08/01/2026
📌KIKAO CHA KIMILA – 6 JANUARY 2026
Taasisi ya MAASAI COMMUNITY CULTURE RESERVE FOUNDATION ilifanya kikao muhimu cha kimila siku ya Jumanne tarehe 6 Januari 2026, ambapo wajumbe na viongozi wa kimila walikaa pamoja kujadili masuala mbalimbali yanayohusu mustakabali wa taasisi yetu na jamii kwa ujumla.
Katika kikao hicho, mjadala mpana ulifanyika kuhusu maandalizi ya sinema maalum inayolenga kushirikiana na Serikali katika kutafuta na kuangazia kwa kina chanzo cha ukeketaji kwa watoto wa k**e, ikiwa ni sehemu ya mapambano ya kulinda haki na usalama wa mtoto wa k**e. Kwa furaha kubwa, mpango huu unaelekea kufikia tamati muda si mrefu ujao.
Aidha, taasisi ya Safari Channel imeonesha dhamira ya dhati kwa kuomba kushirikiana na MAASAI COMMUNITY CULTURE RESERVE FOUNDATION, na kuahidi kutoa ushirikiano na msaada wao katika kila hatua hadi kufikia tamati ya mradi huu muhimu. Viongozi wa kimila hawakusita kutoa pongezi za dhati kwa Safari Channel kwa moyo wao wa kujitolea, ushirikiano na sapoti waliyoendelea kuitoa.
🙏 Tunawashukuru wadau wote kwa kuendelea kuwa nasi katika safari hii ya kulinda mila, utamaduni na haki za mtoto wa k**e.
📢 Endelea kuwa nasi tukiendelea kukujuza hatua kwa hatua kuhusu yote yatakayojiri.
.