa na kutafuta suluhisho.
Nauli zinapandishwa ovyo vitu vingi dukani vimepanda Bei hali inazidi kuwa mbaya hamjui kuwa watu Tanzania wote hawako sawa kuna mtu kipato chake cha siku hata kupata 1,000 ni shughuli wakati wa kampeni wakati mnatembelea vijiji kata na wilaya hamkuwaona watu katika hali zao? Tunaomba muamke muwasikilize wananchi.
Kinachoumiza zaidi ni kuona kwamba mwananchi anapouliza maswali au kuhoji jambo la msingi, h k**a adui au mpinzani. Je, kuzungumzia ugumu wa maisha ni kosa? Je, kuomba huduma bora ni uadui? Hapana. Hiyo ndiyo haki ya msingi ya mwananchi katika nchi yake.
Tunawaomba viongozi wetu wakumbuke kuwa madaraka ni dhamana kutoka kwa wananchi. Hakuna cheo cha kudumu, hakuna madaraka ya milele. Kila mmoja wetu atapita duniani, lakini namna alivyowatendea watu ndiyo itabaki kwenye kumbukumbu za historia.
Wananchi wa Tanzania si watu wa fujo. Hatupendi migogoro wala maandamano. Tunachotaka ni kusikilizwa, kuheshimiwa na kuona matatizo yetu yanatatuliwa. Tunahitaji viongozi wanaokuwa karibu nasi wakati wote, si wakati wa kampeni pekee.
Viongozi wetu, tokeni ofisini na mje mwasikilize wananchi. Msisubiri uchaguzi ukaribie ndipo mkumbuke shida zetu. Mliomba kura mkiahidi kuwa mtatutetea; sasa ni wakati wa kutimiza ahadi hizo.
Mwananchi anahitaji matendo kuliko maneno. Anahitaji majibu kuliko ahadi. Anahitaji uongozi unaosikiliza kuliko uongozi unaonyamaza.
Mungu ibariki Tanzania, na awape viongozi wetu hekima ya kuwatumikia wananchi kwa haki na uadilifu.
Toa maoni yako hapo kwenye comment like na share
— JOSEPH DAUD PANGA