Compassion International Tanzania

Compassion International Tanzania We currently work with more than 580 churches in 22 regions of Tanzania.

Compassion International Tanzania is one of the largest faith based development organizations in Tanzania committed to releasing children from poverty in Jesus' name.

MATUKIO KATIKA PICHAZIARA YA Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini, Bw. Emmanuel Kihampa katika Kituo cha Maendeleo ya Mto...
03/06/2026

MATUKIO KATIKA PICHA

ZIARA YA Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini, Bw. Emmanuel Kihampa katika Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana kinachosimamiwa na KKKT Monduli Mjini mkoani Arusha kwa ushirikiano na Compassion International Tanzania (CIT).



03/06/2026

SIKU YA PILI YA ZIARA YA MSAJILI WA JUMUIYA ZA KIRAIA ARUSHA

Jana ilikua siku ya pili na ya mwisho ya ziara ya Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini, Bw. Emmanuel Kihampa, katika vituo vya maendeleo ya watoto na vijana vinavyoungwa mkono na Compassion International Tanzania mkoani Arusha.

Katika ziara hiyo, Bw. Kihampa ametembelea Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana kinachosimamiwa na Kanisa la KKKT Monduli, ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazolenga kumkomboa mtoto kutoka katika umasikini na kuwezesha maendeleo endelevu ya watoto, vijana na jamii kwa ujumla.

Ziara hiyo imehudhuriwa na viongozi wa dini, viongozi wa serikali, wafanyakazi wa Compassion International Tanzania, wazazi, watoto, vijana pamoja na wadau wengine wa maendeleo. Aidha, Msajili huyo alitembelea kiwanda kidogo cha utengenezaji wa taulo za k**e, mojawapo ya miradi ya uwezeshaji inayowapa vijana na wanawake ujuzi, fursa za kujiajiri na kuboresha maisha yao.

Ziara hii imelenga kujionea kwa karibu matokeo na mchango wa programu za maendeleo zinazotekelezwa kupitia ushirikiano wa makanisa, jamii na Compassion International Tanzania katika kuboresha ustawi wa watoto na familia zao.



MATUKIO KATIKA PICHAZIARA YA Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini, Bw. Emmanuel Kihampa katika Kituo cha Maendeleo ya Mto...
01/06/2026

MATUKIO KATIKA PICHA

ZIARA YA Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini, Bw. Emmanuel Kihampa katika Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana kinachosimamiwa na Kanisa la Baptist Longido mkoani Arusha kwa ushirikiano na Compassion International Tanzania (CIT).

.district_council

01/06/2026

MSAJILI WA JUMUIYA ZA KIRAIA ATEMBELEA KITUO CHA MAENDELEO YA MTOTO NA KIJANA LONGIDO

Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini, Bw. Emmanuel Kihampa, leo ametembelea Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana kinachosimamiwa na Kanisa la Baptist Longido mkoani Arusha kwa ushirikiano na Compassion International Tanzania (CIT).

Katika ziara hiyo, Bw. Kihampa alipata fursa ya kujionea na kusikiliza shughuli mbalimbali zinazolenga kumkomboa mtoto kutoka katika umasikini, zikiwemo mafunzo ya ujuzi wa mikono, vikundi vya kuweka na kukopa, huduma za afya, elimu, ulinzi wa mtoto na ustawi wa jamii kwa ujumla.

Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Mkurugenzi wa Compassion International Tanzania, Mary Lema, Askofu Mkuu wa Kanisa la Baptist Tanzania, Askofu Arnold Manase, viongozi na wataalamu wa serikali ngazi za kata na wilaya pamoja na wachungaji wa makanisa washirika wa CIT wilayani Longido.

Akizungumza baada ya kutembelea kituo hicho, Bw. Kihampa alilipongeza Shirika la Compassion International Tanzania na makanisa washirika kwa mchango wao katika maendeleo ya watoto na jamii.

“Nimefurahishwa na kazi kubwa inayofanywa hapa. Matokeo yanaonekana wazi kwa watoto, familia na jamii kwa ujumla. Nawapongeza Compassion International Tanzania na makanisa kwa juhudi hizi na ninawahimiza kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. Serikali itaendelea kushirikiana nanyi katika kuhakikisha watoto wetu wanapata fursa bora za kukua na kufikia ndoto zao,” amesema Bw. Kihampa.

Kwa sasa CIT inafanya kazi katika mikoa 22 na wilaya zaidi ya 90 huku zaidi ya watoto na vijana 125,000 wakihudumiwa kupitia vituo vya maendeleo ya mtoto na kijana zaidi ya 600.

.district_council

MATUKIO KATIKA PICHAZiara ya Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini, Bw. Emmanuel Kihampa katika Kituo cha Maendeleo ya Mto...
01/06/2026

MATUKIO KATIKA PICHA

Ziara ya Msajili wa Jumuiya za Kiraia nchini, Bw. Emmanuel Kihampa katika Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana kinachosimamiwa na Kanisa la Baptist Longido mkoani Arusha kwa ushirikiano na Compassion International Tanzania (CIT).

29/05/2026

COMPASSION YAMPONGEZA ALLY HAJI KWA KUNG’ARA AFCON U17

Kutoka mitaa ya Kigoma Ujiji hadi kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya AFCON chini ya miaka 17 nchini Morocco, golikipa wa Serengeti Boys, Ally Haji, ameendelea kuwa mfano wa ndoto zinazowezekana kupitia malezi na uwekezaji kwa watoto.

Ally ni miongoni mwa watoto wanaohudumiwa na Compassion International Tanzania kupitia Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana katika kanisa la Anglikana kilichopo Kigoma Ujiji. Ameonyesha kiwango cha juu katika michuano hiyo baada ya kudaka penalti mbili muhimu zilizoiwezesha Serengeti Boys kutinga hatua ya fainali. Uwezo wake wa kuwa imara langoni umeendelea kuwavutia mashabiki wengi wa soka ndani na nje ya Tanzania.

Compassion International Tanzania inampongeza Ally Haji kwa mafanikio haya makubwa na kwa kuiwakilisha vyema Tanzania katika mashindano ya kimataifa. Mafanikio yake yanaonyesha kuwa watoto wanapopewa malezi bora na fursa wanaweza kufikia ndoto zao na kuwa chachu ya mabadiliko katika jamii.

Tunajivunia kuona mtoto aliyepitia programu za Compassion aking’ara katika jukwaa la kimataifa na kuwa hamasa kwa watoto na vijana wengine nchini Tanzania.

Serengeti Boys wanatarajiwa kushuka dimbani siku ya Jumanne, tarehe 02 Juni 2026, kucheza mchezo wa fainali dhidi ya Senegal. Compassion International Tanzania inawatakia Ally Haji na timu nzima ya Serengeti Boys kila la heri wanapoendelea kuipeperusha bendera ya Tanzania.

Hongera Ally Haji! Hongera Serengeti Boys! Tanzania inajivunia mafanikio yenu. 🇹🇿⚽️

Video Credits:

MAFUNZO YA KUIMARISHA HUDUMA ZA WATOTO NA VIJANA YAFANYIKA ARUSHAZaidi ya washiriki 100 kutoka makanisa washirika wa Com...
20/05/2026

MAFUNZO YA KUIMARISHA HUDUMA ZA WATOTO NA VIJANA YAFANYIKA ARUSHA

Zaidi ya washiriki 100 kutoka makanisa washirika wa Compassion International Tanzania katika klasta za Monduli, Olmotonyi na Namanga wamekutana katika Kanisa la Zion City kwa ajili ya mafunzo maalumu ya “Esther Encounter” yaliyoandaliwa kuimarisha huduma za watoto na vijana, kuongeza mshik**ano wa makanisa na kuwajengea washiriki uwezo wa kulitumikia kanisa na jamii kwa ufanisi zaidi.

Mafunzo hayo yamewakutanisha viongozi kutoka makanisa 20 pamoja na wawezeshaji na wataalamu kutoka CIT kwa ajili ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kufufua huduma ya mtoto katika Kanda ya Ngorongoro.

Akifungua rasmi mafunzo hayo, Meneja Mwandamizi wa Ushirika Wenza, Zelote Lukumay, amesema kuwa mafanikio yenye tija katika huduma yanahitaji maombi, ushirikiano na kujitoa kwa dhati katika kazi ya Mungu.

Naye Mhe. Balozi Profesa Emmanuel Mbennah, mwanachama mwanzilishi wa CIT, amewahimiza washiriki kutumia mafunzo hayo kuleta mabadiliko chanya katika huduma za watoto na vijana ndani ya makanisa na jamii wanazozihudumia.


Zaidi ya watoto 400 kutoka kaya zenye uhitaji wamepata wafadhili na kuboreshewa makazi kupitia mbio za hisani za   ziliz...
14/05/2026

Zaidi ya watoto 400 kutoka kaya zenye uhitaji wamepata wafadhili na kuboreshewa makazi kupitia mbio za hisani za zilizofanyika Mkoani Singida.

Washiriki zaidi ya 200 kutoka Tanzania na Uholanzi waliungana katika mbio na matembezi ya hisani kuchangisha fedha za kuboresha maisha ya watoto kupitia makazi bora na huduma muhimu za maendeleo.

WATEMBEA KILOMITA 63 BILA KUPUMZIKA… NI KWA AJILI YA MTOTOSio kwa ajili ya medali.Sio kwa ajili ya mashindano.Bali kwa a...
14/05/2026

WATEMBEA KILOMITA 63 BILA KUPUMZIKA… NI KWA AJILI YA MTOTO

Sio kwa ajili ya medali.
Sio kwa ajili ya mashindano.
Bali kwa ajili ya kumrudishia mtoto matumaini ya maisha bora.

Baadhi ya Washiriki wa Muskathlon 2026 kutoka Uholanzi waliandika historia ya upendo na kujitoa baada ya kutembea kilomita 63 mjini Kisaki, Singida, wakibeba dhamira moja — kuwagusa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu nchini Tanzania.

Kwa zaidi ya mwaka mmoja walijiandaa kimwili na kiakili kukabiliana na safari hiyo ngumu, wakionesha uthubutu, mshik**ano na moyo wa kweli wa kibinadamu.

Licha ya uchovu, jua kali na safari ndefu, waliendelea kutembea huku nyuso zao zikijaa tabasamu na matumaini. Kila hatua waliyoipiga ilikuwa sauti ya upendo na msaada kwa mtoto mwenye uhitaji.

Kupitia matembezi na mbio hizi za hisani, fedha zinazokusanywa zitasaidia watoto kupata elimu, malezi na maisha bora zaidi.

Washiriki wa Muskathlon 2026 kutoka nchini Uholanzi, wakiongozana na wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Compassion Internat...
12/05/2026

Washiriki wa Muskathlon 2026 kutoka nchini Uholanzi, wakiongozana na wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Compassion International Tanzania pamoja na viongozi wa shirika hilo, wametembelea watoto na familia zao mkoani Singida k**a sehemu ya maandalizi ya matembezi na mbio za hisani zinazolenga kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Katika ziara hiyo, washiriki hao walifika kwenye vituo mbalimbali vya huduma ya mtoto na kijana vinavyoendeshwa na makanisa washirika, ambapo walipata nafasi ya kukutana na watoto pamoja na familia zao, kusikiliza simulizi za maisha yao na kujionea changamoto wanazokabiliana nazo kila siku. Aidha, wageni hao walitoa msaada wa vyakula, kushiriki maombi pamoja na familia hizo na kuonesha upendo na faraja kwa watoto wanaohudumiwa kupitia programu hiyo.
Washiriki wa Muskathlon pia walitembelea shughuli mbalimbali za ujasiriamali na kazi za mikono zinazofanywa na watoto pamoja na wazazi wao, huku wakitumia muda kucheza, kuzungumza na kufurahi pamoja nao. Wengi wao walieleza kuguswa na ushuhuda wa familia hizo na kuahidi kuendelea kushirikiana na Compassion International Tanzania katika kusaidia watoto kujikomboa kutoka kwenye mzunguko wa umaskini.

Msafara huo umeambatana na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Compassion International Tanzania akiwemo Widson Swalala, Mchungaji Dr. Elieshi Kisinza na Rebecca Muna, pamoja na viongozi waandamizi wa shirika hilo wakiongozwa na Mkurugenzi Mary Lema.

inahusisha watembeaji na wakimbiaji zaidi ya 200 wakiwemo wageni 90 kutoka nchini Uholanzi kwa lengo la kuchangisha fedha kwaajili ya watoto wenye uhitaji hapa nchini.


EndingChildPoverty

Address

Olorien Street
Arusha
P.O.BOX3064

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Compassion International Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Compassion International Tanzania:

Share