GLORY KWAYU

GLORY KWAYU Life for All Nations Ministry. Huduma hii ni kwa ajili ya kuleta Uzima kwenye Maisha ya watoto wa Mungu na Hatima zao Duniani.

Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.--Yohana 10:10

🇹🇿🇹🇿🎤
22/04/2026

🇹🇿🇹🇿🎤

Ukishaokoka usiwe Mjinga mjinga,Usiwe mvivu,usiwe na visingizio vya kitoto,acha kutia huruma kwa watu,Komaaa na Mungu,Fa...
20/04/2026

Ukishaokoka usiwe Mjinga mjinga,

Usiwe mvivu,usiwe na visingizio vya kitoto,acha kutia huruma kwa watu,

Komaaa na Mungu,Fanya Kazi kwa bidii,Omba sana,Soma neno Sana,Imani yako kwa Mungu isiingiliane na chochote kile,Moyo wako amiliki Yesu peke yake,Vaa vizuri,Nukia Vizuri.

Wewe ni Familia ya Ufalme wa mbinguni ingawa upo Duniani.

Mwl.Gloria Kwayu.
Dodoma-Tanzania.

HEKIMA KWA VIONGOZI..Kiingozi yeyote yule Duniani,Ambaye anaongoza watu siyo wanyama,Anahitaji HEKIMA kutoka kwa Mungu…W...
19/04/2026

HEKIMA KWA VIONGOZI..

Kiingozi yeyote yule Duniani,Ambaye anaongoza watu siyo wanyama,
Anahitaji HEKIMA kutoka kwa Mungu…

Watu ni watu wa Mungu,hizo ni roho zinazotoka kwa Mungu,Mungu anawajua vizuri sana maana wametoka kwake.

Hekima ya Mungu ndani ya Kiongozi ni majibu kwa watu anaowaongoza.

Usiku ule Mungu akamtokea Sulemani, akamwambia, Omba utakalo nikupe.
2 Mambo ya Nyakati 1:7

Sulemani akamwambia Mungu, Umemfanyia baba yangu Daudi fadhili kuu, nawe umenimilikisha mimi badala yake.
2 Mambo ya Nyakati 1:8

Basi sasa, Ee Bwana Mungu, na limyakinie baba yangu Daudi neno lako; maana umenitawaza niwe mfalme juu ya watu wengi k**a mavumbi ya nchi.
2 Mambo ya Nyakati 1:9

Basi sasa nipe hekima na maarifa, nijue kutoka na kuingia mbele ya watu hawa; kwa kuwa ni nani awezaye kuwahukumu watu wako hawa walio wengi?
2 Mambo ya Nyakati 1:10

Naye Mungu akamwambia Sulemani, Kwa sababu neno hili lilikuwamo moyoni mwako, wala hukujitakia mali, wala utajiri, wala utukufu, wala maisha za wakuchukiao, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; bali umejitakia hekima na maarifa, upate kuwahukumu watu wangu, niliokutawaza juu yao;
2 Mambo ya Nyakati 1:11

Uongozi unahitaji Hekima na Maaarifa kutoka kwa Mungu.

……..
Mwl.Glory Kwayu
Dodoma-Tanzania

Elewa unapendwa na Mungu❤️
19/04/2026

Elewa unapendwa na Mungu❤️

KUTOKUZIAMINI KAZI ZA MUNGU NI KUMDHARAU MUNGU.K**a Mkristo ambaye unaona matendo makubwa ya Mungu,Ishara na maajabu yak...
18/04/2026

KUTOKUZIAMINI KAZI ZA MUNGU NI KUMDHARAU MUNGU.

K**a Mkristo ambaye unaona matendo makubwa ya Mungu,Ishara na maajabu yake na bado unasema si kweli hiyo ni sawa na umedharau Mungu.

Unataka kusema Mungu hawezi?

Kwa nini unaona mambo makubwa ambayo yanatokea na bado unasema ni nguvu za giza? kwamba Mungu Hana Nguvu wala uwezo wa kufanya mambo makubwa?

Mtumishi wa Mungu anapofanikiwa kwa nini useme ni utapeli au ni nguvu za giza?kwa nini usiseme huyu ni Mungu!

Imani yako kwa Mungu iko wapi?na kwa nini unajiita Mkristo na huziamini kazi zake?

Bwana akamwuliza Musa, Je! Watu hawa watanidharau hata lini? Wasiniamini hata lini? Nijapokuwa nimefanya ishara hizo zote kati yao.
Hesabu 14:11

K**a ulikuwa huamini shuhuda ambazo watu wengine wametendewa,na kuona Ishara na Miujiza ya Mungu ni utapeli,elewa ulikuwa unamdharau Mungu.

Rudi kwa Mungu.

Mwl.Glory Kwayu
Dodoma-Tanzania

Ukijua Unapendwa na Mungu…
18/04/2026

Ukijua Unapendwa na Mungu…

DALILI YA KUWA MUNGU YUPO NDANI YAKO.Kuna walokole ambao hawajui K**a wameokoka au la!wanataka kuishi K**a dunia inavyot...
15/04/2026

DALILI YA KUWA MUNGU YUPO NDANI YAKO.

Kuna walokole ambao hawajui K**a wameokoka au la!wanataka kuishi K**a dunia inavyotaka na si K**a Mungu anavyotaka.

Hawana uhakika k**a kweli Mungu Yupo ndani yao,na hii ni kitu cha hatari sana kwa Mwamini maana shetani hutumia nafasi hii kudanganganya na kuwarudusha Duniani Tena.

Ukishaokoka huwezi kuishi kiholela tu,Tayari wewe ni Raia wa Mbinguni unayeishi Duniani,ni Balozi wa Kristo hapa Duniani,

Sasa Basi nisiende mbali,Utajuaje Mungu Yupo Ndani yako?

1.hutaki kabisa kutenda dhambi hasa dhambi za siri K**a vile wizi hasa vitu vya kazini,uzinzi,Uongo,masengenyo na unafki.

Kwa sababu Mungu ni Mtakatifu huwa anapenda sana na sisi tuwe watakatifu, baada ya kuokoka.

kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.
1 Petro 1:16

Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.
Zaburi 16:3

Mungu hataki na hapendi mtu apotee Tena baada ya kuokoka,na moja ya kitu kinachopotezaga watu waliokoka ni kurudi kwenye dhambi hasa za siri,anasingizia alipitiwa.

Huku nje unaonekana mlokole safi,ndani yako unafanya mambo ya Siri ambayo ni chukizo kwa Mungu,

Ukijua Mungu Yupo ndani yako,utakuwa ni mtu wa kujiepusha sana na uovu K**a ilivyokuwa kwa Ayubu,hata k**a umebanwa mahali utahakikisha dhambi haikushindi,

2.Utapenda sana Kumpendeza Mungu na kumfurahisha,kwa kuwaleta wengine kwake na Kulisema neno lake kwa Ujasiri.

Utakuwa ni mtu ambaye unaeneza Neno la Mungu ili na wengine waokolewe,utashangaa kwa nini unafanya hivyo,siyo wewe ni Mungu ndani yako,

Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Matendo ya Mitume 1:8

Mungu akiwa ndani ya Mtu ni Raha isiyoelezeka,Unakuwa kiumbe mzuri wa Mbinguni hapa Duniani.

Ongezea na wewe tujifunze pamoja.

Mwl.Glory Kwayu
Dodoma-Tanzania

Ibada…
15/04/2026

Ibada…

Mwanza,Mwanza,Mwanza-Tanzania Bwana Yesu AsifiweHuduma ya Life for All Nations iliyo chini ya Mtumishi wa Mungu  na anay...
14/04/2026

Mwanza,Mwanza,Mwanza-Tanzania
Bwana Yesu Asifiwe

Huduma ya Life for All Nations iliyo chini ya Mtumishi wa Mungu na anayetumika kwa Nguvu za Mungu ,Mwl.Glory Kwayu

Inakukaribisha kwenye Mkesha Mkubwa wa Kujazwa Roho Mtakatifu,ni neno ambalo Mungu amelitaka kwa Majira haya ili kila mmoja aweze kuongozwa na Roho wake hapa Duniani…

Ni usiku wa Ishara na Miujiza kwa nguvu za Roho Mtakatifu….

Ni Tarehe 22/5/2026 siku ya Ijumaa.

Muda:Saa moja kamili mpaka saa kumi na mbili Asubuhi.

UKUMBI WA VIJANA CENTRE,MLANGO MMOJA BARABARA YA UHURU

Njoo wewe na Familia yako,Njoo wewe na Rafiki zako,Njoo wewe na majirani zako,Njoo wewe na wafanyaki wenzako,njoo wewe na wafanyabiashara wenzako,

Ni Usiku utakaobadilisha Maisha yako 100%..

Tutaomba…
Tutapata Maarifa ya Neno la Mungu,
Tutasifu na Kumuabudu Mungu,
Tutaomba,

Neno linasema; Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
-Matendo ya Mitume 1:8

Malango yatakuwa wazi kabisa kuanzia saa moja kamili jioni mpaka saa kumi na mbili Asubuhi,

Kwa Mawasiliano Tuma ujumbe/Piga Simu
-0749-828857
-0765-625055

Watu wote Mnakaribishwa bila kujali Dini yako,kabila lako au dhehebu lako,Mungu ni Mungu wa wote wenye mwili….

Mwl.Glory Kwayu
0775625055

Elewa neno Alitupenda,
14/04/2026

Elewa neno Alitupenda,

Address

Dodoma
Dodoma

Telephone

+255765625055

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when GLORY KWAYU posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to GLORY KWAYU:

Share