05/09/2025
MUSTAPHA HEB FOUNDATION
Ni taasisi isiyo ya kiserikali iliyoanzishwa na mmiliki wake MUSTAPHA MISUNGWI JIMONDOGWE mnamo mwaka 2025 ikiwa na dhumuni la kuwainua vijana kupitia idara ya afya, elimu na ujasiliamali(biashara)
Taasisi hii inalenga zaidi katika kuwainua vijana hasa wale wanaotokea katika mazingira magumu na familia za kimasikini, aidha taasisi hii imedhamilia katika kurudisha matumaini hasa kwa vijana waliokata tamaa pamoja na kuongeza mwamko wa elimu katika jamii
Taasisi hii imeainisha wazi kwa kujikita katika misingi ya Elimu, Afya Pmoja na Ujasiliamali au biashara ambayo ndiyo misingi mikuu na mzizi mkuu wa maisha ya mwanadamu katika kuelekea kujikwamua kimaisha.
Taasisi hii inatambua uwepo wa changamoto nyingi kwa vijana walio wengi mitaani katika soko la ajira. MUSTAPHA HEB FOUNDATION imejikita pia katika utoaji wa ajira ndogondogo katika biashara ili kupunguza tatizo la ajira inchini paoja na inchi zingine za afrika mashariki na kati
Taasisi hii imebeba matumaini pia kwa watu wenye uhitaji kupitia makundi mbalimbali wakiwemo yatima, wasiojiweza, wazee, walemavu, familia masikini pamoja na wajane
Taasisi hii imelenga pia katika kuelimisha jamii juu ya afya ya jamii kupitia mikutano, semina mbalimbali,pamoja na usambazaji wa nakala za vitabu mbalimbalivinavyotoa elimu juu ya afya katika kulinda afya ya jamii ikiwemo elimu juu ya uelewa wa magonjwa na visababishi vyake, njia bora za kujikinga na magonjwa, madhara ya madawa ya kulevya, malezi bora katika jamii, afya ya uzazi,ulaji ufaao afya, pamoja na kubadili mitindo ya maisha ili kulinda afya zao kimwili, kiakili/kisaikolojia pamoja na kiroho
Aidha taasisi hii imelenga kuwawezesha vijana hasa wanaotoka katika mazingira magumu kwa kuwasomesha na kuwapatia mahitaji yao ili kuwasaidia kutimiza malengo yao kupitia elimu.
Kwa kushirikiana na serikali kupitia sekta ya Elimu, taasisi hii imelenga kuandaa vitabu maalumu katika kuwawezesha wanafunzi mashuleni kujitambua, kujua mbinu sahihi za usomaji, mbinu za ujibuji mitihani,, namna sahihi na jinsi ya kufaulu masomo yote ya sekondari, mbinu za kuwa mwanafunzi bora shuleni. Na miongozo yote ya usomaji na namna ya ujibuji wa maswali katika somo husika.
Aidha katika kulitekeleza hili, taasisi hii itatoa semina kwa wanafunzi katika mashule kwa kuwaelimisha na kuwafundisha juu ya umuhimu wa elimu na kisha kuwapatia vitabu vya miongozo yote, hasa katika shule za kata na shule zote zilizopo vijijini ambako mwamuko wa elimu bado ni kidogo.
Taasisi hii pia imelenga katika kuandaa miradi mbalimbali ya kibiashara itakayowezesha kupunguza tatizo la ajira inchini kwa kuajiri vijana zaidi ya 200 kila mwaka kupitia biashara na miradi mbalimbali ikiwemo kilimo na ufugaji,bustani, ufundi pamoja na mengineyo
Taasisi hii imelenga kufungua na kuanzisha miradi mbalimbali ya kibiashara katika kuajiri vijana ikiwemo maduka, stationary, studio/library, kumbi za mpira na mikutano, maduka ya madawa, vituo vya kuchoma chipsi, kumbi za starehe k**a vile baa, hoteli, migahahawa na cafeteria, vituo vya kutengeneza juice za matunda na juice ya muwa, nyama choma, maduka ya vinywaji, maduka ya nafaka na bidhaa za sokoni, maduka ya aina zote, ufundi seremala, ufundi cherehani, saloon za k**e, maduka ya vitabu na maktaba ya kisasa pamoja na computer lab, mitambo ya bustani za mbogamboga na matunda pamoja na mazao mengine, ufugaji wa ng”ombe wa kisasa wa maziwa, kuku wa mayai pamoja na viwanda vingine vidogovidogo vya kuteneneza sabuni na kufuga samaki.
WELLCOME Mustapha HEB Foundation
SUPPORT YAKO NDIYO MAFANIKIO YA TAASISI HII
Mawasiliano
Manager: 0766232427