28/11/2025
Leo namleta kwenu kijana mwenzetu mpambanaji na hachoki kutafuta nguvu ya wino wa kalamu sema tu walimu wake walishindwa kumbadilisha Kwenye swala la mwandiko ila yeye ukimuuliza kuhusu mwandiko anakwambia mwandiko sio lolote na Chochote kwake , anakwambia Cha msingi kwake ni kiwango Cha uelewa na kujenga hoja na kupresent uwelewa huo Kwa njia ya speech na sio maandishi
Anyway *hayawi hayawi sasa yamekua* na *Wahenga nao hawaamini macho yao* kijana wetu sasa baada ya darasa letu la 2018 kumpa Jina la *Lawyer* sasa maono ya Class of 2018 yanakwenda kutimia.
Hapa ni baada ya kutunukiwa Degree yake ya kwanza ya sheria na safari ndio kwanza inaanza kuelekea Law school yaani shule ya sheria Kwa vitendo yanayotarajiwa kuanza mwezi January, 2026.
Tumtakie kila lililo jema Kwenye safari yake ya mapambano Kwa masilahi mapana ya Jamii yetu na Tanzania Kwa ujumla
By k***a Mebwanya.