03/09/2026
WADAU KUJADILI NAMNA YA KUIMARISHA MALEZI NCHINI TANZANIA ๐น๐ฟ
Shirika la Compassion International Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo limeandaa Mdahalo wa Wadau kuhusu Kuimarisha Afua za Malezi nchini Tanzania, utakaofanyika tarehe 4 Septemba 2026 Jijini Mwanza, katika Ukumbi wa Ilemela DC.
Mdahalo huo unatarajiwa kuwakutanisha zaidi ya mashirika 20, viongozi wa dini, viongozi wa serikali, vijana, wazazi pamoja na watoto, kwa lengo la kujadili changamoto za malezi, kubadilishana uzoefu na kuweka mikakati ya pamoja ya kuimarisha malezi bora na chanya kwa watoto nchini Tanzania.
Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Bw. Eliakim Chacha Maswi.
Mdahalo huo utaibua maazimio muhimu yatakayotokana na mijadala ya wadau, ambayo yatakusanywa na baadaye kukabidhiwa kwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum katika kilele cha Mbio na Matembezi ya Hisani ya Mtoto ni Malezi Fun Run, tarehe 5 Septemba 2026 Jijini Mwanza.
Pamoja tunaweza kujenga jamii inayotoa malezi bora, salama na chanya kwa kila mtoto.
Mwanza