13/08/2026
Kuelekea hatua inayofuata ya First Foods Africa: Mwongozo wa kimkakati na hatua za kipaumbele.
Wiki hii, Wizara ya Viwanda Biashara , kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Tanzania na UNICEF, iliitisha Kamati ya Ushauri ya Kiufundi ya First Foods Africa (FFA), iliyowakutanisha taasisi za Serikali kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, wasomi, washirika wa maendeleo na wataalamu wa kiufundi.
Mkutano huo ulilenga kuimarisha hatua za pamoja za kuboresha lishe ya watoto wadogo, ikiwemo kuongeza upatikanaji wa vyakula vya kwanza vyenye lishe, salama na vya bei nafuu; kuimarisha sera wezeshi; na kuchochea mahitaji ya lishe bora.
Kupitia First Foods Africa, wadau wanaendelea kushirikiana kuhakikisha kila mtoto mdogo anapata vyakula vya kwanza vyenye lishe anavyohitaji ili kukua na kuendelea vizuri.