Iraqw people

Iraqw people Kama unaipenda kabila lako subscribe iraqw people TV gusa link hii kupata taarifa zote https://youtu.be/yTEDuy7yE1o?si=2hcwx0SyKHnJaS29
(2)

VIONGOZI WETU  KWANINI WAKATI WA UCHAGUZI TUNAKUMBUKWA, BAADA YA UCHAGUZI TUNASAHAULIWA?Kila uchaguzi unapokaribia, vion...
09/06/2026

VIONGOZI WETU KWANINI WAKATI WA UCHAGUZI TUNAKUMBUKWA, BAADA YA UCHAGUZI TUNASAHAULIWA?
Kila uchaguzi unapokaribia, viongozi wanaotafuta kura huonekana kuwa marafiki wakubwa wa wananchi. Wanaingia kwenye nyumba zetu, wanakaa nasi vijiweni, wanakula nasi migahawani, wanasikiliza kila kero na kutuahidi kuwa watakuwa sauti yetu. Wakati huo mwananchi huonekana kuwa wa muhimu sana.
Lakini uchaguzi ukiisha na ushindi kupatikana, mambo hubadilika. Wengi wa viongozi hao huwa mbali na wananchi waliowachagua. Leo ukikutana na baadhi yao barabarani hata salamu imekuwa jambo gumu. Simu hazipokelewi, ofisi hazipatikani kirahisi, na kero za wananchi zinabaki bila majibu.
Wananchi wa Mbulu, Karatu na maeneo mengine mengi wanalia na ugumu wa maisha. Bei za mafuta zimepanda, na kila bidhaa imeongezeka bei. Wafanyabiashara wanapandisha bei kila siku wakitumia gharama za mafuta k**a sababu. Matokeo yake, mwananchi wa kawaida ndiye anayebeba mzigo mkubwa zaidi. Haya ni mambo ambayo viongozi wetu walipaswa kuyazungumzia kwa sauti kubwa na kutafuta suluhisho.
Nauli zinapandishwa ovyo vitu vingi dukani vimepanda Bei hali inazidi kuwa mbaya hamjui kuwa watu Tanzania wote hawako sawa kuna mtu kipato chake cha siku hata kupata 1,000 ni shughuli wakati wa kampeni wakati mnatembelea vijiji kata na wilaya hamkuwaona watu katika hali zao? Tunaomba muamke muwasikilize wananchi.

Kinachoumiza zaidi ni kuona kwamba mwananchi anapouliza maswali au kuhoji jambo la msingi, h k**a adui au mpinzani. Je, kuzungumzia ugumu wa maisha ni kosa? Je, kuomba huduma bora ni uadui? Hapana. Hiyo ndiyo haki ya msingi ya mwananchi katika nchi yake.
Tunawaomba viongozi wetu wakumbuke kuwa madaraka ni dhamana kutoka kwa wananchi. Hakuna cheo cha kudumu, hakuna madaraka ya milele. Kila mmoja wetu atapita duniani, lakini namna alivyowatendea watu ndiyo itabaki kwenye kumbukumbu za historia.
Wananchi wa Tanzania si watu wa fujo. Hatupendi migogoro wala maandamano. Tunachotaka ni kusikilizwa, kuheshimiwa na kuona matatizo yetu yanatatuliwa. Tunahitaji viongozi wanaokuwa karibu nasi wakati wote, si wakati wa kampeni pekee.
Viongozi wetu, tokeni ofisini na mje mwasikilize wananchi. Msisubiri uchaguzi ukaribie ndipo mkumbuke shida zetu. Mliomba kura mkiahidi kuwa mtatutetea; sasa ni wakati wa kutimiza ahadi hizo.
Mwananchi anahitaji matendo kuliko maneno. Anahitaji majibu kuliko ahadi. Anahitaji uongozi unaosikiliza kuliko uongozi unaonyamaza.
Mungu ibariki Tanzania, na awape viongozi wetu hekima ya kuwatumikia wananchi kwa haki na uadilifu.
Toa maoni yako hapo kwenye comment like na share
— JOSEPH DAUD PANGA

MFAHAMU MZEE SAFARI TARMOMzee Safari ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Iraqw na kiongozi mkuu wa jamii ya Wairaqw kati...
08/06/2026

MFAHAMU MZEE SAFARI TARMO
Mzee Safari ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Iraqw na kiongozi mkuu wa jamii ya Wairaqw katika wilaya za Karatu, Mbulu, Hanang na Babati. Amejitolea kuhifadhi, kuendeleza na kuhamasisha utamaduni wa Wairaqw kupitia elimu na ushauri kwa jamii.
Katika nafasi yake ya uongozi, Mzee Safari hutoa elimu kuhusu mila, desturi, maadili na historia ya Wairaqw kwa vijana na jamii kwa ujumla. Pia ni mzee mshauri anayeshiriki katika utatuzi wa migogoro, kuimarisha umoja wa jamii na kutoa mwelekeo katika masuala mbalimbali ya kijamii na kitamaduni.
Aidha, Mzee Safari ni mmoja wa walimu wakuu wa mila za Wairaqw na miongoni mwa wazee wanaoongoza dua na maombi ya kimila katika hafla na matukio muhimu ya kijamii. Kutokana na hekima, uzoefu na uongozi wake, anaheshimiwa na kutambuliwa k**a mmoja wa viongozi muhimu wa jamii ya Wairaqw katika kizazi cha sasa.
Kupitia juhudi zake, urithi wa utamaduni wa Wairaqw unaendelea kuhifadhiwa na kurithishwa kwa vizazi vijavyo, huku akibaki kuwa nguzo muhimu ya mshik**ano, maadili na utambulisho wa jamii hii.
Siku ya tarehe 18/06/2026 ataongea na wairaqw live kupitia page hii ya .

Toa maoni yako like na kushere kwa wairaqw asante.

Iraqw laway leo nina swali kwenu watu wengi hujua kuwa Mbulu ni kabila  kumbe ni mahali leo tuulizane Je wewe ni Mwiraqw...
08/06/2026

Iraqw laway leo nina swali kwenu watu wengi hujua kuwa Mbulu ni kabila kumbe ni mahali leo tuulizane Je wewe ni Mwiraqw wa wapi? Andika hapo kwenye comment mahali umetokea like na share iwafikie wairaqs wote Duniani.
Piga kura yako gusa link na upige kura yako kwenye channel yetu ya iraqw people WhatsApp pia ui follow asanteni taifa. Link hii hapa chini 👇👇👇
https://whatsapp.com/channel/0029Vb78lz9AO7RH2j7D5v43/184

08/06/2026

Jumapili ya tarehe 7/06/2026 ilikuwa siku ya ya maandamano ya Ekarist Takatifu tazama jinsi watu walivyopokea baraka kutoka kwa Padre James Leonard Yarrot akiwabariki na kuwaambia (Akko Mungu Gitsaa'a wokk ng'i stungqi)

Nauli za Dongobesh – Bashay na Dongobesh – Mbulu: Je, Zinafuata Viwango vya LATRA?Kwa mujibu wa viwango vya LATRA, nauli...
06/06/2026

Nauli za Dongobesh – Bashay na Dongobesh – Mbulu: Je, Zinafuata Viwango vya LATRA?
Kwa mujibu wa viwango vya LATRA, nauli za usafiri hupangwa kulingana na umbali wa safari na hali ya barabara.
Dongobesh – Bashay ni chini ya kilomita 10, hivyo nauli ya rejea ni takribani Sh 700, lakini abiria wanatozwa Sh 2,000.
Dongobesh – Mbulu ni chini ya kilomita 40, hivyo nauli ya rejea ni kati ya Sh 1,500 hadi Sh 2,100 kulingana na aina ya barabara, lakini abiria wanatozwa Sh 4,000-5000.
Kwa wastani, LATRA hupanga nauli kwa kiwango cha:
Sh 53.47 kwa kilomita moja kwa barabara ya lami.
Sh 66.67 kwa kilomita moja kwa barabara ya vumbi.
Kutokana na tofauti kubwa kati ya nauli zinazotozwa na viwango vya LATRA, wananchi wana haki ya kuhoji k**a nauli hizi zimeidhinishwa rasmi na LATRA au k**a wamiliki wa vyombo vya usafiri wanajiamulia wenyewe bila kufuata taratibu zilizowekwa.
Mbali na changamoto ya nauli, wananchi pia wanakabiliwa na tatizo la baadhi ya makondakta kutumia lugha chafu, kuwatukana au kuwafokea abiria. Wakati mwingine abiria hushushwa katikati ya safari bila sababu za msingi, labda abiria nanaja nauli ni sh 1000 na na wao walishapandisha kwa kiwango Chao tofauti na mamlaka husika jambo linalowasababishia usumbufu na kuhatarisha usalama wao.
Ni muhimu LATRA kufanya uchunguzi ili kuhakikisha abiria hawatozwi nauli zisizoendana na viwango rasmi.
Ni muhimu kwa mamlaka husika, hususan LATRA na vyombo vya usimamizi wa usafiri, kuchunguza malalamiko haya na kuchukua hatua ili kuhakikisha haki za wananchi zinalindwa na huduma bora zinapatikana kwa wote. Je huko ulipo wewe hali ya usafiri ikoje toa maoni yako.

06/06/2026

Iraqw lawo delor Yarit

05/06/2026

TBT Aprili 10, 2017 | Ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mbao FC tukitokea nyuma.

Iraqw laway hung ukiambiwa leo hii ufanye hii kazi usage kwa kutumia hii mashine utaweza?Hapo toa maoni yako machine zik...
05/06/2026

Iraqw laway hung ukiambiwa leo hii ufanye hii kazi usage kwa kutumia hii mashine utaweza?
Hapo toa maoni yako machine zikiharibika sahivi je wasichana wa karne hii wataweza kusaga unga na hii machine???

04/06/2026

Nitakapomwona mwana wa Adamu

01/06/2026

Iraqw laway hung Leo ninae swali kwenu je jina Hanang (A'nangw) limetokana nini?

Address


27403

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Iraqw people posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Iraqw people:

  • Want your organization to be the top-listed Non Profit Organization?

Share