16/04/2026
Tuendelee kujipatia maarifa.
Leo tujifunze: Biblia inasema nini juu divai.
DIBAJI
Divai ni kileo kinachotengenezwa kwa majimaji ya mmea wa zabibu.
Pengine zabibu huitwa pia mvinyo (kutoka Kireno "vinho"). Neno divai linaweza kubeba maana ya vileo vikali zaidi zaidi ya divai.
AINA ZA DIVAI
Kuna aina mbili za divai: divai nyekundu na divai nyeupe.
UANDAAJI
Maji ya zabibu huwa divai kwa kuchachuka kwa sukari iliyomo ndani yake.
Zabibu hupondwa zikiachwa katika chombo kikubwa Kwa kuchachua. Maji ya zabibu huwa na sukari nyingi pamoja na asidi ndani yake inayohitajika kwa ladha inayohitajika.
Divai safi haitakiwi kuongezwa chochote. Nyongeza inatokea k**a sukari iliyopo kwanye zabibu haitoshi. Kazi ya kuchachua inaendelea kutokana na hamira asilia zinazokaa kwenye maganda lakini inawezekana kuongeza hamira k**a iliyomo haitoshi.
HISTORIA
Kuna dalili za kiakiolojia kwamba divai ilianza kupatikana huko Uajemi miaka 5000 KK.
KUENEA
Divai imekuwa sehemu ya utamaduni wa nchi hasa Mashariki ya Kati na nchi kandokano ya Mediterania. Kwa namna ya pekee sana warona wa kale waliipeleka katika sehemu zote za dola lao.
KILIMO CHA MIZABIBU
Kilimo cha mizabibu hutegemea hali ya tabianchi yenye kiwango cha jua cha kutosha na mvua ya wastani. Katika tabianchi za kaskazini mwa Ulaya mizabibu haistawi.
DIVAI KATIKA DINI
Divai iliingia pia katika dini za Misri, Babeli, na Ugiriki ya Kale.
Katika Biblia.
Nuhu anatajwa kuwa mnywaji wa kwanza wa divai. Katika kitabu cha Zaburi divai ni ishara ya furaha wakati kitabu cha Mithali kinatueleza kuwa divai ni dawa ya mwnye huzuni lakini pia kuna maonyo dhidi ya hatari ya ulevi.
Kitabu cha Yishua bin Sira 31: 27 - 29 kinasema "Kwa wanadamu mvinyo ni k**a maji ya uzima, ukinywa kwa kiasi. Je, anao uzima gani mtu mtu asiye na mvinyo? Nayo imeumbwa ili kuwafurahisha wanadamu. Mvinyo ni furaha ya moyo na changamko ya roho, ikinywewa kwa wakati wake na ya kutosha. Lakini kunywa mno ni uchungu wa roho, na fesheha na ugomvi"
Katika Agano jipya Yesu Kristo anatumia divai na mzabibu k**a ishara za uzima wa milele na pia kwa umoja wa watakatifu.
Jinsi ilivyo katika Uyahudi kwanye ibada ya jioni ya Sabato, divai ni sehemu za ibada ya Ekaristi au chakuka cha Bwana.