01/01/2026
MARAFIKI HATARI
Marafiki zako wanazo sifa hizi?
Kuna aina za marafiki ambao tunawaita marafiki hatari kwenye maisha yako, wanaweza kuwa ni marafiki ambao upo nao karibu, umetoka nao mbali, mnaishi pamoja, kwa bahati mbaya wakawa ni marafiki ambao hawana mchango wowote kwenye maisha yako na wanaweza kuwa na madhara baadae.
Inashauriwa, ni muhimu sana kwa kila rafiki ulienae umpitishe kwenye vipimo maalum ambavyo vitakusaidia k**a huyo rafiki unaweza kuendelea kumuamini au uendelee kuwa nae bila kumtegemea sana.
1. Hawawezi kukutaja kwenye fursa, ni rafiki kweli, anazo fursa fursa nyingi lakini hawezi kukutaja licha ya kufahamu Uwezo na Uzoefu wako. Ukweli ni kwamba yupo tayari kuwa-recommend/Kuwataja/Kuwasemea wengi lakini sio wewe, anahisi akikutaja atakuwa amekupendelea sana, wapo na wewe tu kutokana na kwamba kuna kitu wanapata kwako ila kiukweli hawafurahii kukua kwako.
2. Hawaamini katika Ndoto Zako, ukiwashirikisha kuhusu ndoto zako/malengo yako, hawaamini kabisa, wanaku-doubt sana, hawakupi sapoti yoyote, kila siku wanakukosoa, wanakukatisha tamaa, hawaamini ndoto zako.
3. Hawapatikani kwenye changamoto zako, ukiwa na changamoto hawapatikani, una kesi polisi/umefukuzwa kazi/Huna hela n.k, Yaani ukiwa na changamoto hawapatikani kabisa, wapo bize. Hawapo tayari kukusaidia, hawapo tayari kuambatana na wewe ukipitia changamoto fulani. Watakuwa na wewe tu ukiwa unang'ara na watakukana ukiwa kwenye changamoto.
4. Wanaamini ni lazima wakuzidi, wanataka wakuzidi katika kila kitu, Hela/Umaarufu/Akili/Kimawazo n.k, ukianza kuwazidi tu basi ni tatizo. Wanaamini kuwa siku zite lazima uwe chini yao, ukianza kuwazidi tu wanachukia, wazo lao wanaamini lazima lishinde, wanaamini hutakiwi kuwa mtu mkuu au mtu mkubwa zaidi yao.
Asanteni kwa kuendelea kuwa pamoja na sisi katika programmes zetu.
Subscribe: https://www.youtube.com/channel/UC38VdUM5jqXy2d7gDQSXyYg
Muda wowote ukiwa tayari kujifunza kwa kina kutoka kwangu Bofya hapa
>>>
Entertainments and Educational programmes