15/04/2026
DALILI YA KUWA MUNGU YUPO NDANI YAKO.
Kuna walokole ambao hawajui K**a wameokoka au la!wanataka kuishi K**a dunia inavyotaka na si K**a Mungu anavyotaka.
Hawana uhakika k**a kweli Mungu Yupo ndani yao,na hii ni kitu cha hatari sana kwa Mwamini maana shetani hutumia nafasi hii kudanganganya na kuwarudusha Duniani Tena.
Ukishaokoka huwezi kuishi kiholela tu,Tayari wewe ni Raia wa Mbinguni unayeishi Duniani,ni Balozi wa Kristo hapa Duniani,
Sasa Basi nisiende mbali,Utajuaje Mungu Yupo Ndani yako?
1.hutaki kabisa kutenda dhambi hasa dhambi za siri K**a vile wizi hasa vitu vya kazini,uzinzi,Uongo,masengenyo na unafki.
Kwa sababu Mungu ni Mtakatifu huwa anapenda sana na sisi tuwe watakatifu, baada ya kuokoka.
kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.
1 Petro 1:16
Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.
Zaburi 16:3
Mungu hataki na hapendi mtu apotee Tena baada ya kuokoka,na moja ya kitu kinachopotezaga watu waliokoka ni kurudi kwenye dhambi hasa za siri,anasingizia alipitiwa.
Huku nje unaonekana mlokole safi,ndani yako unafanya mambo ya Siri ambayo ni chukizo kwa Mungu,
Ukijua Mungu Yupo ndani yako,utakuwa ni mtu wa kujiepusha sana na uovu K**a ilivyokuwa kwa Ayubu,hata k**a umebanwa mahali utahakikisha dhambi haikushindi,
2.Utapenda sana Kumpendeza Mungu na kumfurahisha,kwa kuwaleta wengine kwake na Kulisema neno lake kwa Ujasiri.
Utakuwa ni mtu ambaye unaeneza Neno la Mungu ili na wengine waokolewe,utashangaa kwa nini unafanya hivyo,siyo wewe ni Mungu ndani yako,
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Matendo ya Mitume 1:8
Mungu akiwa ndani ya Mtu ni Raha isiyoelezeka,Unakuwa kiumbe mzuri wa Mbinguni hapa Duniani.
Ongezea na wewe tujifunze pamoja.
Mwl.Glory Kwayu
Dodoma-Tanzania