BUFADESO

BUFADESO Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from BUFADESO, Community Organization, Kunzugu ward, Bunda.

Bunda Farmers Development Support Organization is a member based organization focusing on empowering small-holder farmers and develop their capacity to adapt different sustainable farming techniques. BUFADESO ni shirika la kusaidia maendeleo ya wakulima lililopo wilayani Bunda lenye usajili namba 00NGO/00010200 chini ya sheria No 24 ya mwaka 2002 sehemu ya 12(2) ya mashirika yasiyo ya kiserikali.

Leo, BUFADESO imepokea timu kutoka Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania  (TVLA) – Kituo cha Meatu kwa ajili ya kikao...
01/09/2026

Leo, BUFADESO imepokea timu kutoka Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) – Kituo cha Meatu kwa ajili ya kikao kifupi cha kujifunza kuhusu majukumu ya taasisi zetu, kubadilishana uzoefu na kuchunguza fursa za kuimarisha ushirikiano.

Mkutano huu pia ulitoa fursa ya kuhusianisha kazi zetu na Programu ya Agroforestry for Sustainable Livelihoods, Biodiversity and Climate Change (ASILIB-CC), hususan katika kuendeleza mifumo ya UFUGAJI bora na inayostahimili changamoto, inayoboresha maisha ya wakulima huku ikisaidia kulinda mazingira.

Pia tulipata fursa ya kuwaalika TVLA–Meatu kushiriki katika Maonesho ya Kilimo, yatakayofanyika tarehe 19–21 Oktoba 2026 katika Agroforestry Training Centre (ATC), Bweri, Manispaa ya Musoma, Mkoa wa Mara.

Maonesho hayo yatawakutanisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kuonesha maarifa ya vitendo, ubunifu, teknolojia na uzoefu unaoweza kuchangia katika kuboresha maisha, kujenga ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kuongeza uwekezaji katika kilimo-misitu.

TVLA–Meatu imealikwa kushiriki kupitia banda la maonesho au jukwaa lingine linalofaa, ili kutoa nafasi ya kushirikisha wakulima na washiriki wengine maarifa na taarifa muhimu kuhusu afya na huduma za mifugo.

Habari,Tunayo furaha kukukaribisha kujiunga na Tanzania Agroforestry Stakeholders Platform (TASP) — jukwaa linalolenga k...
31/08/2026

Habari,

Tunayo furaha kukukaribisha kujiunga na Tanzania Agroforestry Stakeholders Platform (TASP) — jukwaa linalolenga kuwaunganisha wadau mbalimbali wa kilimomisitu nchini Tanzania ili kuimarisha ushirikiano, kubadilishana maarifa na uzoefu, kuhamasisha uwekezaji, na kuchochea sera na utekelezaji wa kilimomisitu kwa maendeleo endelevu.

Endapo wewe au taasisi yako mngependa kuwa sehemu ya jukwaa hili, tafadhali jaza fomu ya usajili kupitia link ifuatayo:

https://ee.kobotoolbox.org/x/Y5oefggp

Fomu inapatikana kwa Kiswahili na inachukua dakika chache kuijaza. Taarifa utakazotoa zitatumika kwa ajili ya usajili, mawasiliano na uunganishaji wa wadau ndani ya TASP pekee.

Karibu sana.

Siku ya jana na leo BUFADESO tumetembelewa na   kwa ajili ya kukusanya taarifa za awali kwa wakulima tunaofanya nao kazi...
22/08/2026

Siku ya jana na leo BUFADESO tumetembelewa na kwa ajili ya kukusanya taarifa za awali kwa wakulima tunaofanya nao kazi kupitia Programu ya ASILIB-CC, Lengo ikiwa ni kupata taarifa za awali zitakazosaidia kubaini hatua mbalimbali ambazo wakulima watakuwa wakiendelea kunufaika kupitia ASILIB-CC imekuwa ni wakati mzuri wa kupata malengo na matarajio ya wakulima kuhusu utekelezaji na namna watakavonufaika na Programu ya ASILIB-CC

🌱🎙️ KILIMO NA UFUGAJI | MAZINGIRA FM📻 Jumapili | Saa 1:00–2:00 JioniJe, unajua faida za Maonesho ya Wakulima Nane Nane k...
14/08/2026

🌱🎙️ KILIMO NA UFUGAJI | MAZINGIRA FM

📻 Jumapili | Saa 1:00–2:00 Jioni

Je, unajua faida za Maonesho ya Wakulima Nane Nane kwa wakulima na wadau wa kilimo? 🌾🐄

Jumapili hii, Baraka Kamese kutoka BUFADESO atakuwa kwenye kipindi cha KILIMO NA UFUGAJI kupitia MAZINGIRA FM 91.7, akizungumzia:

🌾 Faida za Maonesho ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika mwezi Agosti
🌳 Mipango ya Maonesho ya KilimoMisitu yanayotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba
🤝 Fursa za kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuunganisha wakulima na wadau wa maendeleo.

📡 JINSI YA KUSIKILIZA:
📻 Kanda ya Ziwa: 91.7 MHz
🌍 Duniani kote: Kupitia mtandao wa radiotadio.co.tz/mazingirafm/

📢 Usikose!
Jumapili hii, saa 1:00 hadi 2:00 jioni, kupitia MAZINGIRA FM.

Tunaungana na vijana duniani kote kusherehekea nguvu, ubunifu, uthabiti na nafasi yao muhimu katika kujenga kesho iliyo ...
12/08/2026

Tunaungana na vijana duniani kote kusherehekea nguvu, ubunifu, uthabiti na nafasi yao muhimu katika kujenga kesho iliyo bora.
“Mazingira Tofauti, Fursa Sawa kwa Vijana.”
Vijana wanahitaji mazingira wezeshi, fursa sawa na nafasi zenye maana za kushiriki, kubuni na kuchangia katika maendeleo endelevu.
🌱 Bufadeso - kwa Maendeleo ya Wakulima.

Leo, 8 Agosti 2026, kutoka Viwanja vya Nyakabindi, Bariadi – Simiyu, BUFADESO  inaungana na taifa kusherehekea mkulima —...
08/08/2026

Leo, 8 Agosti 2026, kutoka Viwanja vya Nyakabindi, Bariadi – Simiyu, BUFADESO inaungana na taifa kusherehekea mkulima — mhimili wa uchumi, chakula na maendeleo ya Tanzania. 🌱👩🏽‍🌾👨🏽‍🌾

🤝 Tukiwa pamoja na wakulima na wadau mbalimbali, tunaendelea kusukuma mbele kilimo chenye tija, masoko yenye fursa, teknolojia, kilimomisitu na uhimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

📢 “Tambua Soko; Ongezea Tija Kutekeleza Dira 2050.”

💚 BUFADESO inaamini: Mkulima akipata maarifa + tija + soko = familia imara, jamii imara na Tanzania yenye maendeleo endelevu.

🌾 TUSHIRIKIANE. TUONGEZE TIJA. TUTAMBUA MASOKO. TUJENGE DIRA 2050.

BUFADESO – Kwa Maendeleo ya Wakulima. 🌱🇹🇿

BUFADESO  inawatakia wakulima, wafugaji, wajasiriamali na wadau wote wa sekta ya kilimo Nane Nane yenye mafanikio na tij...
08/08/2026

BUFADESO inawatakia wakulima, wafugaji, wajasiriamali na wadau wote wa sekta ya kilimo Nane Nane yenye mafanikio na tija.
Nane Nane ni wakati wa kutambua na kuthamini mchango wa wakulima katika usalama wa chakula, uchumi wa kaya na maendeleo ya taifa. 🌱🤝

Katika BUFADESO, tunaendelea kushirikiana na wakulima kuimarisha kilimo endelevu, kilimomisitu, uhifadhi wa mazingira, kuongeza uzalishaji na kujenga maisha yenye ustahimilivu.

📢 Kauli Mbiu ya Nane Nane 2026:
“Tambua Soko, Zalisha kwa Tija Kutekeleza Dira 2050.”

🌳 Tuzalishe kwa tija.
🧺 Tufikie masoko yenye uhakika.
🌍 Tulinde mazingira kwa kizazi cha sasa na kijacho.

BUFADESO - Kwa Maendeleo ya Wakulima!

Katika ziara ya Mwenge wa Uhuru wilayani Butiama, uliokuwa ukizindua na kuweka mawe ya msingi kwa miradi mbalimbali ya m...
02/08/2026

Katika ziara ya Mwenge wa Uhuru wilayani Butiama, uliokuwa ukizindua na kuweka mawe ya msingi kwa miradi mbalimbali ya maendeleo, BUFADESO ilipata fursa ya kushiriki katika zoezi la upandaji miti katika Kituo cha Afya cha Kukirango. Ushiriki huu unaonyesha dhamira yetu ya kuhifadhi mazingira, kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kujenga jamii zenye afya na ustahimilivu. Kwa pamoja tunaendelea kukuza Tanzania ya kijani na maendeleo endelevu. 🌱🇹🇿

🌳 USAJILI UMEFUNGULIWA RASMI! 🌳Je, wewe ni mkulima, kijana, mtafiti, mwanafunzi, mdau wa maendeleo, mfanyabiashara, au u...
12/07/2026

🌳 USAJILI UMEFUNGULIWA RASMI! 🌳

Je, wewe ni mkulima, kijana, mtafiti, mwanafunzi, mdau wa maendeleo, mfanyabiashara, au unapenda masuala ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi?

Usikose kushiriki Kongamano la 11 la Kitaifa la Kilimomisitu (11th Annual Agroforestry Symposium 2026) litakalofanyika:

📅 19–21 Oktoba 2026
📍 ATC, Bweri – Musoma, Tanzania

🟢 Kaulimbiu: Kilimomisitu kwa Vijana na Uwekezaji wa Kijani (Agroforestry for Youth and Green Investment).

Utapata fursa ya:
✅ Kujifunza kutoka kwa wataalamu mbalimbali.
✅ Kubadilishana uzoefu na washiriki kutoka sekta mbalimbali.
✅ Kujenga mtandao wa kitaaluma na kibiashara.
✅ Kujadili suluhisho za kilimo endelevu, uhifadhi wa mazingira, na uwekezaji wa kijani.

🚨!
Usajili umefunguliwa sasa na utafungwa rasmi tarehe 10 Oktoba 2026. Jisajiri kupitia fomu ya mtandaoni kwa kiunganishi: https://ee.kobotoolbox.org/x/XpK00tEg

Usisubiri hadi dakika za mwisho! Jisajili mapema ili kuhakikisha nafasi yako katika kongamano hili muhimu.

🌱 "Panapostawi Miti, Watu Hustawi."

🇹🇿 HERI YA SIKUKUU YA SABASABA 🇹🇿Leo, tarehe 7 Julai, tunaungana na Watanzania wote kuadhimisha  Siku ya Sabasaba—siku i...
07/07/2026

🇹🇿 HERI YA SIKUKUU YA SABASABA 🇹🇿

Leo, tarehe 7 Julai, tunaungana na Watanzania wote kuadhimisha Siku ya Sabasaba—siku inayokumbusha umuhimu wa biashara, viwanda, ubunifu na ujasiriamali katika kukuza uchumi wa taifa letu.

Ni fursa ya kuthamini jitihada za wafanyabiashara, wakulima, wajasiriamali, wawekezaji na wadau wote wanaochangia maendeleo ya Tanzania kupitia uzalishaji na biashara.

Tuendelee kufanya kazi kwa bidii, kuunga mkono bidhaa na huduma za ndani, na kutumia ubunifu kujenga uchumi imara na wenye ushindani.

Heri ya Siku ya Sabasaba!
Tanzania Imara, Uchumi Imara. 🇹🇿

Address

Kunzugu Ward
Bunda
P.O.BOX95

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Telephone

+255787926671

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BUFADESO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share