22/03/2026
Ndugu rafiki,
Katika ulimwengu uliojaa changamoto na migawanyiko, kumbuka kwamba kwa Bwana Yesu kuna upatanisho wa kweli. Ndani yake tunapata msamaha, amani ya moyo, na nafasi mpya ya kuanza upya. Pale ambapo kuna maumivu au tofauti, upendo wake huleta uponyaji na kuunganisha tena kilichovunjika.
Tuchague kumkaribia zaidi, kwa maana kwake kuna tumaini jipya na umoja wa kweli. Barikiwa sana mtu wa Mungu