31/05/2026
UNDANI WA KUIBEZA UJIJI
Tunaona kuna kampeni inaanzishwa na vikundi fulani fulani kuibeza ujiji.
Je, ni kweli unabezwa uduni wa maendeleo ya Ujiji?
Hivi, Baa inaweza kuwa kielelezo cha maendeleo badala ya viwanda na miundombinu?
- Tena ya kumilikiwa na mgeni ambaye si raia wa Tanzania na hainufaishi Watanzania.
- Na sheria ipi inampa mgeni ambaye si raia uhalali wa kumiliki ardhi?, na itatwaliwa iwe masabo.
Uchawi unaweza kuzuia maendeleo?
- Hivi Ujiji kuna uchawi wa namna gani ambao Duniani hakuna wa kudhibiti maendeleo?
- Kigoma mahali gani hapajawahi kusifikana kwa hiyo fani?, kwanini hawasemi?
- Hivi Ujiji ina uchawi kushinda Naijeria kusini?, Mfalme tajiri wa kwanza Afrika ni wa Morocco wa pili ni Olugbo wa Ugbo kutoka Naijeria kusini na kuna matajiri wengi mno na wasomi wengi na wako hukohuko uchawini.
- Huyo anayedai Ujiji kuna uchawi ye uchawi anaujua au yeye ndo mchawi?
- Ameshawahi labda hata kushiriki makongamano ya wachawi akapata uzoefu n ithibati maana kusadiki kwa toma ni kuona.
* Majungu, majungu, majungu na kukosa shule.
Ujiji ni wapi?
- Kwa sisi wenyeji, Ujiji ni sawa na Kigoma mjini na kwa zamani ni sawa na mkoa wote wa Kigoma, ukiwa ni wilaya ya Jimbo la magharibi.
Kubeza maendeleo ya Ujiji ni kutukana serikali na hasa halmashauri ya manispaa ya mji ambayo ndiyo inabeba dhamana kubwa juu ya 'ordinances' za mapato na matumizi mbalimbali ya mji k**a ujenzi wa miundombinu na ukusanyaji wa mapato sambamba na utekelezwaji wa sera za kimaendeleo kwa miongozo na bajeti ya serikali kupitia wizara husika. Serikali ambayo inafanya juhudi kila kukicha kuhakikisha maendeleo na miundombinu vinaimarika.
- Kubeza kinachofanyika na kutotaka kukubali mabadiliko ni silika ya harakati za mageuzi ya kisiasa na siyo za kijamii wala kitamaduni.
Je, Usultani unahusikaje kuzuia maendeleo ya kiuchumi?
- Zaidi Usultani umezidi kuitambulisha ujiji na kurudisha ari ya watu kupapenda nyumbani hii inasaidia kuibua fikra mpya za fursa za kiuchumi na mshik**ano wa kijamii ambao ni muhimu katika kuleta maendeleo.
- Pia Usultani haujawahi hata siku moja kupinga harakati zozote halali za maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
- Wenye uchungu wa ujiji ni magirini tu k**a ni kweli wajikite makwao,
lumbu nguni zhakuta mwinobe zhisizihang'ilwa ngata.
Je, k**a si hivyo kinachobezwa na kutukanwa hapo ni nini?
- Ni chuki tu, wivu, ujinga na kasumba.
Mtu anatoka kale kakijiji ka kituo cha reli cha karibu na Luiche, uchumi wa hako kakijiji ni miwa ya shilingi 500, yeye mwenyewe kwao ana miongo hajafika lakini anapatukana ujiji, eti kwa kigezo ni mji wa zamani unatakiwa kuendelea kabla ya kwao. Hivi hicho kipaumbele ni cha dhati au kisingizio kwao pasisemwe?
Je, kuna nini nyuma ya pazia?
Kuna harakati za kisiasa na kitamaduni....
maendeleo yametumika k**a kichaka. Huwezi kuchagiza maendeleo ya kusiko kwenu tena hujawahi hata kupafika kwa kutoa kashfa na madhaifu ya makazi ya watu ambayo bado wenyewe wamo ndani kwa maneno ya kusikia, kuona picha na kuhisi.
Hivi hata wewe ungejisikiaje?
Wengine wanadiriki kusema watu wa Ujiji wahamishwe....hivi kweli hapo si ni kujificha kwenye shamba la karanga?
Kigoma si ndo ya kwetu sote?
K**a kuhamisha watu ndo kunaleta maendeleo kuna mapori ya hekari ngapi ya bure huko makwao kwanini wasitoe mawazo yakawa miji mizuri wanayotaka kuiona?
Hizi ni harakati za hao wanaharakati mchombezo kutishia uwepo wa jamii yetu na wamekosa njia...chuki iliyoje!!!!
Kibalo ni lijitu kubwa k**a likizimgara ukishindana nalo litakumeza!!
Watu ambao harakati za kijamii za mkoa zikianzishwa wanajimega na kuanzisha vikundi vyao vya kiuasi vyenye sura ya Vicoba na Saccos mchombezo, hawawezi kufika mbali wala kupata mafanikio kwasababu wamekosa baraka kwa usaliti.
Elimu ya mjinga siku zote ni majungu..
Wameachwa na jopo la Kibalo kwa kupuuzwa ila watarudishwa mezani ikiwa wataparama maana tuko nao k**a vivuli vyao.
Muhimu kujikita kwenye hoja na mijadala yenye tija , kibalo kina mbinu zaidi ya 100 kuzima majaribio yasiyo na tija.
Wawe makini, wawe makini, wawe makini.
IDUMU MAKKA NDOGO🤲
IDUMU UJIJI NA BUSAIDI YAKE🤲
UDUMU UUNGWANA WA JAMII YETU 🤲
UDUMU USULTANI WA KIMANYEMA WA KIENEMBONWE WA UJIJI 🤲
ADUMU KOLO MALILO II SULTANI NA KILUNGA WETU🤲