Society's Survival & Adjustment

Society's Survival & Adjustment Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Society's Survival & Adjustment, Geita.

Najisikia furaha sana kuwatumikia hawa watu wakuu, ambao Mungu ameweka hazina zake ndani yao.Ni wito wangu kwa  wote (vi...
26/04/2025

Najisikia furaha sana kuwatumikia hawa watu wakuu, ambao Mungu ameweka hazina zake ndani yao.Ni wito wangu kwa wote (viongozi wa dini, taasisi mbalimbali na serikali) tuwekeze sana katika kuwafundisha na kuwaelekeza kwa usahihi (tukiwalea na kuwasimamia ) watoto na vijana kwa maana ni hazina na msaada kwa kanisa, jamii na Taifa kwa ujumla. Hivyo tunapaswa tuwaelekeze nini wafanye na nini wasifanye kwa mstakabali wa maisha yao.
Mithali 22:6 "Mlee mtoto katika njia impasayo,Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee."
Kumbukumbu la Torati 6:7 "nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo."

Ni hakika, kulijenga Kanisa na Taifa bora inawezekana!

by Enos Shengoyi.
Mwandishi,Mnenaji na Mwanzilishi wa SSA.
Kwa kujifanza zaidi tembelea ukrasa wangu wa Instagram ⬇️ https://www.instagram.com/enos.shengoyi?igsh=ZGUzMzM3NWJiOQ==

Shirika la Society's Survival & Adjustment (SSA)  pamoja na mashirika mengine (NGO's) zinazofanya kazi zake mkoa wa Geit...
05/02/2025

Shirika la Society's Survival & Adjustment (SSA) pamoja na mashirika mengine (NGO's) zinazofanya kazi zake mkoa wa Geita kwa pamoja tulipata nafasi ya kuhudhuria kikao cha NACONGO mkoa ambapo tulikuwa na mgeni rasmi ambaye pia ndiye M/kt wa bodi ya mashirika Taifa Mhe. Bi. Mwantumu Mahiza aliyewahi kuwa waziri wa Elimu miaka iliyopita.Tunashukuru sana kwa jinsi alivyotutakia heri na kutupongeza viongozi na wadau wote wa NGO's waliohudhuria kikao hicho huku akituelekeza kufanya shughuli zetu kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi.Mwisho tulipata nafasi ya kutoa maoni na ushauri ili kuendelea kulijenga taifa letu.

Society's Survival & Adjustment (SSA)
We build the future!
by Enos Shengoyi
Author & Founder of SSA.

Pamoja na majukumu mbalimbali ya kikazi katika maisha tunayoendelea nayo  ni mhimu na ni wajibu tuhakikishe tunashiriki ...
28/12/2024

Pamoja na majukumu mbalimbali ya kikazi katika maisha tunayoendelea nayo ni mhimu na ni wajibu tuhakikishe tunashiriki na kushirikiana kuona tunatoa malezi sahihi kwa watoto na vijana wetu. Tusiwaachie wasaidizi wa kazi tu, na tusiishie kuwaagiza watoto mara kwa mara wapelekwe na boda boda bila uwepo wetu na uangalizi wetu (wazazi/walezi).Tukifanya hivyo tutawalinda watoto na kulijenga Taifa lenye Maadili.

SSA tunaungana na wadau mbalimbali k**a wanavyofanya gazeti la mwananchi katika kutoa machapisho mbalimbali yenye kuelimisha Jamii.

Society's Survival & Adjustment (SSA)
We Build the Future!
by Enos Shengoyi
Author & Founder of SSA.

Tarehe 30/08/2024 ilikuwa ni kikao kikuu cha mwaka cha mashirika yasiyo ya kiserikali ( NGO's) kilifanyika ktk ukumbi wa...
02/09/2024

Tarehe 30/08/2024 ilikuwa ni kikao kikuu cha mwaka cha mashirika yasiyo ya kiserikali ( NGO's) kilifanyika ktk ukumbi wa EPZ bombambili (ambao pia ni ukumbi wa maonyesho ya teknolojia ya dhahabu- Mkoani Geita) wakurugenzi na wawakilishi kutoka mashirika mbalimbali pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo walihudhuria kikao hicho, walikuwepo maafisa kutoka TRA, GGML, Benki mbalimbali, wanafunzi kutoka S/Sekondari ya Geita Adventist na maafisa maendeleo kutoka halmashauri.
Ni hakika maendeleo yoyote katika jamii na taifa kwa ujumla yanahitaji ushirikishwaji na ushirikiano kutoka kwa wadau na taasisi mbalimbali.

Together We Can!

by Enos Shengoyi
Founder SOCIETY'S SURVIVAL & ADJUSTMENT (SSA)
"We Build The Future"

Ninamshukuru Mungu sana aliyenijalia kibali, nikiwa k**a mdau wa NGO ninayoisimamia  iitwayo Society's Survival & Adjust...
27/06/2024

Ninamshukuru Mungu sana aliyenijalia kibali, nikiwa k**a mdau wa NGO ninayoisimamia iitwayo Society's Survival & Adjustment (SSA) nilipata nafasi ya kualikwa ktk kikao cha wadau wa Malezi, ukatili, na program iitwayo CLM ( Community Lead Monitoring) hapa Mwanza katika ukumbi wa halimashauri ya manispaa ya Ilemelela. Kikao kazi hiki kimefanyika tar 27/06/2024.

by Enos Shengoyi
Founder of SSA

Ninashukuru Mungu kupata nafasi ya kushirikiana na wadau mbalimbali wa Ustawi na Maendeleo ya jamii H/Wilaya ya Geita, n...
13/06/2024

Ninashukuru Mungu kupata nafasi ya kushirikiana na wadau mbalimbali wa Ustawi na Maendeleo ya jamii H/Wilaya ya Geita, nikiwa k**a kiongozi wa Shirika la SSA (Society's Survival & Adjustment) niliambatana na wadau kutoka Shirika la Nelico, Marafiki wa Elimu, RAPO, GGM na Maafisa Maendeleo wa Wilaya kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii ambapo tulitembelea maeneo tofauti tofauti k**a vile Nkome- Mwalo wa makatani pamoja na Senga-Mchangani. Nilitoa elimu kuhusu "MALEZI KWA WATOTO" zaidi nilisisitiza kuwa Malezi kwa watoto yakitolewa kwa usahihi hupelekea Maadili na Maendeleo kwa jamii na taifa." Hii imekuwa ni sehemu ya shughuli ambayo imefanyika katika kuelekea kuazimisha Siku ya Mtoto wa Africa ambayo huazimishwa tar 16/June kila mwaka, ambapo ki- mkoa itaazimishwa katika kata ya Nyamigota-Geita.

SSA " We build the future"
by Enos Shengoyi
(Author & Founder of SSA)

13/06/2024
Tunaishukuru sana Serikali  kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum  kwa kuja na Progra...
21/09/2023

Tunaishukuru sana Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa kuja na Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT- MMMAM)
Programu hii inalenga kuhakikisha jamii yote tunatambua umuhimu wa kuwekeza kwa watoto kwa kutoa malezi sahihi kwa watoto hususani wenye mwaka 0 hadi 8 ili kulijenga Taifa bora. Nikiwa k**a Founder na CEO wa Shirika la SSA tulipata mwaliko wa kushiriki uzinduzi wa programu hii ya Makuzi na Malezi kwa Mtoto ki mkoa (mkoani Geita) Programu hii ilizinduliwa ki mkoa tarehe 21/09/2023. Hakika juhudi za pamoja kwa watu wote zinahitajika kuanzia ngazi ya familia, wazazi/walezi, jamii, wadau na watenda kazi mbalimbali wa mtoto, ni wakati sasa tushik**ane kuhakikisha tunatoa elimu na malezi sahihi kwa watoto ili kulijenga Taifa bora lenye maadili.

Enos Shengoyi
Founder of SSA

Address

Geita

Telephone

0714637370

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Society's Survival & Adjustment posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Society's Survival & Adjustment:

Share