Ubungo Scouts Local Association

Ubungo Scouts Local Association OFFICIAL PAGE FOR UBUNGO SCOUTS LOCAL ASSOCIATION - The Largest Youth Movement in Tanzania.

UKAGUZI WA ASUBUHI WA KAMBI YA MASHINDANO – GOBA SEKONDARIAsubuhi ya leo, Watahini wa Kambi ya Mashindano walifanya ukag...
12/06/2026

UKAGUZI WA ASUBUHI WA KAMBI YA MASHINDANO – GOBA SEKONDARI

Asubuhi ya leo, Watahini wa Kambi ya Mashindano walifanya ukaguzi maalum kwa kutembelea vikosi mbalimbali vilivyoweka kambi katika Shule ya Sekondari Goba. Ukaguzi huo ulilenga kutathmini utekelezaji wa stadi za Skauti, usafi wa kambi, ubora wa miundo ya kambini, nidhamu, mpangilio wa vifaa pamoja na uwezo wa Skauti kuishi kwa kuzingatia misingi ya Scouting.

Katika zoezi hilo, kila kikosi kilipata nafasi ya kuwasilisha kazi na ubunifu wake mbele ya Watahini huku kikionyesha umahiri katika matumizi ya kamba, ujenzi wa miundo ya kambini, uhifadhi wa mazingira na uendeshaji wa shughuli za kila siku kambini.

Ukaguzi wa asubuhi ni sehemu muhimu ya mashindano kwani huwapa Skauti fursa ya kupimwa maarifa yao kwa vitendo na kujifunza maeneo yanayohitaji kuboreshwa. Aidha, hujenga moyo wa uwajibikaji, umoja, uongozi na ushindani wenye afya kati ya vikosi vinavyoshiriki.

Hongereni kwa vikosi vyote vinavyoendelea kuonyesha ari, nidhamu na kujituma katika shughuli za kambi. Endeleeni kuzingatia Ahadi na Sheria za Skauti huku mkionesha mfano bora wa vijana wenye maadili na uzalendo.

📍 Goba Sekondari
📅 12 Juni 2026





Karibu kushuhudia ufunguzi rasmi wa Kambi ya Mashindano ya Skauti na Jukwaa la Vijana Mkoa wa Dar es Salaam. Pamoja tuna...
11/06/2026

Karibu kushuhudia ufunguzi rasmi wa Kambi ya Mashindano ya Skauti na Jukwaa la Vijana Mkoa wa Dar es Salaam. Pamoja tunajenga kizazi cha viongozi wenye maadili, uzalendo na uwajibikaji.

Mgeni rasmi atakua Mlezi wa Skauti wilaya ya Ubungo, Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Albert Msando.






02/06/2026

JUKWAA LA VIJANA LA 3 SKAUTI MKOA WA DAR ES SALAAM

UBUNGO TUNASEMA KARIBUNI GOBA, KARIBUNI NYUMBANI!

UONGOZI WA SKAUTI UBUNGO WAAMBATANA NA MKOA KUKAGUA ENEO LA KAMBI GOBA SEKONDARILeo tarehe 01 Juni 2026, viongozi wa Ska...
02/06/2026

UONGOZI WA SKAUTI UBUNGO WAAMBATANA NA MKOA KUKAGUA ENEO LA KAMBI GOBA SEKONDARI

Leo tarehe 01 Juni 2026, viongozi wa Skauti kutoka Wilaya ya Ubungo walifanya ziara maalum katika Shule ya Sekondari Goba kwa kushirikiana na viongozi wa Mkoa kwa lengo la kukagua na kutathmini eneo litakalotumika kwa shughuli za kambi za Skauti.

Ziara hiyo imelenga kuhakikisha mazingira yanakidhi mahitaji ya kambi, usalama wa washiriki pamoja na kuweka mikakati bora ya maandalizi ya shughuli zijazo za Skauti. Ushirikiano huu unaonesha dhamira ya viongozi katika kuendelea kuimarisha programu za Skauti na kutoa fursa bora za kujifunza, kuongoza na kuhudumia jamii kwa vijana.

Pamoja tunajenga kizazi chenye maadili, ujuzi na uzalendo kupitia Skauti.

EID MUBARAK
27/05/2026

EID MUBARAK

26/05/2026

MSTAHIKI MEYA WA MWANISPAA YA UBUNGO ANAWAKARIBISHA SKAUTI WOTE KATIKA KAMBI YA KIELIMU NA JUKWAA LA VIJANA SKAUTI MKOA WA DAR ES SALAAM LITAKALOFANYIKA GOBA UBUNGO KUANZIA TAREHE 11 HADI 15 MWEZI JUNI 2026.

12/05/2026

Uongozi wa Skauti wilaya ya Ubungo unayofuraha kuwakaribisha Skauti wote kutoka Wilaya zote, Kinondoni, Kigamboni, Temeke pamoja na Ilala kuja kushiriki tukio la Ki mkoa la Kambi ya Kielimu na Jukwaa la Vijana Skauti.

Tukio linalotarajjwa kuanza tarehe 11 hadi tarehe 15 Mwezi Juni 2026, katika Viwanja vya Goba.

Aidha, kwenye tukio hilo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ya Ubungo, Mheshimiwa Albert Gasper Msando.

Uongozi wa Skauti wilaya ya Ubungo unapenda kuwatakia kila la heri, Wanafunzi wa kidato cha sita kote nchini, Ambao wana...
04/05/2026

Uongozi wa Skauti wilaya ya Ubungo unapenda kuwatakia kila la heri, Wanafunzi wa kidato cha sita kote nchini, Ambao wanatarajia kuanza Mitihani yao ya Mwisho (NECTA) Leo tarehe 04 Mei 2026. Tunawaombea Mwenyezi Mungu akawatangulie na kuwalinda kipindi chote cha Mitihani yenu.

  Katika ziara yake huko Annaba, Algeria, Kiongozi Mkuu wa kanisa Katolili Duniani,  Pope Leo XIV alikutana na vijana wa...
03/05/2026



Katika ziara yake huko Annaba, Algeria, Kiongozi Mkuu wa kanisa Katolili Duniani, Pope Leo XIV alikutana na vijana wa Skauti wa Kiislamu wa Algeria na kushiriki nao kupanda mti wa mzeituni k**a ishara ya amani na umoja. 🕊️

Tukio hilo lilifanyika katika eneo la kihistoria la Hippo na kuwakutanisha Skauti pamoja na viongozi kutoka jamii za Kiislamu na Kikatoliki, likionyesha umuhimu wa mshik**ano, maelewano na kuhudumiana katika jamii. ⚜️

Kupitia shughuli zao za kuwawezesha vijana, kujenga uongozi na kushiriki katika maendeleo ya jamii, Skauti wa Algeria wanaendelea kuwa mfano mzuri wa amani na umoja duniani.




HAPPY WORKER'S DAY 01 MAY
01/05/2026

HAPPY WORKER'S DAY 01 MAY

Address

Mbezi Mwisho
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 16:00
Tuesday 09:00 - 16:00
Wednesday 09:00 - 16:00
Thursday 09:00 - 16:00
Friday 09:00 - 16:00
Saturday 09:00 - 12:00

Telephone

+255682842123

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ubungo Scouts Local Association posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Ubungo Scouts Local Association:

Share