SANJA LUPO

SANJA LUPO Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from SANJA LUPO, Environmental conservation organisation, MWANZA, Bariadi.

MARAFIKI HATARIMarafiki zako wanazo sifa hizi?Kuna aina za marafiki ambao tunawaita marafiki hatari kwenye maisha yako, ...
01/01/2026

MARAFIKI HATARI

Marafiki zako wanazo sifa hizi?

Kuna aina za marafiki ambao tunawaita marafiki hatari kwenye maisha yako, wanaweza kuwa ni marafiki ambao upo nao karibu, umetoka nao mbali, mnaishi pamoja, kwa bahati mbaya wakawa ni marafiki ambao hawana mchango wowote kwenye maisha yako na wanaweza kuwa na madhara baadae.

Inashauriwa, ni muhimu sana kwa kila rafiki ulienae umpitishe kwenye vipimo maalum ambavyo vitakusaidia k**a huyo rafiki unaweza kuendelea kumuamini au uendelee kuwa nae bila kumtegemea sana.

1. Hawawezi kukutaja kwenye fursa, ni rafiki kweli, anazo fursa fursa nyingi lakini hawezi kukutaja licha ya kufahamu Uwezo na Uzoefu wako. Ukweli ni kwamba yupo tayari kuwa-recommend/Kuwataja/Kuwasemea wengi lakini sio wewe, anahisi akikutaja atakuwa amekupendelea sana, wapo na wewe tu kutokana na kwamba kuna kitu wanapata kwako ila kiukweli hawafurahii kukua kwako.

2. Hawaamini katika Ndoto Zako, ukiwashirikisha kuhusu ndoto zako/malengo yako, hawaamini kabisa, wanaku-doubt sana, hawakupi sapoti yoyote, kila siku wanakukosoa, wanakukatisha tamaa, hawaamini ndoto zako.

3. Hawapatikani kwenye changamoto zako, ukiwa na changamoto hawapatikani, una kesi polisi/umefukuzwa kazi/Huna hela n.k, Yaani ukiwa na changamoto hawapatikani kabisa, wapo bize. Hawapo tayari kukusaidia, hawapo tayari kuambatana na wewe ukipitia changamoto fulani. Watakuwa na wewe tu ukiwa unang'ara na watakukana ukiwa kwenye changamoto.

4. Wanaamini ni lazima wakuzidi, wanataka wakuzidi katika kila kitu, Hela/Umaarufu/Akili/Kimawazo n.k, ukianza kuwazidi tu basi ni tatizo. Wanaamini kuwa siku zite lazima uwe chini yao, ukianza kuwazidi tu wanachukia, wazo lao wanaamini lazima lishinde, wanaamini hutakiwi kuwa mtu mkuu au mtu mkubwa zaidi yao.

Asanteni kwa kuendelea kuwa pamoja na sisi katika programmes zetu.

Subscribe: https://www.youtube.com/channel/UC38VdUM5jqXy2d7gDQSXyYg

Muda wowote ukiwa tayari kujifunza kwa kina kutoka kwangu Bofya hapa
>>>

Entertainments and Educational programmes

01/01/2026

MADHARA YA KUNYWA SOFT DRINKS ( SODA JUICE NA KADHARIKA)

Kunywa soft drinks mara kwa mara kunaweza kuwa na madhara kwa afya kwa sababu hizi kuu:

(Kwa kifupi, soft drinks ni vinywaji vyenye: Gesi (carbonation), Sukari nyingi au sweeteners, na caffeine hapa tunaongelea soda zote na baadhi ya juisi)

1. Sukari nyingi sana
Soft drinks nyingi zina sukari nyingi, ambayo:
Huongeza hatari ya unene
Huongeza uwezekano wa kisukari (diabetes type 2)
Husababisha kuchoka haraka baada ya muda mfupi
I
2. Huharibu meno 🦷
Sukari + asidi kwenye soft drinks:
Huoza meno na Hupunguza uimara wa enamel ya meno

3. Huathiri mifupa🦴
Baadhi ya soft drinks (hasa coca cola):
Hupunguza kiwango cha calcium
Huongeza hatari ya mifupa kuwa dhaifu (osteoporosis)

4. Hakuna virutubisho muhimu
Soft drinks: Hazina vitamini, madini, wala protini Ni “kalori tupu” — zinaongeza uzito bila kujenga mwili

5. Huongeza hatari ya matatizo ya moyo ❤️
Kunywa mara kwa mara Huongeza shinikizo la damu na hatari ya magonjwa ya moyo

6. Husababisha utegemezi (addiction)
Mchanganyiko wa sukari na caffeine hufanya mtu atamani kunywa tena na tena
Kuacha ghafla kunaweza kusababisha maumivu ya kichwa au uchovu
Nini mbadala bora?

Maji 💧
Maji ya matunda asilia (bila sukari)
Maziwa
Chai bila sukari

UTAJUAJE KINYWAJI UNACHOKUNYWA NI SOFT DRINK UKIACHANA NA SODA👍
➡️Hivi ndivyo jinsi ya kusoma lebo ya kinywaji ili ujue k**a ni soft drink au la:
1️⃣ Angalia Sukari (Sugar)
Ikiandikwa Sugar, Sucrose, Glucose, Fructose, Corn syrup
Zaidi ya 5g kwa 100ml → hiyo ni soft drink Ina maanisha kwamba Chupa moja inaweza kuwa na vijiko 6–10 vya sukari 😬
2️⃣ Angalia Kalori (Calories)
Kalori nyingi lakini hakuna virutubisho → soft drink Mfano ukikuta imeandikwa : 120–150 kcal bila protini au vitamini
3️⃣ Angalia Asidi
Maneno k**a: Citric acid na Phosphoric acid hii 👉 Huonyesha ni kinywaji chenye asidi (soft drink)
4️⃣ Angalia Caffeine
Ikiwa ipo mara nyingi ni soft drink
5️⃣ Angalia Carbonated
Ikiandikwa Carbonated / Fizzy / Spa

BABA 😭Baba, mwanaume pekee anayekupenda kwa moyo wake wote ni Baba, mengi magumu moyoni kwa Baba ni ngumu kusema, leo ma...
01/01/2026

BABA 😭

Baba, mwanaume pekee anayekupenda kwa moyo wake wote ni Baba, mengi magumu moyoni kwa Baba ni ngumu kusema, leo makosa ya Baba ni rahisi kuwa maarufu kwani wazee wameamua kukaa kimya tu.

Ni kweli Mama ni muhimu, na nafasi yake ni kubwa sana, na mdomo wake unambeba, Baba wanakufa mapema kutokana na kubeba vitu vingi moyoni.

Inashangaza, kadri muda unavyokwenda, upweke kwa Baba unazidi, watoto wanazidi kujenga urafiki na Mama, sheria zipo upande wa Mama kuliko Baba, Dunia haiwapendi akina Baba.

Tazama, vifo vingi vya ghafla ni vya Baba, nyumba nyingi zina wajane, Baba amefariki, Mama anadunda.

Kimsingi, watu wengi wana bibi zao kuliko babu zao.

Baba, Dunia haitupendi, ni rahisi watu na mashirika kusimama pamoja kumtetea Mama lakini sio Baba. Mashirika yameundwa kumpa nguvu Mama, na hata kufikia kuchukua hata haki za Baba.

Baba, tupo njia panda, k**a vifaranga, muda wowote tunachukuliwa na mwewe. Jambo baya likimtokea Baba, ni haki yake ya msingi, tazama Dunia imekuwa dhidi ya Baba, Dunia haicheki na Baba.

Nani k**a mama, waachieni waimbe nani k**a Mama, kwani hakuna wa kuvaa viatu vya Baba.

Maisha mkononi, roho rehani, kuyapa maisha ahueni. Mshua hakutoka kwenye familia tajiri, na bado alihakikisha hatulali njaa na kutupeleka shule, tulitibiwa kila tukipata homa.

Baba, kuna wakati unakaa kimya, sio kwamba huna cha kuongea bali huna uhakika k**a dunia itakuelewa. Tumechagua kucheka wakati wa shida kuonyesha kila kitu kipo sawa. Tunyime kila kitu na tutese kadri uwezavyo, bado tutakuonyesha kuwa sisi ni wanaume.

Kimbiza kwani nakuaminia Baba, hatujaja duniani kulalamika, wanaokuamini acha wabaki, wasiokuamini acha waende.

Kesho tena, tutakuwa na nguvu kuliko jana Baba.

Tusikitike kidogo, nimeshindwa kuendelea kuandika moyo unaumia Baba! 😭😭

Tuwakumbuke Baba zetu.

Entertainments and Educational programmes

07/09/2025

JE IPI NI THAMANI YA YOUNG AFRICANS, NI BILLION MIA AMA CHINI?

Baada ya kuchapisha andiko kuhusu THAMANI ya Young Africans nikapokea simu kutoka kwa Mwalimu wangu ambaye kwasasa ni Mwalimu wa Uchumi kwenye Chuo Kikuu moja wapo nchini, alianza kwanza na swali lake kwangu.

Farhan una Followers Million Moja unaweza kupost tangazo kwa Laki ila mwingine ana Followers laki tano na akapost tangazo kwa Million, unaelewa maana yake? Sikumuelewa ila jibu lake ni kuwa kila kitu ni STANDARDS unazojiwekea.

Mwalimu wangu akaniuliza tena swali, Manchester United haifanyi vizuri kwenye mpira ila bado ni biashara kubwa na ya moto kwenye soko la hisa, unaelewa maana yake? Hapa tena nikakosa majibu ndipo akaanza darasa lake.

Cha kwanza kabisa Klabu yoyote ina namna nyingi za kujipa thamani yake, kwa kesi k**a Manchester United atakutazamia thamani ya mikataba yake kibiashara, idadi ya Wanachama wake na purchasing power, huyu lazima awe na nguvu kubwa kwenye soko.

Kwa suala la Young Africans, Mwalimu akaanza kutoa darasa lake rasmi k**a Yanga ana Wanachama 91,000 duniani kote chukua wote kwa thamani ni 2.8 Billion kwa mwaka hapo ni Wanachama pekee bila Mashabiki na bila kugusa purchasing power yao, ni mtaji huu kwa Klabu.

Mwalimu akaniuliza kuhusu bajeti ya Yanga msimu huu ni Billion 33 hapo akauliza k**a operation costs ndani ya miaka mitatu unafikia thamani ya Klabu iweje uone Billion 100 ni kubwa? Ambayo hiyo ni asking price?

Mwalimu akaendelea kwamba pale Jangwani ni eneo la Yanga, tukisema tulipeleke sokoni kuuza pale patauzwa bei gani? Maana yake thamani ya Jangwani nayo ina maelekezo yake kwenye Billion 100 maana ni Asset ya Yanga.

Mwalimu ak**aliza kwa kuniuliza, endapo Yanga angemuuza Mzize wangepata Billion 5 je Billion tano inaingia kwenye account za Yanga si ndio? Maana yake chukua thamani ya vikosi vyote vya Yanga pia unapaswa kujumlishia kwenye thamani ya Billion 100, unaona haifiki? Aliniuliza Mwalimu.

Mwalimu akauliza kuhusu commercial rights za Yanga kwa

04/09/2025

Mtu aliemuua Rais wa zamani wa Burkina Faso Thomas Sankara ni rafiki yake wa utotoni, jina lake ni Blaise Compaoré, Thomas Sankara na Blaise Compaoré walikua pamoja tangu watoto na waliishi pamoja.

Blaise Compaoré alilelewa na Baba yake Thomas Sankara na waliishi pamoja k**a ndugu, baadae walijiunga na jeshi la Burkina Faso pamoja, pindi Thomas Sankara alipofanikiwa kuwa Rais wa Burkina Faso alimchagua rafiki yake huyo wa utotoni Blaise Compaoré kuwa makamu wake wa Rais.

Siku 5 kabla ya Blaise Compaoré hajafanikisha mauaji ya Thomas Sankara walikua na sherehe yao walikunywa pamoja na kucheza pamoja kusherehekea event hiyo, baada ya muda mfupi Thomas Sankara alipewa taarifa ya siri na watu wake wa usalama kuwa Blaise Compaoré amepanga kumuua.

Thomas Sankara aliipokea taarifa hiyo lakini hakuiamini sana, vipi rafiki yake, k**a ndugu yake waliokua pamoja tangu utotoni waliofanyiana mengi leo hii amuue? Hakuamini k**a kuna uwezekano wa kufanyiwa hivyo na Blaise Compaoré.

Lakini ni lipi linaloshindikana kwenye dunia iliyojaa usaliti? Hatimae October 15, 1987 Thomas Sankara akauwawa kwenye mapinduzi yalioyoongozwa na rafiki yake wa utotoni, mtu walielelewa nae pamoja, mtu aliempenda na akamchukulia k**a ndugu yake.

Sankara alipigwa risasi 11 kifuani na risasi 4 kichwani na vijana walioongozwa na Blaise Compaoré, na hatimae Blaise Compaoré yeye ndo akawa Rais wa Burkina Faso na kuiongoza nchi kwa miaka 27 baaada ya kufanya usaliti huo kwa ndugu yake.

Hivyo ndivyo dunia ilivyojaa usaliti unaemuamini sana ndiye anaeweza kukuangamiza.
Kwa sasa Blaise Compaoré anaishi Ivory Coast na bado hajalipia gharama ya usaliti.
Rest In Peace Thomas Sankara.

04/09/2025

China inaweza kukupa utajiri sana, lakini pia unaweza kupoteza mtaji wako wote.
Sasa kabla hujaenda china, hakikisha unayajua haya mapema ili safari yako iwe ya mafanikio makubwa.
1. Pata passport yako Mapema, Ni vizuri pia k**a Mfanyabiasha mwenye malengo makubwa kuwa na passport.

2. Fatilia Visa yako. Ubalozi wa china uko Masaki. Pata visa yako mapema ili ukate tiketi mapema upate kwa bei nzuri.

3. Pata tiketi yako mapema ya ndege. Mashirika ya ndege ni mengi na kila shirika lina uzuri wake uharaka, mizigo, chakula na huduma. Nauli ya kwenda China na kurudi ni kati Tsh 3M ( bei hubadilika kulingana na season na muda uliokata na shirika)

4. Usiende china hujui utanunua nini, Usiende china kwa lengo la kuagizisha bidhaa kwa oda hasa k**a ni mara ya kwanza. K**a una mtaji mkubwa Fahamu ni mji gani bidhaa zako utapata na utafikaje kwenye huo mji kutoka Ghuanzou

5. Download app ya Wechat, Hii ni k**a whatsapp kwa china, Itakusaidia kukusanya mawasiliano ya supplies lakini pia kuwasiliana na translation

6. Pata laini ya China ukifika. Itakusaidia kwenye mambo mengi.

7. Kabla hujaanza safari ni muhimu kutambua ni nani ambaye atakupokea, na utafikia hoteli gani.

8. Download VPN kabla ya kwenda China kwani huko hutoweza kutumia Google, Whatsapp, instagram, tiktok nk bila VPN hata ukiwa kwenye Wi-Fi ( naweza kukupatia pia laini za china au Dubai kabla hujaenda ili ukifika uwasiliane na wenyeji wako na utumie mitandao yote bila VPN usije ishia Airports, Tunazo dukani)

9. Download app ya DiDi ( ndio Uber /bolt za china) itaokoa gharama zako kuliko kutumia Tax za kawaida

10. Tafuta mtu akufundishe kutumia metro🚇( ni Tren za haraka za ardhini k**a daladala) ni Rahisi na nafuu mno

11. Kwa ushauri, k**a una mtaji wa chini ya 15M na hutaki kuupoteza usiende china kwanza, kwa competition ya sasa ni ngumu bidhaa za 10M kukupa 20M ambayo itarudisha gharama zako, mtaji na faida. Ila China ni sehemu nzuri kwenda kujifunza Biashara hivyo k**a lengo ni kujifunza na kup

03/09/2025

Mkumbusheni Diamond platnam na ommiy dimpoz .
👇
Ndege anapokua hai hupenda saana kula wadudu.lakini anapokufa wadudu humla yeye...usijione Bora kwa sababu uko juu Leo.maisha hujibu kiburi kwa kimya.kua mnyenyekevu kila kitu hubadilika.. usimudharau usie mjua huwenda kile unachokitafuta kipo kwa yule unaemdharau.usione unacho unadharau wengine kwa sababu hawana.ishi na watu vizuri ndugu .dunia mapito....tunajua maisha ni yenu nyie diamond platnam na wenzako ila mazishi ni yetu nyie washamba mnaoita watanzania wenzenu kuma mamae zenu.......kisa tu mmeshiba pesa za Kodi zetu ambazo zinachezewa na wapuuzi wachache......mnahimiza watanzania wafanye kazi kwa watanzania wanakula kwenu .au bando mnawawekea nyie......tupo nyakati za mwisho wenzetu burki nafaso wanapambana kupunguza mashoga Tanzania 🇹🇿 ndo kwanza mashoga wanazidi kuongezeka....in short ni kwamba ukiona mwanaume ana akili zake timamu anatoboa pua .anasuka .na kujipodoa basi ujue nyuma k**a mwanamke tu..........mmezingua saana nawa unfollow wote .....mnajua watanzania maumivu wanayopitia......tusihimizane kufanya kazi wengine pesa za kuchezewa matakoni hatuhitaji ......
👇
pichani k**a mtu k mwenyewe

30/08/2025

ANGUKO KUBWA LA BIASHARA LINATOKANA NA HAYA MAENEO MAKUBWA 7.

Wafanyabiashara wengi huanguka sio kwa sababu hakuna wateja, ila kwa sababu ya makosa ya msingi ambayo hayafanyiwi marekebisho mapema.

Kitaalamu na kwa uhalisia wa Tanzania, anguko kubwa la wafanyabiashara liko kwenye maeneo haya makuu:

1. Kutokujua Hesabu na Mzunguko wa Fedha (Financial Mismanagement)
• Wengi huona pesa ya biashara ni pesa yao binafsi.
• Hawajui tofauti kati ya faida, mtaji na mapato.
• Matokeo yake: biashara inakuwa na mauzo lakini haikui.
• Mfano: Mfanyabiashara anaingiza milioni 5 kwa mwezi, lakini kila mara akitaka kuongeza stock anatoka mfukoni binafsi – hii inaua ukuaji

2. Kutegemea Mawazo, Siyo Data (Lack of Market Research)
• Wengi hufungua biashara kwa kuiga “kwa sababu fulani kafungua” badala ya kufanya research.

• Utafiti wa Harvard Business Review unaonyesha 42% ya biashara duniani hufa kwa sababu bidhaa hazihitajiwi sokoni.

• Kwa Tanzania: watu wanafungua saloons, stationary au butchery kwa kuiga, bila kujua demand halisi ya eneo. Kisa umeona Fetty anauza sana sokoni na yeye anaiga

3. Kukosa Mfumo (Lack of Systems & Processes)
• Biashara inategemea mtu mmoja pekee.
• Mmiliki akiumwa, akisafiri, au akipotea kidogo, biashara nayo inasambaratika.
• Mfumo = accounting, stock control, sales tracking, marketing system.
Mfano wa mfumo ni k**a huu wa THL wanaotumia wengi una features zote na za point no 1. Link yake uitumie www.thlaccounting.com
• Mfano: maduka mengi ya Mangi hubaki duka la mtu binafsi kwa miaka 10 na bila kukua.

4. Kutumia Mtaji Vibaya (Misallocation of Capital)
• Badala ya pesa kuzunguka kwenye biashara, inatumika kwenye vitu vya kibinafsi: magari ya kifahari, sherehe, nguo.
• Hili ndio inaitwa “kula mtaji”.
• Wengi wanakufa kibiashara kwa sababu unakuta biashara haijakomaa lakini mmiliki anaishi maisha ya kifahari ya kufake nje ya duka kapaki RANGE ya na plate number ya jina lake wakati faida kwa mwezi ni 2M tu.

5. Kutokujua Kujitofautisha

tHL Accounting - Accurately and Securely: Track stocks, sales, expenses and profits Manage your Business from Wherever you are! No Headache. Get Everything you need confidently to run your business.

15/08/2025

Nilianza kuwa na adabu Ile siku niliyoona engine ya Benz ikiwa imebebwa kwenye mkokoteni inaenda kuuzwa k**a skrepa.

Niliogopa pale msiba wa yule tajiri kaburi lake kuchimbwa na wale vijana wanaoitwa wezi na masela wa mtaani.

Nilipata mashaka pale dereva mzuri mwenye mbwembwe alipokufa kwa ajali kwenye Kona aliyoizoea.

Nilijifunza pale binti mdogo alipoolewa na mzee ili arithi mali, ajabu akatangulia kufa yeye..

Niliogopa pale hakimu aliyedhurumu haki za watu, na yeye alipata kesi isiyo na dhamana..

Maisha yakikupa ukubwa, chagua kuwa mnyenyekevu🙏

08/08/2025

NCHI IMEKAMATWA NA MAGENGE YA KISIASA – TUNAKWENDA WAPI?

Kauli ya Humphrey Polepole haikuwa ya kawaida. Ilikuwa ni bomu la kisiasa lililoteguliwa katikati ya giza la mfumo wa kifisadi, lililofichika nyuma ya sura za viongozi wetu. Kwa mujibu wake, Tanzania imeingizwa rasmi kwenye kipindi cha utawala wa magenge – kundi la “wanamtandao” ambalo limejipenyeza serikalini na kwenye chama tawala na sasa linaendesha nchi kwa misingi ya hila, chuki, tamaa na kulindana kwa kutumia hofu na udanganyifu.

Mpina kutajwa kuwa ni sehemu ya mradi wa wanamtandao haipaswi kuonekana k**a jambo dogo. Ni onyo. Ni ushahidi kwamba kinachoitwa ushindani wa kisiasa ndani ya CCM si tena ushindani wa hoja, bali ni vita ya makundi yanayopigania maslahi binafsi kwa gharama ya damu ya Watanzania. Kwa mujibu wa Polepole, wanamtandao hawa hawasiti kutumia mbinu chafu: kutoka kwenye fitina, utekaji, hadi kuondoa wapinzani wao kwa risasi au sumu. Kauli ya Polepole kuhusu uhalisia wa Lisu kupigwa risasi inaiondoa kabisa hoja kuwa ilikuwa "tukio la bahati mbaya" au "jambo la mtu binafsi." Hili lilikuwa shambulio la dola – lililobarikiwa na mtandao ulio ndani ya dola hiyo hiyo.

CCM IMEGAWANYIKA: HAKUNA TENA UMOJA WALA MSHIKAMANO

Leo hii ni wazi kabisa: ndani ya CCM hakuna tena mshik**ano wa kweli. Wanachama wake wakuu wanawindana k**a wanyama pori jangwani. Wengine wanatolewa kafara kwa hofu kwamba watazuia mipango ya mrithi wa urais. Kesi ya Ndugai ni mfano hai. Alichinjwa kisiasa ili kulainisha njia ya urithi. Mkapa, Magufuli, Majaliwa, Mpango – ama wameondolewa, wamewekwa pembeni, au wamezimwa kimya kimya. Nani anayefuata?

Huku nyuma, Mama alipewa nguvu na uhalali wa kisiasa kutoka kwa kundi hilo la wanamtandao. Leo, ni mateka wao. Ndio maana baadhi yao wamepachikwa kwenye nafasi za juu za utumishi wa umma, kwenye bodi, kwenye Tume, hadi kwenye taasisi za usalama. Hii ni “dili” ya kuhakikisha mfumo wao unaendelea hata baada ya 2025. Lakini je, hiyo ni dhamira ya wananchi?

UCHAGUZI 2025: HARAMIA

08/08/2025

WAFUNDISHE WANAO UKWELI HUU KUHUSU NGONO – UTAKUZA KIZAZI BORA SANA!

Mwanao ni hazina ya thamani kuliko vitu vyote ulivyonavyo katika huu ulimwengu wa kimwili. Ukimlea kwa maarifa, atakuletea baraka maishani. Lakini ukimlea kwa uoga, kwa kumficha ukweli, na kwa kutoonyesha dira, atakuletea mzigo mzito mbele ya safari.

Leo kuna familia nyingi zinazojutia uamuzi wa kupata watoto. Unakuta mzazi analia ndani kwa ndani, kwa sababu:

👉Mtoto mkubwa ni mlevi sugu.

👉Wa pili ni mbakaji au jambazi.

👉Binti hana dira ya maisha zaidi ya kusaka “sponsors” kwa ajili ya starehe na miamala ya mwili.

👉Yule mdogo anasifika shuleni kwa “utoaji huduma” badala ya uhodari wa kielimu.

Haya yote siyo laana. Mara nyingi ni matokeo ya malezi yasiyo na maarifa ya kweli, hasa kuhusu jambo la msingi k**a uhusiano kati ya ngono na nguvu za kiakili, kimwili na hata kiroho!

Muweke wazi mwanao kuwa Katika mafundisho ya Gnosticism – hususan elimu ya ngono ya kiroho – ukweli wa kina kuhusu ngono ulifichwa kwa karne nyingi. Si elimu ya kawaida; ni elimu ya ndani (esoteric knowledge). Inahitaji mtu kufunguka, kuwa tayari kupokea na kuishi kwa mwanga mpya wa maisha.

Na kwa wanao, huna budi kuwa muwazi. Usikimbie mazungumzo kuhusu ngono. Usikwepe kuyazungumzia kwa sababu ya aibu. Ukweli huu ukiwafikia mapema, utaunda kizazi chenye akili, roho imara na miili yenye mwelekeo.

Waeleweshe kwa logic nyepesi kabisa kuwa Mbegu ya mwanaume + Yai la mwanamke = HUUNDA MTOTO (nafsi mpya kabisa). huu si mchezo, ama burudani– ni nishati ya kiwango cha juu kabisa katika ulimwengu huu wa metafizikia.

Hii si kazi ya kimwili tu, ni tendo la kuumba maisha mapya. Manii ya mwanaume si maji tu; ni nishati kuu ya maisha. Ikitumika vyema huleta baraka, ikitumika hovyo huleta laana na matatizo.

Mwambie ukweli kuwa kutoa manii ama maji matakatifu ya k**e ni kutoa nguvu yako ya kipekee.
Usimfiche kabisa, mwambie Ngono inayofanywa kwa tamaa na kutokuwa na mwelekeo wa kiroho:

✅Hupoteza nishati ya roho

✅Huchosha m

Address

MWANZA
Bariadi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SANJA LUPO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share