BUFADESO

BUFADESO Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from BUFADESO, Community Organization, Kunzugu ward, Bunda.

Bunda Farmers Development Support Organization is a member based organization focusing on empowering small-holder farmers and develop their capacity to adapt different sustainable farming techniques. BUFADESO ni shirika la kusaidia maendeleo ya wakulima lililopo wilayani Bunda lenye usajili namba 00NGO/00010200 chini ya sheria No 24 ya mwaka 2002 sehemu ya 12(2) ya mashirika yasiyo ya kiserikali.

🌱 KARIBU USIKILIZE KIPINDI MAALUM CHA MAZINGIRA FM 91.7 🌱Leo Jumapili, tarehe 31 Mei 2026, kuanzia saa 1:00 hadi saa 2:0...
31/05/2026

🌱 KARIBU USIKILIZE KIPINDI MAALUM CHA MAZINGIRA FM 91.7 🌱

Leo Jumapili, tarehe 31 Mei 2026, kuanzia saa 1:00 hadi saa 2:00 jioni, Mkurugenzi Mtendaji wa BUFADESO, Baraka Kamese, atakuwa mgeni maalum katika kipindi cha Mazingira FM.

Mada: *Umuhimu wa Utunzaji wa Mazingira kuelekea Siku ya Mazingira Duniani.*

Usikose kufuatilia mjadala huu muhimu kuhusu wajibu wetu katika kulinda mazingira, kuhifadhi bioanuwai, na kujenga maisha bora kwa kizazi cha sasa na kijacho.

📻 Sikiliza kupitia Mazingira FM 91.7
🌐 Mtandaoni: https://radiotadio.co.tz/mazingirafm/

🌙 Eid Al-Adha Mubarak 🌙BUFADESO inawatakia Waislamu wote nchini Tanzania na duniani kote heri ya Sikukuu ya Eid Al-Adha....
27/05/2026

🌙 Eid Al-Adha Mubarak 🌙

BUFADESO inawatakia Waislamu wote nchini Tanzania na duniani kote heri ya Sikukuu ya Eid Al-Adha.

Tunawatakia siku yenye amani, upendo, mshik**ano na baraka tele kwa familia na jamii zenu. Sikukuu hii iwe chachu ya kuendeleza moyo wa kujitolea, kusaidiana na kuhurumiana katika jamii.

Eid Mubarak! 🤲✨

🎉HAPPY WORLD BIODIVERSITY DAY🎉🌍🌱 On this World Biodiversity Day, we join the global community in embracing this year’s t...
22/05/2026

🎉HAPPY WORLD BIODIVERSITY DAY🎉

🌍🌱 On this World Biodiversity Day, we join the global community in embracing this year’s theme: “Acting Locally for Global Impact.”

Through the ASILIB-CC Program, local communities are becoming key drivers of biodiversity conservation and climate resilience. By supporting farmer-managed tree nurseries, promoting agroforestry practices, restoring degraded landscapes, and strengthening community awareness on sustainable natural resource management, the program is contributing to healthier ecosystems and improved livelihoods.

Every tree planted, every farm restored, and every community empowered represents a local action with a lasting global impact. Biodiversity conservation is not only about protecting nature — it is about securing food systems, water sources, climate stability, and future generations.

As we celebrate this important day, we reaffirm our commitment to working hand in hand with communities to protect biodiversity while promoting sustainable development.

Leo mashirika wabia wa program ya   tumefanya kikao cha pili cha maandalizi ya Maonesho ya Kilimomisitu yatakayofanyika ...
21/05/2026

Leo mashirika wabia wa program ya tumefanya kikao cha pili cha maandalizi ya Maonesho ya Kilimomisitu yatakayofanyika mwezi Oktoba mwaka huu. Kikao hiki kimewakutanisha wadau mbalimbali kujadili maandalizi muhimu kwa ajili ya kuhakikisha maonesho yanafanyika kwa mafanikio makubwa.

Maonesho haya yanalenga kuendelea kuhamasisha uwekezaji katika kilimomisitu, uhifadhi wa mazingira, kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuwainua vijana kupitia fursa mbalimbali zinazotokana na sekta ya kilimo na misitu.🌱🌳





Wakulima chini ya Programu ya ASILIB CC wanaendelea kujengewa uwezo katika kilimo endelevu kupitia mafunzo na uwezeshaji...
20/05/2026

Wakulima chini ya Programu ya ASILIB CC wanaendelea kujengewa uwezo katika kilimo endelevu kupitia mafunzo na uwezeshaji wa uanzishaji na usimamizi wa vitalu vya miti vinavyoendeshwa na wakulima wenyewe. 🌱

Mpango huu unalenga kuimarisha ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, kuboresha maisha ya jamii, na kuhamasisha uhifadhi wa mazingira katika jamii za maeneo husika. Kupitia juhudi hizi, wakulima wanapata maarifa kuhusu uzalishaji wa miche, usimamizi wa vitalu, na umuhimu wa kilimomisitu katika kurejesha mifumo ya ikolojia na kuongeza kipato cha kaya.

Vitalu vya miti vinavyoendeshwa na wakulima vinaendelea kuleta fursa za mazingira ya kijani, kuongeza ushiriki wa jamii, na kuhakikisha maendeleo endelevu ya muda mrefu. Kwa pamoja, tunaendelea kupanda mbegu za mazingira bora na mustakabali wenye ustahimilivu zaidi. 🌍💚

BUFADESO inashiriki katika Warsha ya Ubunifu wa Mawazo (Ideation) na Usimulizi wa Hadithi (Storytelling) iliyofanyika Mu...
18/05/2026

BUFADESO inashiriki katika Warsha ya Ubunifu wa Mawazo (Ideation) na Usimulizi wa Hadithi (Storytelling) iliyofanyika Musoma kwa washirika wa programu ya ASILIB-CC Program.

Warsha hii inatoa nafasi muhimu ya kujifunza na kuimarisha uwezo wa mawasiliano, ubunifu, na usimulizi wa matokeo yanayoonyesha mafanikio, changamoto, na athari chanya za shughuli za kilimomisitu na uhifadhi wa mazingira katika jamii.

Tunathamini fursa hii ya kujifunza, kushirikiana, na kubadilishana uzoefu pamoja na wadau wengine wanaojitolea kujenga jamii imara na endelevu. 🌱


Wakulima wawezeshaji kutoka shirika la BUFADESO wameshiriki katika Mafunzo ya LISHE NA UHAKIKA WA CHAKULA KATIKA KAYA.Ma...
14/05/2026

Wakulima wawezeshaji kutoka shirika la BUFADESO wameshiriki katika Mafunzo ya LISHE NA UHAKIKA WA CHAKULA KATIKA KAYA.Mafunzo haya ya siku mbili yamejumuisha ushiriki wa wawezeshaji jamii kutoka kata za Bukabwa, Muriaza, Kukirango na Bwiregi. Shirika la The Centre for Counselling, Nutrition and Health Care (COUNSENUTH) linaongoza mafunzo haya kupitia programu ya . Kupitia mafunzo haya wawezeshaji jamii wataongeza uelewa wa:-
🥗Masuala ya msingi ya lishe
🥦Makundi ya chakula na mlo kamili
🍇Matatizo makuu ya lishe nchini
🥝Kupanga mlo kamili
🫘Uhakika wa chakula katika kaya.
Mafunzo haya yataongeza uelewa kwa wawezeshaji jamii ili kufikia na kuelimisha jamii .

Tunawatakia Watanzania wote maadhimisho mema ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar 🤝🇹🇿Kauli mbiu:Miaka 62 ya Muungano: A...
26/04/2026

Tunawatakia Watanzania wote maadhimisho mema ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar 🤝

🇹🇿Kauli mbiu:
Miaka 62 ya Muungano: AMANI,UMOJA NA MSHIKAMANO NI MSINGI WA MAENDELEO ENDELEVU

FAIDA ZA KILIMOMISITU 🌳🌾Je, unajua kuwa unaweza kuongeza mavuno na kuboresha udongo bila gharama kubwa?Kilimomisitu ni n...
23/04/2026

FAIDA ZA KILIMOMISITU 🌳🌾

Je, unajua kuwa unaweza kuongeza mavuno na kuboresha udongo bila gharama kubwa?

Kilimomisitu ni njia rahisi inayochanganya miti na mazao k**a mahindi na maharage pamoja na mifugo—na kinaleta matokeo makubwa kwa wakulima.

Faida zake ni pamoja na:
🌾 Huongeza afya na uzalishaji wa mazao
🌳 Huboresha rutuba ya udongo na kuhifadhi unyevu
🌱 Hupunguza athari za ukame na mabadiliko ya tabianchi
🌍 Hulinda mazingira na kuongeza bioanuwai
💰 Hutoa vyanzo vya ziada vya kipato (matunda, mbao, n.k.)

Kwa wakulima wa maeneo k**a Muriaza, Butiama ambapo mradi wa ASILIB-CC unatekelezwa, mabadiliko tayari yanaonekana—mazao bora na udongo wenye afya.

Kilimomisitu ni suluhisho rahisi, la gharama nafuu, na lenye manufaa ya muda mrefu kwa mkulima na mazingira.

Katika jitihada za kuimarisha uhifadhi wa mazingira na kukuza maisha endelevu, kupitia program ya   jumla ya miti 2,500 ...
14/04/2026

Katika jitihada za kuimarisha uhifadhi wa mazingira na kukuza maisha endelevu, kupitia program ya jumla ya miti 2,500 imegawiwa katika Kata ya Bwiregi, ambapo vijiji vya Kamgendi na Masurura vimenufaika na zoezi hili.

Aina za miche iliyogawiwa ni pamoja na:
🌲 Misindano – 1,440
🌿 Misideri – 400
🌳 Misanduku – 200
🍐 Mipera – 100
🍊 Michungwa – 160

Mgawanyo huu unalenga kuchochea upandaji wa miti kwa ajili ya:
✔️ Uhifadhi wa mazingira
✔️ Kuongeza kipato kwa jamii kupitia matunda
✔️ Kuboresha afya ya ardhi na hali ya hewa

Tunatoa wito kwa wanajamii kuhakikisha miche hii inapandwa na kutunzwa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

🌍 Tupande miti leo kwa kesho bora!

Address

Kunzugu Ward
Bunda
P.O.BOX95

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Telephone

+255787926671

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BUFADESO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to BUFADESO:

Share