07/09/2024
*NENO LA MUNGU LI HAI*_
_*TENA LINA NGUVU*_
_*(WAEBRANIA 4:12).*_
*2 YOHANA 1:9&10*
9 Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia.
10 Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.
Mpendwa jifunze;
■ *Kudumu katika mafundisho ya Yesu Kristo.*
■ *Usikaribishe moyoni mwako mafundisho ya uongo.*
Mpendwa,
1.Je, wewe umepokea
mafundisho ya Yesu Kristo?
2.Je, wewe umewasaidia
wengine kumjua Kristo
kupitia mafundisho
yake?
*TAFAKARI*
Mpendwa, kila fundisho lililojengwa kwenye msingi wa imani ya Yesu Kristo linafaa kwa mafundisho.
👉🏽Mpendwa, mafundisho ya Yesu Kristo ni neno la Mungu lililo hai lenye kuhuisha na kuponya mioyo yetu. Hufungua fahamu na uelewa wetu katika mambo yote. Linatusaidia kuijua kweli yote ya Mungu, na kutuwezesha kutembea sawa sawa na mapenzi ya Mungu. Hutupa kuambatana na Mungu sawa sawa tukifuata maagizo yake.
👉🏽Mpendwa, k**a huwezi kudumu katika kuenenda sawa sawa na neno la Mungu linavyoelekeza, ina maana Mungu hayumo ndani yako. Neno la Mungu ndilo linalotusaidia kujiepusha na uovu ili kuishi maisha matakatifu ya kumcha Mungu.
👉🏽Mpendwa, yapo mafundisho mengi nyakati hizi ambayo hayatokani na imani ya Yesu Kristo. K**a hujaweka mizizi yako sawa sawa ndani ya Yesu yanakuyumbisha. Mpendwa anza kwa kujenga msingi wako wa imani ndani ya *YESU KRISTO* kwa kumwamini kuwa *BWANA NA MWOKOZI* wa maisha yako. Yesu atakusamehe dhambi zako zote na kukupa uzima wa milele. Atakupa na Roho Mtakatifu atakayekuwa Msaidizi wako.
*2 TIMOTHEO 3:16.*
*16. Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;*
*Omba sala hii;*
👉🏽 _Eee Bwana Yesu, naomba unisamehe dhambi zangu zote, ninatubu kwako. Nimefungua moyo wangu ingia ndani yangu sas