15/05/2026
Tusisubiri kuwa na uwezo mkubwa ndipo tushiriki kuwainua wengine. Kila mtoto anayepata elimu leo hujengwa kuwa kijana mwenye maadili, maono na mchango chanya kwa jamii ya kesho.” ❤️
“Uwekezaji kwa watoto na vijana si hisani pekee, bali ni ujenzi wa rasilimali watu na mustakabali wa taifa. Uharakati wa kweli ni kusimamia haki yao ya kupata elimu, malezi bora na fursa sawa za kuendelea kielimu.”
“Na hakuna zawadi kubwa k**a kuona tabasamu la mtoto anayehisi kuthaminiwa, kusikilizwa na kupewa matumaini ya maisha bora. Tabasamu lao ni ishara kuwa bado tuna nafasi ya kuibadilisha dunia kupitia upendo, elimu na mshik**ano.”
Katika ziara ya kijamii iliyofanywa na WAYCO Organization katika visiwa vya Wilaya ya Nansio, Ukerewe mkoani Mwanza, Mkurugenzi wa WAYCO, Dr. Florah Msuya, alitembelea maeneo ya visiwani humo na kukutana na mtoto aitwaye Joseph, mwenye umri wa miaka 9, anayesoma darasa la pili.
Joseph anaishi na babu na bibi yake katika mazingira ya visiwani yenye changamoto za kijamii na kiuchumi. Babu yake ni mlemavu, hali inayofanya familia hiyo kuwa katika hali ngumu zaidi ya maisha, ikiwa na changamoto za kupata mahitaji ya msingi k**a elimu, chakula na huduma za afya.
Pamoja na mazingira hayo, Joseph anaendelea kuonyesha bidii na matumaini makubwa katika masomo yake, jambo lililogusa sana moyo wa timu ya WAYCO Organization.
Ziara hiyo ililenga kuona hali halisi ya maisha ya watoto wanaoishi visiwani, na kuhamasisha jamii na wadau mbalimbali kushirikiana kuwasaidia watoto k**a Joseph ili wasikose haki yao ya elimu na malezi bora.
Kisa cha Joseph kinatukumbusha kuwa hata katika maeneo ya visiwani, kuna watoto wenye ndoto kubwa wanaohitaji mikono ya upendo kuwainua.