Mviwama

Mviwama Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mviwama, Community Organization, Stendi ya Mahakama, Barabara ya Dodoma, Babati.

MVIWAMA - Mtandao wa Vikundi vya Wakulima na Wafugaji wa Mkoa wa Manyara (Regional Network of Farmers' Groups in Manyara)
Ni Jumuiya wa Wanachama inayolenga kutetea maslahi ya wakulima (wazalishaji wa mazao ya mimea, mifugo na samaki) wadogo.

Katika shamba hili la kitafiti tunaonesha jinsi mbinu ya Makingamaji ya Nusu Mwezi inaweza kutumika kuhifadhi maji na ku...
04/05/2026

Katika shamba hili la kitafiti tunaonesha jinsi mbinu ya Makingamaji ya Nusu Mwezi inaweza kutumika kuhifadhi maji na kupandwa nyasi za malisho ya mifugo

Katika eneo hili tumeunganisha mbinu mbili ya NUSU MWEZI na KISIKI HAI kurejesha uoto wa asili na kukuza malisho

Pongezi kwa maafisa ugani wetu ambao wanafanya juhudi za kurithisha mbinu hizi kwa wanachama wetu

Utekelezaji huu umefanyika Simanjiro kupitia mradi wa REDAA unaofadhiliwa na
📍Simanjiro

📸 mviwama ||


Joseph na mke wake—wanandoa vijana walioamua kubadilisha mwelekeoKupitia mradi wa Forest and Farm Facility, walipata fur...
27/04/2026

Joseph na mke wake—wanandoa vijana walioamua kubadilisha mwelekeo

Kupitia mradi wa Forest and Farm Facility, walipata fursa ya kujifunza na kuwezeshwa kutumia nishati mbadala, biogas.

Wanajishughulisha na ufugaji wa nguruwe na ng’ombe, pamoja na kilimo na sasa mabaki ya mifugo yao yanazalisha nishati ya kupikia.

Hakuna tena utegemezi wa kuni wala gharama za nishati.

"Tulikuwa tunatumia muda mwingi kutafuta kuni. Sasa tunatumia muda huo kuboresha maisha yetu."

Forest and Farm Facility ni mradi unaotoa fursa sahihi kwa Vijana na kuleta mabadiliko.
Umefadhiliwa na FAO

Wewe unafuga aina ipi kwa sasa au una mpango wa kubadilisha?Sio kila mbuzi anakupa matokeo unayotakaTofauti halisi iko k...
22/04/2026

Wewe unafuga aina ipi kwa sasa au una mpango wa kubadilisha?

Sio kila mbuzi anakupa matokeo unayotaka

Tofauti halisi iko kwenye aina unayochagua

Kwa wafugaji wetu wanaotaka kufikia uhuru wa kifedha kupitia ufugaji, anza na mifugo yenye tija, inayokua haraka, na inayorudisha faida toshelevu.

Tumia taarifa sahihi, si mazoea
Kwa ufadhili wa Mradi wa REDAA

#

Unaweza kuwa na visiki hai shambani bila kuathiri mazao yako—na bado ukapata faida zote 🌱. Chagua miti yenye kivuli cha ...
20/04/2026

Unaweza kuwa na visiki hai shambani bila kuathiri mazao yako—na bado ukapata faida zote 🌱. Chagua miti yenye kivuli cha wastani 🌳, ipunguze mara kwa mara ✂️, na isambaze vizuri shambani ili kuepuka msongamano.

Kwa kufanya hivyo, unaboreshа rutuba ya udongo kupitia majani yanayooza 🍂 na kuhifadhi unyevu ardhini kwa msaada wa mizizi yake 💧.

Fanya kwa faida ya shamba lako🌍🌿
Kwa ufadhili wa na .tz - Kupitia mradi wa HUSISHA
📸| MVIWAMA

💚 Tunarithisha elimu ya utunzaji wa mazingira kupitia mbinu ya KISIKI HAI, 🌱tukilenga taasisi zenye watu wengi ili kila ...
17/04/2026

💚 Tunarithisha elimu ya utunzaji wa mazingira kupitia mbinu ya KISIKI HAI, 🌱tukilenga taasisi zenye watu wengi ili kila mmoja apate uelewa na kushiriki kwa vitendo. Tunapoanza na mtu mmoja, ☺️ tunabadilisha jamii nzima. Jamii inapobadilika, vitendo vinakuwa sahihi na mazingira yanarejea kuwa hai, yenye afya, na endelevu. 💚🌱🌲

Tunawezeshwa kupitia mradi wa HUSISHA unaofadhiliwa na @ na .tz (pamoja katika utekelezaji)
Kuwa sehemu ya kuleta mabadiliko halisi

📸| Mviwama

Hiki tunachokiita KISIKI HAI kinatusaidia kurejesha miti ya asili ambayo tayari ipo ardhini. Badala ya kupanda tu, tunal...
15/04/2026

Hiki tunachokiita KISIKI HAI kinatusaidia kurejesha miti ya asili ambayo tayari ipo ardhini. Badala ya kupanda tu, tunalinda mashina yaliyopo ili yaote tena na kukua kuwa miti mikubwa. Kupitia mbinu hii, tunahusika moja kwa moja katika kurejesha mifumo ya ikolojia ya mazingira yetu.
Kupitia mradi wa HUSISHA .tz

📸|

Unatumia mbinu gani kupata mavuno Mengi? 🌽Kila mkulima ana nafasi ya kupata mavuno mengi kwa kutumia mbinu sahihi.Njia m...
13/04/2026

Unatumia mbinu gani kupata mavuno Mengi? 🌽

Kila mkulima ana nafasi ya kupata mavuno mengi kwa kutumia mbinu sahihi.

Njia mojawapo ni kutumia mbinu makinga maji ya FANYA JUU FANYA CHINI ambayo si tu kwamba hutunza maji ya mvua na kuzuia mmomonyoko wa shamba bali pia husambaza unyevu wa kutosha ardhini kusaidia mazao kustawi. 🌱🌧

Utatumia gharama ndogo kuchimba na mavuno ni uhakika 💚🌽
Kwa ufadhili wa .tz kupitia mradi wa HUSISHA
📸 |

.

  siku IV | KILIMO IKOLOJIA - Kinavutia, na Kinawezekana Eneo lolote 🌱Unaona Ardhi hii Isiyozalisha Imekuwa yenye Uhai 🌱...
26/03/2026

siku IV | KILIMO IKOLOJIA - Kinavutia, na Kinawezekana Eneo lolote 🌱

Unaona Ardhi hii Isiyozalisha Imekuwa yenye Uhai 🌱
..ni juhudi za mafunzo ya kivitendo kwa kikundi cha Watafutaji, Mtandao wa msingi Dosidosi
..ambao wanasimamia shamba darasa hili la mahindi la mwanachama Fatuma Abed
..Utofauti mkubwa unaonekana wazi kati ya upande wenye MBOLEA YA SAMADI na ule usio na mbolea
..Mazao yenye mbolea yana AFYA BORA na WINGI, 🌽 huku sehemu bila mbolea ikionyesha ukuaji mdogo 🍂

HII INAVUTIA, INAHAMASISHA NA INAWEZEKANA KWA ENEO LOLOTE 💚
..Tumekupa picha tu ya matokeo ya mradi wa REDAA unaotuwezesha
..kufundisha mbinu za kilimo ikolojia zinazoboresha rutuba ya udongo, kuongeza uzalishaji, na kukuza kipato 🤑
..kwa wanachama wetu 💚

Mradi wa REDAA unafadhiliwa na

Picha na |
Mshauri wa Miradi
Mratibu

Share 🌱 Ifikie Wakulima wengi

  Siku ya III | Maono Yetu ya Ustawi wa Kifedha kwa Wanawake Wafugaji Yanatekelezwaje?..Ni kupitia ufugaji wa mbuzi hawa...
25/03/2026

Siku ya III | Maono Yetu ya Ustawi wa Kifedha kwa Wanawake Wafugaji Yanatekelezwaje?
..Ni kupitia ufugaji wa mbuzi hawa wa Isiolo ambapo wanawake 14 wananufaika
..kutoka kikundi cha Ererai mtandao wa msingi Partimbo, Kiteto

Katika shamba darasa hili mbuzi 13 wamezaliwa (1 pure Isiolo na 12 chotara)
..na tumeona mifugo ikiwa imeongozeka 🐐 🐐

Juhudi hii inainua ustahimilivu wa wanawake katika uchumi na ustawi wa familia zao.

Mshauri wa Miradi kutoka Trias Neema Mollel alizungumza na wanachama hawa kubaini faida na changamoto wanazokabiliana nazo.

Hivi ndivo TUNATIMIZA MAONO YETU ya kuimarisha mifumo
..inayokuza ustawi wa maisha na ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi kwa wanachama wetu.

Kupitia mradi wa REDAA \ C.L.E.A.R

Picha na |
Mshauri wa Miradi @
Mratibu

  Siku II | Ongezeko la Uhusishaji wa Kijinsia kupitia CMGs 💰Wakufunzi wa CMG waliojengewa uwezo na  kupitia mradi wa RE...
24/03/2026

Siku II | Ongezeko la Uhusishaji wa Kijinsia kupitia CMGs 💰

Wakufunzi wa CMG waliojengewa uwezo na kupitia mradi wa REDAA
..wameunda vikundi vipya na kufundisha usimamizi kwa viongozi wa vikundi vya zamani 🧑‍💼
..Katika vikundi 8 vilivyoundwa hadi sasa, ongezeko la mtaji ni asilimia 9.2 wastani kwa kila CMG 📈
..na wanachama wanadumisha mzunguko mzuri wa fedha kupitia hisa zao na kurejesha mikopo.
..Kilichovutia zaidi, wanachama wamebuni miradi ya kukuza mtaji kupitia UNENEPESHAJI WA MIFUGO na KUUZA 🤑
.. na wanagawana faida kwa kuiweka kwenye hisa zao, kuimarisha mzunguko wa fedha. 💰
..hii ni kazi kubwa wakufunzi ToTs wamefanya kivitendo 👍
..Wanawake na Vijana kwa idadi ni wengi (65%++) ikiashiria ongezeko la Uhusishaji
..haya ni matokeo ya aina yake ya mradi huu👉REDAA

Mdau tarajia matokeo makubwa zaidi katika robo zinazofuata za utekelezaji.

Tunafadhiliwa na

📸Picha na |

📍Kiteto

  Siku I | Maeneo ya Urejeshaji wa Mazingira C.L.E.A.R 💚Mshauri wa miradi kutoka Trias East Africa  Neema Mollel, ametem...
23/03/2026

Siku I | Maeneo ya Urejeshaji wa Mazingira C.L.E.A.R 💚

Mshauri wa miradi kutoka Trias East Africa Neema Mollel, ametembelea maeneo tunayotekeleza shughuli za mradi wa REDAA wilayani Simanjiro na Kiteto kwa siku nne.

Tumetembelea mashamba ya kitafiti ya urejeshaji wa mazingira kwa mbinu ya Kisiki Hai yanayohifadhiwa 🌳
..Mashamba ya Makingamaji ya nusu mwezi ambayo nyasi za malisho zimeanza kuota 🐄🌾
..Maeneo ya malisho yaliyong’olewa magugu vamizi na sasa yameota nyasi nzuri 🌱
.. na mashamba darasa ya mbuzi wa Isiolo

Tumeona matokeo chanya ya mvua hizi katika ustawi wa malisho na ukuaji wa miti ya asili 🌧️🌿

Mollel amepongeza wanachama wetu kwa kutoa maeneo kuwa mashamba ya kitafiti kwa suluhisho la malisho ya mifugo 🌱

na Maafisa ugani wetu Evance Mushi, Alamokola Komba kwa juhudi na msaada 🤝

JUHUDI ZETU za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi NI ENDELEVU kupitia mradi wa REDAA

| Picha na |

Address

Stendi Ya Mahakama, Barabara Ya Dodoma
Babati
255

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00

Telephone

0788466966

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mviwama posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Mviwama:

Share