Kigoma ndio kwetu

Kigoma ndio kwetu KWA PAMOJA TUTAIJENGA KIGOMA YETU
(1)

Samaki hawa wanaitwaje? ๐Ÿ˜
09/06/2026

Samaki hawa wanaitwaje? ๐Ÿ˜


Mlima Chanza - Buhoro Bunganda - Kasulu ๐Ÿ˜
09/06/2026

Mlima Chanza - Buhoro Bunganda - Kasulu ๐Ÿ˜


BREAKING NWES: Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Kampasi ya Kigoma, umefikia  Asilim...
09/06/2026

BREAKING NWES: Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Kampasi ya Kigoma, umefikia Asilimia 78.9 huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Agosti,2026.

Kukamilika kwa ujenzi wa Taasisi hiyo kunatoa fursa ya udahili wa kwanza kwa wanachuo watakaohitaji kusoma katika Kampasi hiyo mwaka wa Masomo 2026, jambo litakaloongeza fursa za kitaaluma kwa kada ya Afya na kuimarisha Sekta ya matibabu mkoani hapa.

Akizungumza mara baada ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa mradi huo, Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma CPSP. Hassan Rugwa amesema kwa sasa Serikali inaendelea kukamilisha miundombinu muhimu ikiwemo barabara ili kulifanya eneo hilo kufikika kwa urahisi.

Amesema Taasisi hiyo ni kiungo muhimu hivyo wakazi wanapaswa kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazojitokeza kutokana na uwepo wa chuo hicho.

Naye Mhandisi Mkazi wa mradi huo Selemani Malambo, amesema kazi zote za msingi katika ujenzi huo zimekamilika huku zikibaki kazi chache za ukamilishaji wa miundombinu ya ndani sambamba na usimamizi wa ardhi nje ya majengo hayo.


BREAKING NEWS Nyota wa Fc Dallas ya USA ๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡ธ Bernard Kamungo Mzaliwa mkoa wa Kigoma yupo tayari kuitumikia timu ya Taifa y...
09/06/2026

BREAKING NEWS

Nyota wa Fc Dallas ya USA ๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡ธ Bernard Kamungo Mzaliwa mkoa wa Kigoma yupo tayari kuitumikia timu ya Taifa ya Tanzania,awali aliitumikia USA U-23 na mechi moja ya kirafiki katika timu ya wakubwa, Mchakato wa kuitumikia Tanzania umeanza

โ€œNimezaliwa kigoma na kukulia Kigoma, Nimesoma shule za Tanzania mpaka sekondari,tulihamia Marekani nikiwa na umri wa miaka 14,Nina cheti cha Tanzania,Nathibitisha kuwa nina uraia wa Tanzania mpaka sasa,Itakuwa fahari kubwa sana kwangu nikiitwa kuitumikia timu ya Taifa ya Tanzania"
Bernard Kamungo ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

Bernad kamungo alizaliwa 2002 katika kambi ya wakimbizi nyarugusu iliyopo wilaya ya Kasulu - Kigoma


Zahanati ya kijiji cha Busunzu - Kibondo
09/06/2026

Zahanati ya kijiji cha Busunzu - Kibondo


Je! Samaki huyu anafahamika kwa jina gani? Karibuni Kigoma kusini (Uvinza)๐Ÿ™
09/06/2026

Je! Samaki huyu anafahamika kwa jina gani? Karibuni Kigoma kusini (Uvinza)๐Ÿ™


WAHAMIAJI HARAMU 96 RAIA WA BURUNDI WAKAMATWA DAR ES SALAAMOfisi ya Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam imefanikiwa kuwak**at...
08/06/2026

WAHAMIAJI HARAMU 96 RAIA WA BURUNDI WAKAMATWA DAR ES SALAAM

Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam imefanikiwa kuwak**ata wahamiaji haramu 96 raia wa Burundi wanaotuhumiwa kwa makosa mbalimbali ya kiuhamiaji kinyume na Sheria ya Uhamiaji Sura ya 54, Kifungu cha 47, Marejeo ya mwaka 2023.

Wahamiaji hao walik**atwa tarehe 7 Juni 2026 katika operesheni maalumu iliyofanyika katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, yakiwemo Jagwani na Kigogo katika Wilaya ya Ilala pamoja na Keko katika Wilaya ya Temeke.

Akitoa taarifa hiyo, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji (SACI) Vincent Haule, amesema kuwa wahamiaji hao watachukuliwa hatua kali za kisheria, ikiwemo kufikishwa mahak**ani mara baada ya kukamilika kwa taratibu za uchunguzi na upelelezi.

SACI Haule amewataka wageni wote wanaoingia na kuishi nchini kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za uhamiaji ili kuepuka kukiuka sheria na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Aidha, amesisitiza kuwa operesheni za kuwabaini na kuwak**ata wahamiaji haramu zinaendelea katika maeneo yote ya Mkoa wa Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya juhudi za Idara ya Uhamiaji katika kuimarisha usalama wa Taifa na kudhibiti uingiaji na ukaaji holela wa wageni nchini.




Muonekano wa kijiji cha Busunzu kilichopo wilaya ya Kibondo, Wรฌlaya hiyo inaendelea na ufungaji wa Taaza barabara na sok...
08/06/2026

Muonekano wa kijiji cha Busunzu kilichopo wilaya ya Kibondo, Wรฌlaya hiyo inaendelea na ufungaji wa Taaza barabara na sokoni kuruhusu shughuli za kiuchumi kuendelea wakati wowote


Miaka sita baada ya kifo cha Pierre Nkurunziza, wananchi wa Burundi wanaadhimisha Siku ya Kitaifa ya Uzalendo sambamba n...
08/06/2026

Miaka sita baada ya kifo cha Pierre Nkurunziza, wananchi wa Burundi wanaadhimisha Siku ya Kitaifa ya Uzalendo sambamba na kumbukumbu ya kiongozi huyo aliyefariki dunia tarehe 8 Juni 2020 kutokana na mshtuko wa moyo akiwa madarakani.

Nkurunziza, aliyeiongoza Burundi kwa miaka 15, anakumbukwa na wafuasi wake kwa mchango wake katika kuimarisha huduma za kijamii.

Katika kipindi chake cha uongozi, alianzisha sera zilizowezesha wanawake wajawazito kupata huduma za kujifungua bila malipo, watoto chini ya miaka mitano kupata matibabu bure, na wanafunzi wa shule za msingi kupata elimu bila malipo.

Maadhimisho ya mwaka huu yanatoa nafasi kwa wananchi wa Burundi kutafakari urithi wake wa kisiasa na kijamii.

Serikali na wananchi wanaendelea kuheshimu kumbukumbu yake huku baadhi ya sera zake muhimu katika sekta za afya na elimu zikiendelea kutekelezwa nchini humo hadi sasa.
๐Ÿ‡ง๐Ÿ‡ฎ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

"Tukisema ukweli bila kupepesa macho Ubaguzi ujiji ni mwingi sana kila sekta ya uchumi wanataka wao wenyewe, mfano soko ...
08/06/2026

"Tukisema ukweli bila kupepesa macho Ubaguzi ujiji ni mwingi sana kila sekta ya uchumi wanataka wao wenyewe, mfano soko kubwa waligawa viwanja hakuna mtu wa inje ya ujiji aliopewa ndio maana soko la ujiji liko vile, folozani hawezi kufanya kazi mtu yoyote tofauti na kijana wa ujiji hivo wamebana ushindani madhara yake ukipeleka mzigo unapigwa bei ya kukukomowa mzigo ungepakiliwa kwa 5000 wao ni 40000

Soko la ujiji litarudi hadi pale watakapoanza kugawa viwanja upya au waliopewa viwanja na ambao hawana uwezo wa kujenga vibanda wanyanganywe wapewe wengine, k**a ulivyosema hapo mwanzo ujiji wakiacha ubaguzi itaendelea bila hivyo hakuna chochote kitakachofanyika jambo muhimu wabadilike "


Address

Kasulu
Kigoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kigoma ndio kwetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share